Zaburi 141 Swahili & English
Listen/Download AudioZaburi 141 (Swahili) | Psalms 141 (English) |
---|---|
Ee Bwana, nimekuita, unijie hima, Uisikie sauti yangu nikuitapo. Zaburi 141:1 |
> Yahweh, I have called on you. Come to me quickly! Listen to my voice when I call to you. |
Sala yangu ipae mbele zako kama uvumba, Kuinuliwa mikono yangu kama dhabihu ya jioni. Zaburi 141:2 |
Let my prayer be set before you like incense; The lifting up of my hands like the evening sacrifice. |
Ee Bwana, uweke mlinzi kinywani pangu, Mngojezi mlangoni pa midomo yangu. Zaburi 141:3 |
Set a watch, Yahweh, before my mouth. Keep the door of my lips. |
Usiuelekeze moyo wangu kunako jambo baya, Nisiyazoelee matendo yasiyofaa, Pamoja na watu watendao maovu; Wala nisile vyakula vyao vya anasa. Zaburi 141:4 |
Don't incline my heart to any evil thing, To practice deeds of wickedness with men who work iniquity. Don't let me eat of their delicacies. |
Mwenye haki na anipige, itakuwa fadhili; Anikemee, itakuwa kama mafuta kichwani; Kichwa changu kisikatae, Maana siachi kusali kati ya mabaya yao. Zaburi 141:5 |
Let the righteous strike me, it is kindness; Let him reprove me, it is like oil on the head; Don't let my head refuse it; Yet my prayer is always against evil deeds. |
Makadhi wao wakiangushwa kando ya genge, Watayasikia maneno yangu, maana ni matamu. Zaburi 141:6 |
Their judges are thrown down by the sides of the rock. They will hear my words, for they are well spoken. |
Kama kupasua kuni na kuzichanja juu ya nchi, Ndivyo ilivyo mifupa yetu mdomoni pa kuzimu. Zaburi 141:7 |
"As when one plows and breaks up the earth, Our bones are scattered at the mouth of Sheol." |
Macho yangu yanakuelekea Wewe, MUNGU Bwana, Nimekukimbilia Wewe, usiniache nafsi yangu. Zaburi 141:8 |
For my eyes are on you, Yahweh, the Lord. In you, I take refuge. Don't leave my soul destitute. |
Unilinde na mtego walionitegea, Na matanzi yao watendao maovu. Zaburi 141:9 |
Keep me from the snare which they have laid for me, From the traps of the workers of iniquity. |
Wabaya na waanguke katika nyavu zao wenyewe, Pindi mimi ninapopita salama. Zaburi 141:10 |
Let the wicked fall together into their own nets, While I pass by. |