Zaburi 14

Psalms Chapter 14

Download Audio (Pakua)
« Orodha ya Sura
English Translation
1
Mpumbavu amesema moyoni, Hakuna Mungu; Wameharibu matendo yao na kuyafanya chukizo, Hakuna atendaye mema.
> The fool has said in his heart, "There is no God." They are corrupt. They have done abominable works. There is none who does good.
2
Toka mbinguni Bwana aliwachungulia wanadamu, Aone kama yuko mtu mwenye akili, Amtafutaye Mungu.
Yahweh looked down from heaven on the children of men, To see if there were any who did understand, Who did seek after God.
3
Wote wamepotoka, wameoza wote pamoja, Hakuna atendaye mema, La! Hata mmoja.
They have all gone aside. They have together become corrupt. There is none who does good, no, not one.
4
Je! Wote wafanyao maovu hawajui? Walao watu wangu kama walavyo mkate, Hawamwiti Bwana.
Have all the workers of iniquity no knowledge, Who eat up my people as they eat bread, And don't call on Yahweh?
5
Hapo ndipo walipoingiwa na hofu nyingi, Maana Mungu yupo pamoja na kizazi cha haki.
There they were in great fear, For God is in the generation of the righteous.
6
Mnalitia aibu shauri la mtu mnyonge, Bali Bwana ndiye aliye kimbilio lake.
You frustrate the plan of the poor, Because Yahweh is his refuge.
7
Laiti wokovu wa Israeli utoke katika Sayuni! Bwana awarudishapo wafungwa wa watu wake; Yakobo atashangilia, Israeli atafurahi.
Oh that the salvation of Israel would come out of Zion! When Yahweh restores the fortunes of his people, Then Jacob shall rejoice, and Israel shall be glad.
« 13 15 »

Chagua Sura Nyingine (Select Chapter)