Zaburi 48 Swahili & English
Listen/Download AudioZaburi 48 (Swahili) | Psalms 48 (English) |
---|---|
Bwana ndiye aliye mkuu, Na mwenye kusifiwa sana. Katika mji wa Mungu wetu, Katika mlima wake mtakatifu. Zaburi 48:1 |
> Great is Yahweh, and greatly to be praised, In the city of our God, in his holy mountain. |
Kuinuka kwake ni mzuri sana, Ni furaha ya dunia yote. Mlima Sayuni pande za kaskazini, Mji wa Mfalme mkuu. Zaburi 48:2 |
Beautiful in elevation, the joy of the whole earth, Is Mount Zion, on the north sides, The city of the great King. |
Mungu katika majumba yake Amejijulisha kuwa ngome. Zaburi 48:3 |
God has shown himself in her citadels as a refuge. |
Maana, tazama, wafalme walikusanyika; Walipita wote pamoja. Zaburi 48:4 |
For, behold, the kings assembled themselves, They passed by together. |
Waliona, mara wakashangaa; Wakafadhaika na kukimbia. Zaburi 48:5 |
They saw it, then they were amazed. They were dismayed, They hurried away. |
Papo hapo tetemeko liliwashika, Utungu kama wa mwanamke azaaye. Zaburi 48:6 |
Trembling took hold of them there, Pain, as of a woman in travail. |
Kwa upepo wa mashariki Wavunja jahazi za Tarshishi. Zaburi 48:7 |
With the east wind, you break the ships of Tarshish. |
Kama tulivyosikia, ndivyo tulivyoona, Katika mji wa Bwana wa majeshi. Mji wa Mungu wetu; Mungu ataufanya imara hata milele. Zaburi 48:8 |
As we have heard, so we have seen, In the city of Yahweh of Hosts, in the city of our God. God will establish it forever. Selah. |
Tumezitafakari fadhili zako, Ee Mungu, Katikati ya hekalu lako. Zaburi 48:9 |
We have thought about your loving kindness, God, In the midst of your temple. |
Kama lilivyo jina lako, Ee Mungu, Ndivyo na sifa yako hata miisho ya dunia. Mkono wako wa kuume umejaa haki; Zaburi 48:10 |
As is your name, God, So is your praise to the ends of the earth. Your right hand is full of righteousness. |
Na ufurahi mlima Sayuni. Binti za Yuda na washangilie Kwa sababu ya hukumu zako. Zaburi 48:11 |
Let Mount Zion be glad! Let the daughters of Judah rejoice, Because of your judgments. |
Tembeeni katika Sayuni, Uzungukeni mji, Ihesabuni minara yake, Zaburi 48:12 |
Walk about Zion, and go around her. Number its towers; |
Tieni moyoni boma zake, Yafikirini majumba yake, Mpate kuwaambia kizazi kitakachokuja. Zaburi 48:13 |
Mark well her bulwarks. Consider her palaces, That you may tell it to the next generation. |
Kwa maana ndivyo alivyo MUNGU, Mungu wetu. Milele na milele Yeye ndiye atakayetuongoza. Zaburi 48:14 |
For this God is our God forever and ever. He will be our guide even to death. |