Zaburi BSB

Zaburi 30

Psalms Chapter 30

1
Ee Bwana, nitakutukuza kwa maana umeniinua, Wala hukuwafurahisha adui zangu juu yangu.
A Psalm. A song for the dedication of the temple. Of David. I will exalt You, O LORD, for You have lifted me up and have not allowed my foes to rejoice over me.
2
Ee Bwana, Mungu wangu, Nalikulilia ukaniponya.
O LORD my God, I cried to You for help, and You healed me.
3
Umeniinua nafsi yangu, Ee Bwana, kutoka kuzimu. Umenihuisha na kunitoa Miongoni mwao washukao shimoni.
O LORD, You pulled me up from Sheol; You spared me from descending into the Pit.
4
Mwimbieni Bwana zaburi, Enyi watauwa wake. Na kufanya shukrani. Kwa kumbukumbu la utakatifu wake.
Sing to the LORD, O you His saints, and praise His holy name.
5
Maana ghadhabu zake ni za kitambo kidogo, Katika radhi yake mna uhai. Huenda kilio huja kukaa usiku, Lakini asubuhi huwa furaha.
For His anger is fleeting, but His favor lasts a lifetime. Weeping may stay the night, but joy comes in the morning.
6
Nami nilipofanikiwa nalisema, Sitaondoshwa milele.
In prosperity I said, “I will never be shaken.”
7
Bwana, kwa radhi yako Wewe uliuimarisha mlima wangu. Uliuficha uso wako, Nami nikafadhaika.
O LORD, You favored me; You made my mountain stand strong. When You hid Your face, I was dismayed.
8
Ee Bwana, nalikulilia Wewe, Naam, kwa Bwana naliomba dua.
To You, O LORD, I called, and I begged my Lord for mercy:
9
Mna faida gani katika damu yangu Nishukapo shimoni? Mavumbi yatakusifu? Yataitangaza kweli yako?
“What gain is there in my bloodshed, in my descent to the Pit? Will the dust praise You? Will it proclaim Your faithfulness?
10
Ee Bwana, usikie, unirehemu, Bwana, uwe msaidizi wangu.
Hear me, O LORD, and have mercy; O LORD, be my helper.”
11
Uligeuza matanga yangu kuwa machezo; Ulinivua gunia, ukanivika furaha.
You turned my mourning into dancing; You peeled off my sackcloth and clothed me with joy,
12
Ili utukufu wangu ukusifu, Wala usinyamaze. Ee Bwana, Mungu wangu, Nitakushukuru milele.
that my heart may sing Your praises and not be silent. O LORD my God, I will give thanks forever.

Chagua Sura