Zaburi 118 Swahili & English

Listen/Download Audio
Zaburi 118 (Swahili) Psalms 118 (English)

Haleluya. Mshukuruni Bwana kwa kuwa ni mwema, Kwa maana fadhili zake ni za milele. Zaburi 118:1

Give thanks to Yahweh, for he is good, For his loving kindness endures forever.

Israeli na aseme sasa, Ya kwamba fadhili zake ni za milele. Zaburi 118:2

Let Israel now say That his loving kindness endures forever.

Mlango wa Haruni na waseme sasa, Ya kwamba fadhili zake ni za milele. Zaburi 118:3

Let the house of Aaron now say That his loving kindness endures forever.

Wamchao Bwana na waseme sasa, Ya kwamba fadhili zake ni za milele. Zaburi 118:4

Now let those who fear Yahweh say That his loving kindness endures forever.

Katika shida yangu nalimwita Bwana; Bwana akanijibu akaniweka panapo nafasi. Zaburi 118:5

Out of my distress, I called on Yah. Yah answered me with freedom.

Bwana yuko upande wangu, sitaogopa; Mwanadamu atanitenda nini? Zaburi 118:6

Yahweh is on my side. I will not be afraid. What can man do to me?

Bwana yuko upande wangu, msaidizi wangu, Kwa hiyo nitawaona wanaonichukia wameshindwa. Zaburi 118:7

Yahweh is on my side among those who help me. Therefore I will look in triumph at those who hate me.

Ni heri kumkimbilia Bwana Kuliko kuwatumainia wanadamu. Zaburi 118:8

It is better to take refuge in Yahweh, Than to put confidence in man.

Ni heri kumkimbilia Bwana. Kuliko kuwatumainia wakuu. Zaburi 118:9

It is better to take refuge in Yahweh, Than to put confidence in princes.

Mataifa yote walinizunguka; Kwa jina la Bwana naliwakatilia mbali. Zaburi 118:10

All the nations surrounded me, But in the name of Yahweh, I cut them off.

Walinizunguka, naam, walinizunguka; Kwa jina la Bwana naliwakatilia mbali. Zaburi 118:11

They surrounded me, yes, they surrounded me. In the name of Yahweh I indeed cut them off.

Walinizunguka kama nyuki, Walizimika kama moto wa miibani; Kwa jina la Bwana naliwakatilia mbali. Zaburi 118:12

They surrounded me like bees. They are quenched like the burning thorns. In the name of Yahweh I cut them off.

Ulinisukuma sana ili nianguke; Lakini Bwana akanisaidia. Zaburi 118:13

You pushed me back hard, to make me fall, But Yahweh helped me.

Bwana ni nguvu zangu na wimbo wangu, Naye amekuwa wokovu wangu. Zaburi 118:14

Yah is my strength and song. He has become my salvation.

Sauti ya furaha na wokovu Imo hemani mwao wenye haki; Mkono wa kuume wa Bwana hutenda makuu. Zaburi 118:15

The voice of rejoicing and salvation is in the tents of the righteous. "The right hand of Yahweh does valiantly.

Mkono wa kuume wa Bwana umetukuzwa; Mkono wa kuume wa Bwana hutenda makuu. Zaburi 118:16

The right hand of Yahweh is exalted! The right hand of Yahweh does valiantly!"

Sitakufa bali nitaishi, Nami nitayasimulia matendo ya Bwana. Zaburi 118:17

I will not die, but live, And declare Yah's works.

Bwana ameniadhibu sana, Lakini hakuniacha nife. Zaburi 118:18

Yah has punished me severely, But he has not given me over to death.

Nifungulieni malango ya haki, Nitaingia na kumshukuru Bwana. Zaburi 118:19

Open to me the gates of righteousness. I will enter into them. I will give thanks to Yah.

Lango hili ni la Bwana, Wenye haki ndio watakaoliingia. Zaburi 118:20

This is the gate of Yahweh; The righteous will enter into it.

Nitakushukuru kwa maana umenijibu, Nawe umekuwa wokovu wangu. Zaburi 118:21

I will give thanks to you, for you have answered me, And have become my salvation.

Jiwe walilolikataa waashi Limekuwa jiwe kuu la pembeni. Zaburi 118:22

The stone which the builders rejected has become the head of the corner.

Neno hili limetoka kwa Bwana, Nalo ni ajabu machoni petu. Zaburi 118:23

This is Yahweh's doing. It is marvelous in our eyes.

Siku hii ndiyo aliyoifanya Bwana, Tutashangilia na kuifurahia. Zaburi 118:24

This is the day that Yahweh has made. We will rejoice and be glad in it!

Ee Bwana, utuokoe, twakusihi; Ee Bwana, utufanikishe, twakusihi. Zaburi 118:25

Save us now, we beg you, Yahweh; Yahweh, we beg you, now send prosperity.

Na abarikiwe yeye ajaye kwa jina la Bwana; Tumewabarikia toka nyumbani mwa Bwana. Zaburi 118:26

Blessed is he who comes in the name of Yahweh! We have blessed you out of the house of Yahweh.

Bwana ndiye aliye Mungu, Naye ndiye aliyetupa nuru. Ifungeni dhabihu kwa kamba Pembeni mwa madhabahu. Zaburi 118:27

Yahweh is God, and he has given us light. Bind the sacrifice with cords, even to the horns of the altar.

Ndiwe Mungu wangu, nami nitakushukuru, Ndiwe Mungu wangu, nami nitakutukuza. Zaburi 118:28

You are my God, and I will give thanks to you. You are my God, I will exalt you.

Mshukuruni Bwana kwa kuwa ni mwema, Kwa maana fadhili zake ni za milele. Zaburi 118:29

Oh give thanks to Yahweh, for he is good, For his loving kindness endures forever.