Zaburi BSB

Zaburi 52

Psalms Chapter 52

1
Kwa nini kujisifia uovu, Ewe jabari? Wema wa Mungu upo sikuzote.
For the choirmaster. A Maskil of David. After Doeg the Edomite went to Saul and told him, “David has gone to the house of Ahimelech.” Why do you boast of evil, O mighty man? The loving devotion of God endures all day long.
2
Ulimi wako watunga madhara, Kama wembe mkali, Ewe mwenye hila
Your tongue devises destruction like a sharpened razor, O worker of deceit.
3
Umependa mabaya kuliko mema, Na uongo kuliko kusema kweli.
You love evil more than good, falsehood more than speaking truth. Selah
4
Umependa maneno yote ya kupoteza watu, Ewe ulimi wenye hila.
You love every word that devours, O deceitful tongue.
5
Lakini Mungu atakuharibu hata milele; Atakuondolea mbali; Atakunyakua hemani mwako; Atakung'oa katika nchi ya walio hai.
Surely God will bring you down to everlasting ruin; He will snatch you up and tear you away from your tent; He will uproot you from the land of the living. Selah
6
Nao wenye haki wataona; Wataingiwa na hofu na kumcheka;
The righteous will see and fear; they will mock the evildoer, saying,
7
Kumbe! Huyu ndiye mtu yule, Asiyemfanya Mungu kuwa nguvu zake. Aliutumainia wingi wa mali zake, Na kujifanya hodari kwa madhara yake.
“Look at the man who did not make God his refuge, but trusted in the abundance of his wealth and strengthened himself by destruction.”
8
Bali mimi ni kama mzeituni Umeao katika nyumba ya Mungu. Nazitumainia fadhili za Mungu milele na milele.
But I am like an olive tree flourishing in the house of God; I trust in the loving devotion of God forever and ever.
9
Nitakushukuru milele kwa maana umetenda; Nitalingojea jina lako kwa kuwa ni jema; Mbele ya wacha Mungu wako.
I will praise You forever, because You have done it. I will wait on Your name—for it is good—in the presence of Your saints.

Chagua Sura