Zaburi 72 Swahili & English
Listen/Download AudioZaburi 72 (Swahili) | Psalms 72 (English) |
---|---|
Ee Mungu, mpe mfalme hukumu zako, Na mwana wa mfalme haki yako. Zaburi 72:1 |
> God, give the king your justice; Your righteousness to the royal son. |
Atawaamua watu wako kwa haki, Na watu wako walioonewa kwa hukumu. Zaburi 72:2 |
He will judge your people with righteousness, And your poor with justice. |
Milima itawazalia watu amani, Na vilima navyo kwa haki. Zaburi 72:3 |
The mountains shall bring prosperity to the people. The hills bring the fruit of righteousness. |
Atawahukumu walioonewa wa watu, Atawaokoa wahitaji, atamseta mwenye kuonea. Zaburi 72:4 |
He will judge the poor of the people. He will save the children of the needy, And will break the oppressor in pieces. |
Watakuogopa wakati wote wa kudumu jua, Na wakati wa kung'aa mwezi kizazi hata kizazi. Zaburi 72:5 |
They shall fear you while the sun endures; And as long as the moon, throughout all generations. |
Atashuka kama mvua juu ya majani yaliyokatwa, Kama manyunyu yainyweshayo nchi. Zaburi 72:6 |
He will come down like rain on the mown grass, As showers that water the earth. |
Siku zake yeye, mtu mwenye haki atasitawi, Na wingi wa amani hata mwezi utakapokoma. Zaburi 72:7 |
In his days, the righteous shall flourish, And abundance of peace, until the moon is no more. |
Na awe na enzi toka bahari hata bahari, Toka Mto hata miisho ya dunia. Zaburi 72:8 |
He shall have dominion also from sea to sea, From the River to the ends of the earth. |
Wakaao jangwani na wainame mbele zake; Adui zake na warambe mavumbi. Zaburi 72:9 |
Those who dwell in the wilderness shall bow before him. His enemies shall lick the dust. |
Wafalme wa Tarshishi na visiwa na walete kodi; Wafalme wa Sheba na Seba na watoe vipawa. Zaburi 72:10 |
The kings of Tarshish and of the isles will bring tribute. The kings of Sheba and Seba shall offer gifts. |
Naam, wafalme wote na wamsujudie; Na mataifa yote wamtumikie. Zaburi 72:11 |
Yes, all kings shall fall down before him. All nations shall serve him. |
Kwa maana atamkomboa mhitaji aliapo, Na mtu aliyeonewa iwapo hana msaidizi. Zaburi 72:12 |
For he will deliver the needy when he cries; The poor, who has no helper. |
Atamhurumia aliye dhaifu na maskini, Na nafsi za wahitaji ataziokoa. Zaburi 72:13 |
He will have pity on the poor and needy. He will save the souls of the needy. |
Atawakomboa nafsi zao na kuonewa na udhalimu, Na damu yao ina thamani machoni pake. Zaburi 72:14 |
He will redeem their soul from oppression and violence. Their blood will be precious in his sight. |
Basi na aishi; Na wampe dhahabu ya Sheba; Na wamwombee daima; Na kumbariki mchana kutwa. Zaburi 72:15 |
They shall live, and to him shall be given of the gold of Sheba. Men shall pray for him continually. They shall bless him all day long. |
Na uwepo wingi wa nafaka Katika ardhi juu ya milima; Matunda yake na yawaye-waye kama Lebanoni, Na watu wa mjini wasitawi kama majani ya nchi. Zaburi 72:16 |
There shall be abundance of grain throughout the land. Its fruit sways like Lebanon. Let it flourish, thriving like the grass of the field. |
Jina lake na lidumu milele, Pindi ling'aapo jua jina lake liwe na wazao; Mataifa yote na wajibariki katika yeye, Na kumwita heri. Zaburi 72:17 |
His name endures forever. His name continues as long as the sun. Men shall be blessed by him. All nations will call him blessed. |
Na ahimidiwe Bwana, Mungu, Mungu wa Israeli, Atendaye miujiza Yeye peke yake; Zaburi 72:18 |
Praise be to Yahweh God, the God of Israel, Who alone does marvelous deeds. |
Jina lake tukufu na lihimidiwe milele; Dunia yote na ijae utukufu wake. Amina na Amina. Zaburi 72:19 |
Blessed be his glorious name forever! Let the whole earth be filled with his glory! Amen and amen. |
Maombi ya Daudi mwana wa Yese yamekwisha. Zaburi 72:20 |
This ends the prayers by David, the son of Jesse. |