Zaburi 132 Swahili & English

Listen/Download Audio
Zaburi 132 (Swahili) Psalms 132 (English)

Bwana, umkumbukie Daudi Taabu zake zote alizotaabika. Zaburi 132:1

> Yahweh, remember David and all his affliction,

Ndiye aliyemwapia Bwana, Akaweka nadhiri kwa Shujaa wa Yakobo. Zaburi 132:2

How he swore to Yahweh, And vowed to the Mighty One of Jacob:

Sitaingia hemani mwa nyumba yangu, Wala sitapanda matandiko ya kitanda changu; Zaburi 132:3

"Surely I will not come into the structure of my house, Nor go up into my bed;

Sitaacha macho yangu kuwa na usingizi, Wala kope zangu kusinzia; Zaburi 132:4

I will not give sleep to my eyes, Or slumber to my eyelids;

Hata nitakapompatia Bwana mahali, Na Shujaa wa Yakobo maskani. Zaburi 132:5

Until I find out a place for Yahweh, A dwelling for the Mighty One of Jacob."

Tazama, tulisikia habari zake katika Efrata, Katika konde la Yearimu tuliiona. Zaburi 132:6

Behold, we heard of it in Ephrathah. We found it in the field of Jaar:

Na tuingie katika maskani yake, Tusujudu penye kiti cha kuwekea miguu yake. Zaburi 132:7

"We will go into his dwelling place. We will worship at his footstool.

Ee Bwana, uinuke, uende kwenye raha yako, Wewe na sanduku la nguvu zako. Zaburi 132:8

Arise, Yahweh, into your resting place; You, and the ark of your strength.

Makuhani wako na wavikwe haki, Watauwa wako na washangilie. Zaburi 132:9

Let your priest be clothed with righteousness. Let your saints shout for joy!"

Kwa ajili ya Daudi, mtumishi wako, Usiurudishe nyuma uso wa masihi Zaburi 132:10

For your servant David's sake, Don't turn away the face of your anointed one.

Bwana amemwapia Daudi neno la kweli, Hatarudi nyuma akalihalifu, Baadhi ya wazao wa mwili wako Nitawaweka katika kiti chako cha enzi. Zaburi 132:11

Yahweh has sworn to David in truth. He will not turn from it: "I will set the fruit of your body on your throne.

Wanao wakiyashika maagano yangu, Na shuhuda nitakazowafundisha; Watoto wao nao wataketi Katika kiti chako cha enzi milele. Zaburi 132:12

If your children will keep my covenant, My testimony that I will teach them, Their children also will sit on your throne forevermore."

Kwa kuwa Bwana ameichagua Sayuni, Ameitamani akae ndani yake. Zaburi 132:13

For Yahweh has chosen Zion. He has desired it for his habitation.

Hapo ndipo mahali pangu pa raha milele, Hapo nitakaa kwa maana nimepatamani. Zaburi 132:14

"This is my resting place forever. Here I will live, for I have desired it.

Hakika nitavibariki vyakula vyake Wahitaji wake nitawashibisha chakula. Zaburi 132:15

I will abundantly bless her provision. I will satisfy her poor with bread.

Na makuhani wake nitawavika wokovu, Na watauwa wake watashangilia. Zaburi 132:16

Her priests I will also clothe with salvation. Her saints will shout aloud for joy.

Hapo nitamchipushia Daudi pembe, Na taa nimemtengenezea masihi wangu. Zaburi 132:17

There I will make the horn of David to bud. I have ordained a lamp for my anointed.

Adui zake nitawavika aibu, Bali juu yake taji yake itasitawi. Zaburi 132:18

I will clothe his enemies with shame, But on himself, his crown will be resplendant."