Zaburi 26

Psalms Chapter 26

Download Audio (Pakua)
« Orodha ya Sura
English Translation
1
Ee Bwana, unihukumu mimi, Maana nimekwenda kwa ukamilifu wangu, Nami nimemtumaini Bwana bila wasiwasi.
> Judge me, Yahweh, for I have walked in my integrity. I have trusted also in Yahweh without wavering.
2
Ee Bwana, unijaribu na kunipima; Unisafishe mtima wangu na moyo wangu.
Examine me, Yahweh, and prove me. Try my heart and my mind.
3
Maana fadhili zako zi mbele ya macho yangu, Nami nimekwenda katika kweli yako.
For your loving kindness is before my eyes. I have walked in your truth.
4
Sikuketi pamoja na watu wa ubatili, Wala sitaingia mnamo wanafiki.
I have not sat with deceitful men, Neither will I go in with hypocrites.
5
Nimelichukia kusanyiko la watenda mabaya, Wala sitaketi pamoja na watu waovu.
I hate the assembly of evil-doers, And will not sit with the wicked.
6
Nitanawa mikono yangu kwa kutokuwa na hatia, Na kuizunguka madhabahu yako, Ee Bwana
I will wash my hands in innocence, So I will go about your altar, Yahweh;
7
Ili niitangaze sauti ya kushukuru, Na kuzisimulia kazi zako za ajabu.
That I may make the voice of thanksgiving to be heard, And tell of all your wondrous works.
8
Bwana, nimependa makao ya nyumba yako, Na mahali pa maskani ya utukufu wako.
Yahweh, I love the habitation of your house, The place where your glory dwells.
9
Usiiondoe nafsi yangu pamoja na wakosaji, Wala uhai wangu pamoja na watu wa damu.
Don't gather my soul with sinners, Nor my life with bloodthirsty men;
10
Mikononi mwao mna madhara, Na mkono wao wa kuume umejaa rushwa.
In whose hands is wickedness, Their right hand is full of bribes.
11
Ila mimi nitakwenda kwa ukamilifu wangu; Unikomboe, unifanyie fadhili.
But as for me, I will walk in my integrity. Redeem me, and be merciful to me.
12
Mguu wangu umesimama palipo sawa; Katika makusanyiko nitamhimidi Bwana.
My foot stands in an even place. In the congregations I will bless Yahweh.
« 25 27 »

Chagua Sura Nyingine (Select Chapter)