1
Enyi watu wangu, sikilizeni sheria yangu, Tegeni masikio kwa maneno ya kinywa changu.
A Maskil of Asaph. Give ear, O my people, to my instruction; listen to the words of my mouth.
2
Na nifunue kinywa changu kwa mithali, Niyatamke mafumbo ya kale.
I will open my mouth in parables; I will utter things hidden from the beginning,
3
Mambo tuliyoyasikia na kuyafahamu, Ambayo baba zetu walituambia.
that we have heard and known and our fathers have relayed to us.
4
Hayo hatutawaficha wana wao, Huku tukiwaambia kizazi kingine, Sifa za Bwana, na nguvu zake, Na mambo yake ya ajabu aliyoyafanya.
We will not hide them from their children but will declare to the next generation the praises of the LORD and His might and the wonders He has performed.
5
Maana alikaza ushuhuda katika Yakobo, Na sheria aliiweka katika Israeli. Aliyowaamuru baba zetu Wawajulishe wana wao,
For He established a testimony in Jacob and appointed a law in Israel, which He commanded our fathers to teach to their children,
6
Ili kizazi kingine wawe na habari, Ndio hao wana watakaozaliwa. Wasimame na kuwaambia wana wao
that the coming generation would know them—even children yet to be born—to arise and tell their own children
7
Wamwekee Mungu tumaini lao. Wala wasiyasahau matendo ya Mungu, Bali wazishike amri zake.
that they should put their confidence in God, not forgetting His works, but keeping His commandments.
8
Naam, wasiwe kama baba zao, Kizazi cha ukaidi na uasi. Kizazi kisichojitengeneza moyo, Wala roho yake haikuwa amini kwa Mungu.
Then they will not be like their fathers, a stubborn and rebellious generation, whose heart was not loyal, whose spirit was not faithful to God.
9
Wale Waefraimu, wenye silaha, wapiga upinde, Walirudi nyuma siku ya vita.
The archers of Ephraim turned back on the day of battle.
10
Hawakulishika agano la Mungu; Wakakataa kuenenda katika sheria yake;
They failed to keep God’s covenant and refused to live by His law.
11
Wakayasahau matendo yake, Na mambo yake ya ajabu aliyowaonyesha.
They forgot what He had done, the wonders He had shown them.
12
Mbele ya baba zao alifanya mambo ya ajabu, Katika nchi ya Misri, konde la Soani.
He worked wonders before their fathers in the land of Egypt, in the region of Zoan.
13
Aliipasua bahari akawavusha; Aliyasimamisha maji mfano wa chungu.
He split the sea and brought them through; He set the waters upright like a wall.
14
Akawaongoza kwa wingu mchana, Na usiku kucha kwa nuru ya moto.
He led them with a cloud by day and with a light of fire all night.
15
Akapasua miamba jangwani; Akawanywesha maji mengi kama maji ya vilindi.
He split the rocks in the wilderness and gave them drink as abundant as the seas.
16
Akatokeza na vijito gengeni, Akatelemsha maji kama mito.
He brought streams from the stone and made water flow down like rivers.
17
Lakini wakazidi kumtenda dhambi, Walipomwasi Aliye juu katika nchi ya kiu.
But they continued to sin against Him, rebelling in the desert against the Most High.
18
Wakamjaribu Mungu mioyoni mwao Kwa kutaka chakula kwa tamaa zao.
They willfully tested God by demanding the food they craved.
19
Naam, walimwamba Mungu, wakasema, Je! Mungu aweza kuandika meza jangwani?
They spoke against God, saying, “Can God really prepare a table in the wilderness?
20
Tazama, aliupiga mwamba; Maji yakabubujika, ikafurika mito. Pia aweza kutupa chakula? Atawaandalia watu wake nyama?
When He struck the rock, water gushed out and torrents raged. But can He also give bread or supply His people with meat?”
21
Hivyo Bwana aliposikia akaghadhibika; Moto ukawashwa juu ya Yakobo, Hasira nayo ikapanda juu ya Israeli.
Therefore the LORD heard and was filled with wrath; so a fire was kindled against Jacob, and His anger flared against Israel,
22
Kwa kuwa hawakumwamini Mungu, Wala hawakuutumainia wokovu wake.
because they did not believe God or rely on His salvation.
23
Lakini aliyaamuru mawingu juu; Akaifungua milango ya mbinguni;
Yet He commanded the clouds above and opened the doors of the heavens.
24
Akawanyeshea mana ili wale; Akawapa nafaka ya mbinguni.
He rained down manna for them to eat; He gave them grain from heaven.
25
Mwanadamu akala chakula cha mashujaa; Aliwapelekea chakula cha kuwashibisha.
Man ate the bread of angels; He sent them food in abundance.
26
Aliuelekeza upepo wa mashariki mbinguni; Akaiongoza kusi kwa uweza wake.
He stirred the east wind from the heavens and drove the south wind by His might.
27
Akawanyeshea nyama kama mavumbi, Na ndege wenye mbawa, Kama mchanga wa bahari.
He rained meat on them like dust, and winged birds like the sand of the sea.
28
Akawaangusha kati ya matuo yao, Pande zote za maskani zao.
He felled them in the midst of their camp, all around their dwellings.
29
Wakala wakashiba sana; Maana aliwaletea walivyovitamani;
So they ate and were well filled, for He gave them what they craved.
30
Hawakuachana na matakwa yao. Ila chakula chao kikali ki vinywani mwao
Yet before they had filled their desire, with the food still in their mouths,
31
Hasira ya Mungu ikapanda juu yao, Akawaua waliokuwa wanono; Akawaangusha chini vijana wa Israeli.
God’s anger flared against them, and He put to death their strongest and subdued the young men of Israel.
32
Pamoja na hayo wakazidi kutenda dhambi, Wala hawakuyaamini matendo yake ya ajabu.
In spite of all this, they kept on sinning; despite His wonderful works, they did not believe.
33
Kwa hiyo akazikomesha siku zao kama pumzi, Na miaka yao kwa hofu ya kuwasitusha.
So He ended their days in futility, and their years in sudden terror.
34
Alipowaua ndipo walipokuwa wakimtafuta; Wakarudi wakamtaka Mungu kwa bidii.
When He slew them, they would seek Him; they repented and searched for God.
35
Wakakumbuka kuwa Mungu ni mwamba wao, Na Mungu Aliye juu ni mkombozi wao.
And they remembered that God was their Rock, that God Most High was their Redeemer.
36
Lakini walimdanganya kwa vinywa vyao, Wakamwambia uongo kwa ndimi zao.
But they deceived Him with their mouths, and lied to Him with their tongues.
37
Kwa maana mioyo yao haikuwa thabiti kwake, Wala hawakuwa waaminifu katika agano lake.
Their hearts were disloyal to Him, and they were unfaithful to His covenant.
38
Lakini Yeye, kwa kuwa anayo rehema, Husamehe uovu wala haangamizi. Mara nyingi huipishia mbali ghadhabu yake, Wala haiwashi hasira yake yote.
And yet He was compassionate; He forgave their iniquity and did not destroy them. He often restrained His anger and did not unleash His full wrath.
39
Akakumbuka ya kuwa wao ni kiwiliwili, Upepo upitao wala haurudi.
He remembered that they were but flesh, a passing breeze that does not return.
40
Walimwasi jangwani mara ngapi? Na kumhuzunisha nyikani!
How often they disobeyed Him in the wilderness and grieved Him in the desert!
41
Wakarudi nyuma wakamjaribu Mungu; Wakampa mpaka Mtakatifu wa Israeli.
Again and again they tested God and provoked the Holy One of Israel.
42
Hawakuukumbuka mkono wake, Wala siku ile alipowakomboa na mtesi.
They did not remember His power—the day He redeemed them from the adversary,
43
Alivyoziweka ishara zake katika Misri, Na miujiza yake katika konde la Soani.
when He performed His signs in Egypt and His wonders in the fields of Zoan.
44
Aligeuza damu mito yao, Na vijito wasipate kunywa.
He turned their rivers to blood, and from their streams they could not drink.
45
Aliwapelekea mainzi wakawala, Na vyura wakawaharibu.
He sent swarms of flies that devoured them, and frogs that devastated them.
46
Akawapa tunutu mazao yao, Na nzige kazi yao.
He gave their crops to the grasshopper, the fruit of their labor to the locust.
47
Aliiharibu mizabibu yao kwa mvua ya mawe, Na mikuyu yao kwa mawe ya barafu.
He killed their vines with hailstones and their sycamore-figs with sleet.
48
Akaacha ng'ombe zao wapigwe kwa mvua ya mawe, Na makundi yao kwa umeme.
He abandoned their cattle to the hail and their livestock to bolts of lightning.
49
Akawapelekea ukali wa hasira yake, Ghadhabu, na uchungu, na taabu, Kundi la malaika waletao mabaya.
He unleashed His fury against them, wrath, indignation, and calamity—a band of destroying angels.
50
Akiifanyizia njia hasira yake; Wala hakuziepusha roho zao na mauti, Bali aliiachia tauni uhai wao;
He cleared a path for His anger; He did not spare them from death but delivered their lives to the plague.
51
Akampiga kila mzaliwa wa kwanza wa Misri, Malimbuko ya nguvu katika hema za Hamu.
He struck all the firstborn of Egypt, the virility in the tents of Ham.
52
Bali aliwaongoza watu wake kama kondoo, Akawachunga kama kundi jangwani.
He led out His people like sheep and guided them like a flock in the wilderness.
53
Hao akawachukua salama wala hawakuogopa, Bali bahari iliwafunikiza adui zao.
He led them safely, so they did not fear, but the sea engulfed their enemies.
54
Akawapeleka hadi mpaka wake mtakatifu, Mlima alioununua kwa mkono wake wa kuume.
He brought them to His holy land, to the mountain His right hand had acquired.
55
Akawafukuza mataifa mbele yao, Akawapimia urithi kwa kamba, Na kuwakalisha kabila za Israeli katika hema zao.
He drove out nations before them and apportioned their inheritance; He settled the tribes of Israel in their tents.
56
Lakini walimjaribu Mungu Aliye juu, wakamwasi, Wala hawakuzishika shuhuda zake.
But they tested and disobeyed God Most High, for they did not keep His decrees.
57
Bali walirudi nyuma, wakahaini kama baba zao; Wakaepea kama upinde usiofaa.
They turned back and were faithless like their fathers, twisted like a faulty bow.
58
Wakamkasirisha kwa mahali pao pa juu, Wakamtia wivu kwa sanamu zao.
They enraged Him with their high places and provoked His jealousy with their idols.
59
Mungu akasikia, akaghadhibika, Akamkataa Israeli kabisa.
On hearing it, God was furious and rejected Israel completely.
60
Akaiacha maskani ya Shilo, Hema aliyoiweka katikati ya wanadamu;
He abandoned the tabernacle of Shiloh, the tent He had pitched among men.
61
Akaziacha nguvu zake kutekwa, Na fahari yake mkononi mwa mtesi.
He delivered His strength to captivity, and His splendor to the hand of the adversary.
62
Akawatoa watu wake wapigwe kwa upanga; Akaughadhibikia urithi wake.
He surrendered His people to the sword because He was enraged by His heritage.
63
Moto ukawala vijana wao, Wanawali wao hawakuimbiwa nyimbo za arusi,
Fire consumed His young men, and their maidens were left without wedding songs.
64
Makuhani wao walianguka kwa upanga, Wala wajane wao hawakuomboleza.
His priests fell by the sword, but their widows could not lament.
65
Ndipo Bwana alipoamka kama aliyelala usingizi, Kama shujaa apigaye kelele sababu ya mvinyo;
Then the Lord awoke as from sleep, like a mighty warrior overcome by wine.
66
Akawapiga watesi wake akawarudisha nyuma, Akawatia aibu ya milele.
He beat back His foes; He put them to everlasting shame.
67
Ila akaikataa hema ya Yusufu; Wala hakuichagua kabila ya Efraimu.
He rejected the tent of Joseph and refused the tribe of Ephraim.
68
Bali aliichagua kabila ya Yuda, Mlima Sayuni alioupenda.
But He chose the tribe of Judah, Mount Zion, which He loved.
69
Akajenga patakatifu pake kama vilele, Kama dunia aliyoiweka imara milele.
He built His sanctuary like the heights, like the earth He has established forever.
70
Akamchagua Daudi, mtumishi wake, Akamwondoa katika mazizi ya kondoo.
He chose David His servant and took him from the sheepfolds;
71
Nyuma ya kondoo wanyonyeshao alimwondoa, Awachunge Yakobo watu wake, na Israeli urithi wake.
from tending the ewes He brought him to be shepherd of His people Jacob, of Israel His inheritance.
72
Akawalisha kwa ukamilifu wa moyo wake, Na kuwaongoza kwa busara ya mikono yake.
So David shepherded them with integrity of heart and guided them with skillful hands.
Chagua Sura
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28
29
30
31
32
33
34
35
36
37
38
39
40
41
42
43
44
45
46
47
48
49
50
51
52
53
54
55
56
57
58
59
60
61
62
63
64
65
66
67
68
69
70
71
72
73
74
75
76
77
78
79
80
81
82
83
84
85
86
87
88
89
90
91
92
93
94
95
96
97
98
99
100
101
102
103
104
105
106
107
108
109
110
111
112
113
114
115
116
117
118
119
120
121
122
123
124
125
126
127
128
129
130
131
132
133
134
135
136
137
138
139
140
141
142
143
144
145
146
147
148
149
150