Haleluya. Mshukuruni Bwana kwa kuwa ni mwema, Kwa maana fadhili zake ni za milele.
Give thanks to Yahweh, for he is good, For his loving kindness endures forever.
Israeli na aseme sasa, Ya kwamba fadhili zake ni za milele.
Let Israel now say That his loving kindness endures forever.
Mlango wa Haruni na waseme sasa, Ya kwamba fadhili zake ni za milele.
Let the house of Aaron now say That his loving kindness endures forever.
Wamchao Bwana na waseme sasa, Ya kwamba fadhili zake ni za milele.
Now let those who fear Yahweh say That his loving kindness endures forever.
Katika shida yangu nalimwita Bwana; Bwana akanijibu akaniweka panapo nafasi.
Out of my distress, I called on Yah. Yah answered me with freedom.
Bwana yuko upande wangu, sitaogopa; Mwanadamu atanitenda nini?
Yahweh is on my side. I will not be afraid. What can man do to me?
Bwana yuko upande wangu, msaidizi wangu, Kwa hiyo nitawaona wanaonichukia wameshindwa.
Yahweh is on my side among those who help me. Therefore I will look in triumph at those who hate me.
Ni heri kumkimbilia Bwana Kuliko kuwatumainia wanadamu.
It is better to take refuge in Yahweh, Than to put confidence in man.
Ni heri kumkimbilia Bwana. Kuliko kuwatumainia wakuu.
It is better to take refuge in Yahweh, Than to put confidence in princes.
Mataifa yote walinizunguka; Kwa jina la Bwana naliwakatilia mbali.
All the nations surrounded me, But in the name of Yahweh, I cut them off.
Walinizunguka, naam, walinizunguka; Kwa jina la Bwana naliwakatilia mbali.
They surrounded me, yes, they surrounded me. In the name of Yahweh I indeed cut them off.
Walinizunguka kama nyuki, Walizimika kama moto wa miibani; Kwa jina la Bwana naliwakatilia mbali.
They surrounded me like bees. They are quenched like the burning thorns. In the name of Yahweh I cut them off.
Ulinisukuma sana ili nianguke; Lakini Bwana akanisaidia.
You pushed me back hard, to make me fall, But Yahweh helped me.
Bwana ni nguvu zangu na wimbo wangu, Naye amekuwa wokovu wangu.
Yah is my strength and song. He has become my salvation.
Sauti ya furaha na wokovu Imo hemani mwao wenye haki; Mkono wa kuume wa Bwana hutenda makuu.
The voice of rejoicing and salvation is in the tents of the righteous. "The right hand of Yahweh does valiantly.
Mkono wa kuume wa Bwana umetukuzwa; Mkono wa kuume wa Bwana hutenda makuu.
The right hand of Yahweh is exalted! The right hand of Yahweh does valiantly!"
Sitakufa bali nitaishi, Nami nitayasimulia matendo ya Bwana.
I will not die, but live, And declare Yah's works.
Bwana ameniadhibu sana, Lakini hakuniacha nife.
Yah has punished me severely, But he has not given me over to death.
Nifungulieni malango ya haki, Nitaingia na kumshukuru Bwana.
Open to me the gates of righteousness. I will enter into them. I will give thanks to Yah.
Lango hili ni la Bwana, Wenye haki ndio watakaoliingia.
This is the gate of Yahweh; The righteous will enter into it.
Nitakushukuru kwa maana umenijibu, Nawe umekuwa wokovu wangu.
I will give thanks to you, for you have answered me, And have become my salvation.
Jiwe walilolikataa waashi Limekuwa jiwe kuu la pembeni.
The stone which the builders rejected has become the head of the corner.
Neno hili limetoka kwa Bwana, Nalo ni ajabu machoni petu.
This is Yahweh's doing. It is marvelous in our eyes.
Siku hii ndiyo aliyoifanya Bwana, Tutashangilia na kuifurahia.
This is the day that Yahweh has made. We will rejoice and be glad in it!
Ee Bwana, utuokoe, twakusihi; Ee Bwana, utufanikishe, twakusihi.
Save us now, we beg you, Yahweh; Yahweh, we beg you, now send prosperity.
Na abarikiwe yeye ajaye kwa jina la Bwana; Tumewabarikia toka nyumbani mwa Bwana.
Blessed is he who comes in the name of Yahweh! We have blessed you out of the house of Yahweh.
Bwana ndiye aliye Mungu, Naye ndiye aliyetupa nuru. Ifungeni dhabihu kwa kamba Pembeni mwa madhabahu.
Yahweh is God, and he has given us light. Bind the sacrifice with cords, even to the horns of the altar.
Ndiwe Mungu wangu, nami nitakushukuru, Ndiwe Mungu wangu, nami nitakutukuza.
You are my God, and I will give thanks to you. You are my God, I will exalt you.
Mshukuruni Bwana kwa kuwa ni mwema, Kwa maana fadhili zake ni za milele.
Oh give thanks to Yahweh, for he is good, For his loving kindness endures forever.