Zaburi BSB

Zaburi 26

Psalms Chapter 26

1
Ee Bwana, unihukumu mimi, Maana nimekwenda kwa ukamilifu wangu, Nami nimemtumaini Bwana bila wasiwasi.
Of David. Vindicate me, O LORD! For I have walked with integrity; I have trusted in the LORD without wavering.
2
Ee Bwana, unijaribu na kunipima; Unisafishe mtima wangu na moyo wangu.
Test me, O LORD, and try me; examine my heart and mind.
3
Maana fadhili zako zi mbele ya macho yangu, Nami nimekwenda katika kweli yako.
For Your loving devotion is before my eyes, and I have walked in Your truth.
4
Sikuketi pamoja na watu wa ubatili, Wala sitaingia mnamo wanafiki.
I do not sit with deceitful men, nor keep company with hypocrites.
5
Nimelichukia kusanyiko la watenda mabaya, Wala sitaketi pamoja na watu waovu.
I hate the mob of evildoers, and refuse to sit with the wicked.
6
Nitanawa mikono yangu kwa kutokuwa na hatia, Na kuizunguka madhabahu yako, Ee Bwana
I wash my hands in innocence that I may go about Your altar, O LORD,
7
Ili niitangaze sauti ya kushukuru, Na kuzisimulia kazi zako za ajabu.
to raise my voice in thanksgiving and declare all Your wonderful works.
8
Bwana, nimependa makao ya nyumba yako, Na mahali pa maskani ya utukufu wako.
O LORD, I love the house where You dwell, the place where Your glory resides.
9
Usiiondoe nafsi yangu pamoja na wakosaji, Wala uhai wangu pamoja na watu wa damu.
Do not take my soul away with sinners, or my life with men of bloodshed,
10
Mikononi mwao mna madhara, Na mkono wao wa kuume umejaa rushwa.
in whose hands are wicked schemes, whose right hands are full of bribes.
11
Ila mimi nitakwenda kwa ukamilifu wangu; Unikomboe, unifanyie fadhili.
But I will walk with integrity; redeem me and be merciful to me.
12
Mguu wangu umesimama palipo sawa; Katika makusanyiko nitamhimidi Bwana.
My feet stand on level ground; in the congregations I will bless the LORD.

Chagua Sura