Zaburi 52 Swahili & English
Listen/Download AudioZaburi 52 (Swahili) | Psalms 52 (English) |
---|---|
Kwa nini kujisifia uovu, Ewe jabari? Wema wa Mungu upo sikuzote. Zaburi 52:1 |
> Why do you boast of mischief, mighty man? God's loving kindness endures continually. |
Ulimi wako watunga madhara, Kama wembe mkali, Ewe mwenye hila Zaburi 52:2 |
Your tongue plots destruction, Like a sharp razor, working deceitfully. |
Umependa mabaya kuliko mema, Na uongo kuliko kusema kweli. Zaburi 52:3 |
You love evil more than good, Lying rather than speaking the truth. Selah. |
Umependa maneno yote ya kupoteza watu, Ewe ulimi wenye hila. Zaburi 52:4 |
You love all devouring words, You deceitful tongue. |
Lakini Mungu atakuharibu hata milele; Atakuondolea mbali; Atakunyakua hemani mwako; Atakung'oa katika nchi ya walio hai. Zaburi 52:5 |
God will likewise destroy you forever. He will take you up, and pluck you out of your tent, And root you out of the land of the living. Selah. |
Nao wenye haki wataona; Wataingiwa na hofu na kumcheka; Zaburi 52:6 |
The righteous also will see it, and fear, And laugh at him, saying, |
Kumbe! Huyu ndiye mtu yule, Asiyemfanya Mungu kuwa nguvu zake. Aliutumainia wingi wa mali zake, Na kujifanya hodari kwa madhara yake. Zaburi 52:7 |
"Behold, this is the man who didn't make God his strength, But trusted in the abundance of his riches, And strengthened himself in his wickedness." |
Bali mimi ni kama mzeituni Umeao katika nyumba ya Mungu. Nazitumainia fadhili za Mungu milele na milele. Zaburi 52:8 |
But as for me, I am like a green olive tree in God's house. I trust in God's loving kindness forever and ever. |
Nitakushukuru milele kwa maana umetenda; Nitalingojea jina lako kwa kuwa ni jema; Mbele ya wacha Mungu wako. Zaburi 52:9 |
I will give you thanks forever, because you have done it. I will hope in your name, for it is good, In the presence of your saints. |