Zaburi BSB

Zaburi 88

Psalms Chapter 88

1
Ee Bwana, Mungu wa wokovu wangu Mchana na usiku nimelia mbele zako.
A song. A Psalm of the sons of Korah. For the choirmaster. According to Mahalath Leannoth. A Maskil of Heman the Ezrahite. O LORD, the God of my salvation, day and night I cry out before You.
2
Maombi yangu yafike mbele zako, Uutegee ukelele wangu sikio lako.
May my prayer come before You; incline Your ear to my cry.
3
Maana nafsi yangu imeshiba taabu, Na uhai wangu umekaribia kuzimu.
For my soul is full of troubles, and my life draws near to Sheol.
4
Nimehesabiwa pamoja nao washukao shimoni; Nimekuwa kama mtu asiye na msaada.
I am counted among those descending to the Pit. I am like a man without strength.
5
Miongoni mwao waliokufa nimetupwa, Kama waliouawa walalao makaburini. Hao ambao Wewe huwakumbuki tena, Wametengwa mbali na mkono wako.
I am forsaken among the dead, like the slain who lie in the grave, whom You remember no more, who are cut off from Your care.
6
Mimi umenilaza katika shimo la chini, Katika mahali penye giza vilindini.
You have laid me in the lowest Pit, in the darkest of the depths.
7
Ghadhabu yako imenilemea, Umenitesa kwa mawimbi yako yote.
Your wrath weighs heavily upon me; all Your waves have submerged me. Selah
8
Wanijuao umewatenga nami; Umenifanya kuwa chukizo kwao; Nimefungwa wala siwezi kutoka.
You have removed my friends from me; You have made me repulsive to them; I am confined and cannot escape.
9
Jicho langu limefifia kwa ajili ya mateso Bwana, nimekuita kila siku; Nimekunyoshea Wewe mikono yangu.
My eyes grow dim with grief. I call to You daily, O LORD; I spread out my hands to You.
10
Wafu je! Utawafanyia miujiza? Au waliofariki watasimama na kukuhimidi?
Do You work wonders for the dead? Do departed spirits rise up to praise You? Selah
11
Fadhili zako zitasimuliwa kaburini? Au uaminifu wako katika uharibifu?
Can Your loving devotion be proclaimed in the grave, Your faithfulness in Abaddon?
12
Miujiza yako itajulikana gizani? Au haki yako katika nchi ya usahaulifu?
Will Your wonders be known in the darkness, or Your righteousness in the land of oblivion?
13
Lakini mimi nimekulilia Wewe, Bwana, Na asubuhi maombi yangu yatakuwasilia.
But to You, O LORD, I cry for help; in the morning my prayer comes before You.
14
Bwana, kwa nini kuitupa nafsi yangu, Na kunificha uso wako?
Why, O LORD, do You reject me? Why do You hide Your face from me?
15
Nateswa mimi hali ya kufa tangu ujana, Nimevumilia vitisho vyako na kufadhaika.
From my youth I was afflicted and near death. I have borne Your terrors; I am in despair.
16
Hasira zako kali zimepita juu yangu, Maogofyo yako yameniangamiza.
Your wrath has swept over me; Your terrors have destroyed me.
17
Yamenizunguka kama maji mchana kutwa, Yamenisonga yote pamoja.
All day long they engulf me like water; they enclose me on every side.
18
Mpenzi na rafiki umewatenga nami, Nao wanijuao wamo gizani.
You have removed my beloved and my friend; darkness is my closest companion.

Chagua Sura