Zaburi 10 Swahili & English
Listen/Download AudioZaburi 10 (Swahili) | Psalms 10 (English) |
---|---|
Ee Bwana, kwa nini wasimama mbali? Kwani kujificha nyakati za shida? Zaburi 10:1 |
Why do you stand far off, Yahweh? Why do you hide yourself in times of trouble? |
Kwa kiburi chake asiye haki mnyonge anafuatiwa kwa ukali; Na wanaswe kwa hila zizo hizo walizoziwaza. Zaburi 10:2 |
In arrogance, the wicked hunt down the weak; They are caught in the schemes that they devise. |
Maana mdhalimu hujisifia tamaa ya nafsi yake, Na mwenye choyo humkana Bwana na kumdharau. Zaburi 10:3 |
For the wicked boasts of his heart's cravings, He blesses the greedy, and condemns Yahweh. |
Mdhalimu kwa kiburi cha uso wake Asema, Hatapatiliza. Jumla ya mawazo yake ni, Hakuna Mungu; Zaburi 10:4 |
The wicked, in the pride of his face, Has no room in his thoughts for God. |
Njia zake ni thabiti kila wakati. Hukumu zako ziko juu asizione, Adui zake wote awafyonya. Zaburi 10:5 |
His ways are prosperous at all times; He is haughty, and your laws are far from his sight: As for all his adversaries, he sneers at them. |
Asema moyoni mwake, Sitaondoshwa, Kizazi baada ya kizazi sitakuwamo taabuni. Zaburi 10:6 |
He says in his heart, "I shall not be shaken; For generations I shall have no trouble." |
Kinywa chake kimejaa laana, Na hila na dhuluma. Chini ya ulimi wake kuna madhara na uovu, Zaburi 10:7 |
His mouth is full of cursing, deceit, and oppression. Under his tongue is mischief and iniquity. |
Hukaa katika maoteo ya vijiji. Mahali pa siri humwua asiye na hatia, Macho yake humvizia mtu duni. Zaburi 10:8 |
He lies in wait near the villages. From ambushes, he murders the innocent. His eyes are secretly set against the helpless. |
Huotea faraghani kama simba pangoni, Huotea amkamate mtu mnyonge. Naam, humkamata mtu mnyonge, Akimkokota wavuni mwake. Zaburi 10:9 |
He lurks in secret as a lion in his ambush. He lies in wait to catch the helpless. He catches the helpless, when he draws him in his net. |
Hujikunyata na kuinama; Watu duni huanguka kwa nguvu zake. Zaburi 10:10 |
The helpless are crushed, they collapse, They fall under his strength. |
Asema moyoni mwake, Mungu amesahau, Auficha uso wake, haoni kamwe. Zaburi 10:11 |
He says in his heart, "God has forgotten. He hides his face. He will never see it." |
Bwana, uondoke, Ee Mungu, uuinue mkono wako, Usiwasahau wanyonge. Zaburi 10:12 |
Arise, Yahweh! God, lift up your hand! Don't forget the helpless. |
Kwani mdhalimu kumdharau Mungu. Akisema moyoni mwake, Hutapatiliza? Zaburi 10:13 |
Why does the wicked person condemn God, And say in his heart, "God won't call me into account?" |
Umeona, maana unaangalia madhara na jeuri, Uyatwae mkononi mwako. Mtu duni hukuachia nafsi yake, Maana umekuwa msaidizi wa yatima. Zaburi 10:14 |
But you do see trouble and grief; You consider it to take it into your hand. You help the victim and the fatherless. |
Uuvunje mkono wake mdhalimu, Na mbaya, uipatilize dhuluma yake, hata usiione. Zaburi 10:15 |
Break the arm of the wicked. As for the evil man, seek out his wickedness until you find none. |
Bwana ndiye Mfalme milele na milele; Mataifa wamepotea kutoka nchi yake. Zaburi 10:16 |
Yahweh is King forever and ever! The nations will perish out of his land. |
Bwana, umeisikia tamaa ya wanyonge, Utaitengeneza mioyo yao, utalitega sikio lako. Zaburi 10:17 |
Yahweh, you have heard the desire of the humble. You will prepare their heart. You will cause your ear to hear, |
Ili kumhukumu yatima naye aliyeonewa, Binadamu aliye udongo asizidi kudhulumu. Zaburi 10:18 |
To judge the fatherless and the oppressed, That man who is of the earth may terrify no more. |