Zaburi 118 Swahili & English
Listen/Download AudioZaburi 118 (Swahili) | Psalms 118 (English) |
---|---|
Haleluya. Mshukuruni Bwana kwa kuwa ni mwema, Kwa maana fadhili zake ni za milele. Zaburi 118:1 |
Give thanks to Yahweh, for he is good, For his loving kindness endures forever. |
Israeli na aseme sasa, Ya kwamba fadhili zake ni za milele. Zaburi 118:2 |
Let Israel now say That his loving kindness endures forever. |
Mlango wa Haruni na waseme sasa, Ya kwamba fadhili zake ni za milele. Zaburi 118:3 |
Let the house of Aaron now say That his loving kindness endures forever. |
Wamchao Bwana na waseme sasa, Ya kwamba fadhili zake ni za milele. Zaburi 118:4 |
Now let those who fear Yahweh say That his loving kindness endures forever. |
Katika shida yangu nalimwita Bwana; Bwana akanijibu akaniweka panapo nafasi. Zaburi 118:5 |
Out of my distress, I called on Yah. Yah answered me with freedom. |
Bwana yuko upande wangu, sitaogopa; Mwanadamu atanitenda nini? Zaburi 118:6 |
Yahweh is on my side. I will not be afraid. What can man do to me? |
Bwana yuko upande wangu, msaidizi wangu, Kwa hiyo nitawaona wanaonichukia wameshindwa. Zaburi 118:7 |
Yahweh is on my side among those who help me. Therefore I will look in triumph at those who hate me. |
Ni heri kumkimbilia Bwana Kuliko kuwatumainia wanadamu. Zaburi 118:8 |
It is better to take refuge in Yahweh, Than to put confidence in man. |
Ni heri kumkimbilia Bwana. Kuliko kuwatumainia wakuu. Zaburi 118:9 |
It is better to take refuge in Yahweh, Than to put confidence in princes. |
Mataifa yote walinizunguka; Kwa jina la Bwana naliwakatilia mbali. Zaburi 118:10 |
All the nations surrounded me, But in the name of Yahweh, I cut them off. |
Walinizunguka, naam, walinizunguka; Kwa jina la Bwana naliwakatilia mbali. Zaburi 118:11 |
They surrounded me, yes, they surrounded me. In the name of Yahweh I indeed cut them off. |
Walinizunguka kama nyuki, Walizimika kama moto wa miibani; Kwa jina la Bwana naliwakatilia mbali. Zaburi 118:12 |
They surrounded me like bees. They are quenched like the burning thorns. In the name of Yahweh I cut them off. |
Ulinisukuma sana ili nianguke; Lakini Bwana akanisaidia. Zaburi 118:13 |
You pushed me back hard, to make me fall, But Yahweh helped me. |
Bwana ni nguvu zangu na wimbo wangu, Naye amekuwa wokovu wangu. Zaburi 118:14 |
Yah is my strength and song. He has become my salvation. |
Sauti ya furaha na wokovu Imo hemani mwao wenye haki; Mkono wa kuume wa Bwana hutenda makuu. Zaburi 118:15 |
The voice of rejoicing and salvation is in the tents of the righteous. "The right hand of Yahweh does valiantly. |
Mkono wa kuume wa Bwana umetukuzwa; Mkono wa kuume wa Bwana hutenda makuu. Zaburi 118:16 |
The right hand of Yahweh is exalted! The right hand of Yahweh does valiantly!" |
Sitakufa bali nitaishi, Nami nitayasimulia matendo ya Bwana. Zaburi 118:17 |
I will not die, but live, And declare Yah's works. |
Bwana ameniadhibu sana, Lakini hakuniacha nife. Zaburi 118:18 |
Yah has punished me severely, But he has not given me over to death. |
Nifungulieni malango ya haki, Nitaingia na kumshukuru Bwana. Zaburi 118:19 |
Open to me the gates of righteousness. I will enter into them. I will give thanks to Yah. |
Lango hili ni la Bwana, Wenye haki ndio watakaoliingia. Zaburi 118:20 |
This is the gate of Yahweh; The righteous will enter into it. |
Nitakushukuru kwa maana umenijibu, Nawe umekuwa wokovu wangu. Zaburi 118:21 |
I will give thanks to you, for you have answered me, And have become my salvation. |
Jiwe walilolikataa waashi Limekuwa jiwe kuu la pembeni. Zaburi 118:22 |
The stone which the builders rejected has become the head of the corner. |
Neno hili limetoka kwa Bwana, Nalo ni ajabu machoni petu. Zaburi 118:23 |
This is Yahweh's doing. It is marvelous in our eyes. |
Siku hii ndiyo aliyoifanya Bwana, Tutashangilia na kuifurahia. Zaburi 118:24 |
This is the day that Yahweh has made. We will rejoice and be glad in it! |
Ee Bwana, utuokoe, twakusihi; Ee Bwana, utufanikishe, twakusihi. Zaburi 118:25 |
Save us now, we beg you, Yahweh; Yahweh, we beg you, now send prosperity. |
Na abarikiwe yeye ajaye kwa jina la Bwana; Tumewabarikia toka nyumbani mwa Bwana. Zaburi 118:26 |
Blessed is he who comes in the name of Yahweh! We have blessed you out of the house of Yahweh. |
Bwana ndiye aliye Mungu, Naye ndiye aliyetupa nuru. Ifungeni dhabihu kwa kamba Pembeni mwa madhabahu. Zaburi 118:27 |
Yahweh is God, and he has given us light. Bind the sacrifice with cords, even to the horns of the altar. |
Ndiwe Mungu wangu, nami nitakushukuru, Ndiwe Mungu wangu, nami nitakutukuza. Zaburi 118:28 |
You are my God, and I will give thanks to you. You are my God, I will exalt you. |
Mshukuruni Bwana kwa kuwa ni mwema, Kwa maana fadhili zake ni za milele. Zaburi 118:29 |
Oh give thanks to Yahweh, for he is good, For his loving kindness endures forever. |