Zaburi 30 Swahili & English
Listen/Download AudioZaburi 30 (Swahili) | Psalms 30 (English) |
---|---|
Ee Bwana, nitakutukuza kwa maana umeniinua, Wala hukuwafurahisha adui zangu juu yangu. Zaburi 30:1 |
> I will extol you, Yahweh, for you have raised me up, And have not made my foes to rejoice over me. |
Ee Bwana, Mungu wangu, Nalikulilia ukaniponya. Zaburi 30:2 |
Yahweh my God, I cried to you, And you have healed me. |
Umeniinua nafsi yangu, Ee Bwana, kutoka kuzimu. Umenihuisha na kunitoa Miongoni mwao washukao shimoni. Zaburi 30:3 |
Yahweh, you have brought up my soul from Sheol. You have kept me alive, that I should not go down to the pit. |
Mwimbieni Bwana zaburi, Enyi watauwa wake. Na kufanya shukrani. Kwa kumbukumbu la utakatifu wake. Zaburi 30:4 |
Sing praise to Yahweh, you saints of his. Give thanks to his holy name. |
Maana ghadhabu zake ni za kitambo kidogo, Katika radhi yake mna uhai. Huenda kilio huja kukaa usiku, Lakini asubuhi huwa furaha. Zaburi 30:5 |
For his anger is but for a moment; His favor is for a lifetime. Weeping may stay for the night, But joy comes in the morning. |
Nami nilipofanikiwa nalisema, Sitaondoshwa milele. Zaburi 30:6 |
As for me, I said in my prosperity, "I shall never be moved." |
Bwana, kwa radhi yako Wewe uliuimarisha mlima wangu. Uliuficha uso wako, Nami nikafadhaika. Zaburi 30:7 |
You, Yahweh, when you favored me, made my mountain to stand strong. But when you hid your face, I was troubled. |
Ee Bwana, nalikulilia Wewe, Naam, kwa Bwana naliomba dua. Zaburi 30:8 |
I cried to you, Yahweh. To Yahweh I made supplication: |
Mna faida gani katika damu yangu Nishukapo shimoni? Mavumbi yatakusifu? Yataitangaza kweli yako? Zaburi 30:9 |
"What profit is there in my destruction, if I go down to the pit? Shall the dust praise you? Shall it declare your truth? |
Ee Bwana, usikie, unirehemu, Bwana, uwe msaidizi wangu. Zaburi 30:10 |
Hear, Yahweh, and have mercy on me. Yahweh, be my helper." |
Uligeuza matanga yangu kuwa machezo; Ulinivua gunia, ukanivika furaha. Zaburi 30:11 |
You have turned my mourning into dancing for me. You have removed my sackcloth, and clothed me with gladness, |
Ili utukufu wangu ukusifu, Wala usinyamaze. Ee Bwana, Mungu wangu, Nitakushukuru milele. Zaburi 30:12 |
To the end that my heart may sing praise to you, and not be silent. Yahweh my God, I will give thanks to you forever! |