Zaburi 48 Swahili & English

Listen/Download Audio
Zaburi 48 (Swahili) Psalms 48 (English)

Bwana ndiye aliye mkuu, Na mwenye kusifiwa sana. Katika mji wa Mungu wetu, Katika mlima wake mtakatifu. Zaburi 48:1

> Great is Yahweh, and greatly to be praised, In the city of our God, in his holy mountain.

Kuinuka kwake ni mzuri sana, Ni furaha ya dunia yote. Mlima Sayuni pande za kaskazini, Mji wa Mfalme mkuu. Zaburi 48:2

Beautiful in elevation, the joy of the whole earth, Is Mount Zion, on the north sides, The city of the great King.

Mungu katika majumba yake Amejijulisha kuwa ngome. Zaburi 48:3

God has shown himself in her citadels as a refuge.

Maana, tazama, wafalme walikusanyika; Walipita wote pamoja. Zaburi 48:4

For, behold, the kings assembled themselves, They passed by together.

Waliona, mara wakashangaa; Wakafadhaika na kukimbia. Zaburi 48:5

They saw it, then they were amazed. They were dismayed, They hurried away.

Papo hapo tetemeko liliwashika, Utungu kama wa mwanamke azaaye. Zaburi 48:6

Trembling took hold of them there, Pain, as of a woman in travail.

Kwa upepo wa mashariki Wavunja jahazi za Tarshishi. Zaburi 48:7

With the east wind, you break the ships of Tarshish.

Kama tulivyosikia, ndivyo tulivyoona, Katika mji wa Bwana wa majeshi. Mji wa Mungu wetu; Mungu ataufanya imara hata milele. Zaburi 48:8

As we have heard, so we have seen, In the city of Yahweh of Hosts, in the city of our God. God will establish it forever. Selah.

Tumezitafakari fadhili zako, Ee Mungu, Katikati ya hekalu lako. Zaburi 48:9

We have thought about your loving kindness, God, In the midst of your temple.

Kama lilivyo jina lako, Ee Mungu, Ndivyo na sifa yako hata miisho ya dunia. Mkono wako wa kuume umejaa haki; Zaburi 48:10

As is your name, God, So is your praise to the ends of the earth. Your right hand is full of righteousness.

Na ufurahi mlima Sayuni. Binti za Yuda na washangilie Kwa sababu ya hukumu zako. Zaburi 48:11

Let Mount Zion be glad! Let the daughters of Judah rejoice, Because of your judgments.

Tembeeni katika Sayuni, Uzungukeni mji, Ihesabuni minara yake, Zaburi 48:12

Walk about Zion, and go around her. Number its towers;

Tieni moyoni boma zake, Yafikirini majumba yake, Mpate kuwaambia kizazi kitakachokuja. Zaburi 48:13

Mark well her bulwarks. Consider her palaces, That you may tell it to the next generation.

Kwa maana ndivyo alivyo MUNGU, Mungu wetu. Milele na milele Yeye ndiye atakayetuongoza. Zaburi 48:14

For this God is our God forever and ever. He will be our guide even to death.