Zaburi BSB

Zaburi 118

Psalms Chapter 118

1
Haleluya. Mshukuruni Bwana kwa kuwa ni mwema, Kwa maana fadhili zake ni za milele.
Give thanks to the LORD, for He is good; His loving devotion endures forever.
2
Israeli na aseme sasa, Ya kwamba fadhili zake ni za milele.
Let Israel say, “His loving devotion endures forever.”
3
Mlango wa Haruni na waseme sasa, Ya kwamba fadhili zake ni za milele.
Let the house of Aaron say, “His loving devotion endures forever.”
4
Wamchao Bwana na waseme sasa, Ya kwamba fadhili zake ni za milele.
Let those who fear the LORD say, “His loving devotion endures forever.”
5
Katika shida yangu nalimwita Bwana; Bwana akanijibu akaniweka panapo nafasi.
In my distress I called to the LORD, and He answered and set me free.
6
Bwana yuko upande wangu, sitaogopa; Mwanadamu atanitenda nini?
The LORD is on my side; I will not be afraid. What can man do to me?
7
Bwana yuko upande wangu, msaidizi wangu, Kwa hiyo nitawaona wanaonichukia wameshindwa.
The LORD is on my side; He is my helper. Therefore I will look in triumph on those who hate me.
8
Ni heri kumkimbilia Bwana Kuliko kuwatumainia wanadamu.
It is better to take refuge in the LORD than to trust in man.
9
Ni heri kumkimbilia Bwana. Kuliko kuwatumainia wakuu.
It is better to take refuge in the LORD than to trust in princes.
10
Mataifa yote walinizunguka; Kwa jina la Bwana naliwakatilia mbali.
All the nations surrounded me, but in the name of the LORD I cut them off.
11
Walinizunguka, naam, walinizunguka; Kwa jina la Bwana naliwakatilia mbali.
They surrounded me on every side, but in the name of the LORD I cut them off.
12
Walinizunguka kama nyuki, Walizimika kama moto wa miibani; Kwa jina la Bwana naliwakatilia mbali.
They swarmed around me like bees, but they were extinguished like burning thorns; in the name of the LORD I cut them off.
13
Ulinisukuma sana ili nianguke; Lakini Bwana akanisaidia.
I was pushed so hard I was falling, but the LORD helped me.
14
Bwana ni nguvu zangu na wimbo wangu, Naye amekuwa wokovu wangu.
The LORD is my strength and my song, and He has become my salvation.
15
Sauti ya furaha na wokovu Imo hemani mwao wenye haki; Mkono wa kuume wa Bwana hutenda makuu.
Shouts of joy and salvation resound in the tents of the righteous: “The right hand of the LORD performs with valor!
16
Mkono wa kuume wa Bwana umetukuzwa; Mkono wa kuume wa Bwana hutenda makuu.
The right hand of the LORD is exalted! The right hand of the LORD performs with valor!”
17
Sitakufa bali nitaishi, Nami nitayasimulia matendo ya Bwana.
I will not die, but I will live and proclaim what the LORD has done.
18
Bwana ameniadhibu sana, Lakini hakuniacha nife.
The LORD disciplined me severely, but He has not given me over to death.
19
Nifungulieni malango ya haki, Nitaingia na kumshukuru Bwana.
Open to me the gates of righteousness, that I may enter and give thanks to the LORD.
20
Lango hili ni la Bwana, Wenye haki ndio watakaoliingia.
This is the gate of the LORD; the righteous shall enter through it.
21
Nitakushukuru kwa maana umenijibu, Nawe umekuwa wokovu wangu.
I will give You thanks, for You have answered me, and You have become my salvation.
22
Jiwe walilolikataa waashi Limekuwa jiwe kuu la pembeni.
The stone the builders rejected has become the cornerstone.
23
Neno hili limetoka kwa Bwana, Nalo ni ajabu machoni petu.
This is from the LORD, and it is marvelous in our eyes.
24
Siku hii ndiyo aliyoifanya Bwana, Tutashangilia na kuifurahia.
This is the day that the LORD has made; we will rejoice and be glad in it.
25
Ee Bwana, utuokoe, twakusihi; Ee Bwana, utufanikishe, twakusihi.
O LORD, save us, we pray. We beseech You, O LORD, cause us to prosper!
26
Na abarikiwe yeye ajaye kwa jina la Bwana; Tumewabarikia toka nyumbani mwa Bwana.
Blessed is he who comes in the name of the LORD. From the house of the LORD we bless you.
27
Bwana ndiye aliye Mungu, Naye ndiye aliyetupa nuru. Ifungeni dhabihu kwa kamba Pembeni mwa madhabahu.
The LORD is God; He has made His light to shine upon us. Bind the festal sacrifice with cords to the horns of the altar.
28
Ndiwe Mungu wangu, nami nitakushukuru, Ndiwe Mungu wangu, nami nitakutukuza.
You are my God, and I will give You thanks. You are my God, and I will exalt You.
29
Mshukuruni Bwana kwa kuwa ni mwema, Kwa maana fadhili zake ni za milele.
Give thanks to the LORD, for He is good; His loving devotion endures forever.

Chagua Sura