Zaburi BSB

Zaburi 113

Psalms Chapter 113

1
Haleluya. Enyi watumishi wa Bwana, sifuni, Lisifuni jina la Bwana.
Hallelujah! Give praise, O servants of the LORD; praise the name of the LORD.
2
Jina la Bwana lihimidiwe Tangu leo na hata milele.
Blessed be the name of the LORD both now and forevermore.
3
Toka maawio ya jua hata machweo yake Jina la Bwana husifiwa.
From where the sun rises to where it sets, the name of the LORD is praised.
4
Bwana ni mkuu juu ya mataifa yote, Na utukufu wake ni juu ya mbingu.
The LORD is exalted over all the nations, His glory above the heavens.
5
Ni nani aliye mfano wa Bwana, Mungu wetu aketiye juu;
Who is like the LORD our God, the One enthroned on high?
6
Anyenyekeaye kutazama, Mbinguni na duniani?
He humbles Himself to behold the heavens and the earth.
7
Humwinua mnyonge kutoka mavumbini, Na kumpandisha maskini kutoka jaani.
He raises the poor from the dust and lifts the needy from the dump
8
Amketishe pamoja na wakuu, Pamoja na wakuu wa watu wake.
to seat them with nobles, with the princes of His people.
9
Huweka nyumbani mwanamke aliye tasa, Awe mama ya watoto mwenye furaha.
He settles the barren woman in her home as a joyful mother to her children. Hallelujah!

Chagua Sura