1
Hakika Mungu ni mwema kwa Israeli, Kwa hao walio safi mioyo yao.
A Psalm of Asaph. Surely God is good to Israel, to those who are pure in heart.
2
Nami miguu yangu ilikuwa karibu na kupotoka, Hatua zangu zilikuwa karibu na kuteleza.
But as for me, my feet had almost stumbled; my steps had nearly slipped.
3
Maana naliwaonea wivu wenye kujivuna, Nilipoiona hali ya amani ya wasio haki.
For I envied the arrogant when I saw the prosperity of the wicked.
4
Maana hawana maumivu katika kufa kwao, Na mwili wao una nguvu.
They have no struggle in their death; their bodies are well-fed.
5
Katika taabu ya watu hawamo, Wala hawapati mapigo pamoja na wanadamu.
They are free of the burdens others carry; they are not afflicted like other men.
6
Hivyo kiburi kimekuwa mkufu shingoni mwao, Jeuri huwavika kama nguo.
Therefore pride is their necklace; a garment of violence covers them.
7
Macho yao hutokeza kwa kunenepa, Wameipita kadiri ya mawazo ya mioyo yao.
From their prosperity proceeds iniquity; the imaginations of their hearts run wild.
8
Hudhihaki, husimulia mabaya, Husimulia udhalimu kana kwamba wako juu.
They mock and speak with malice; with arrogance they threaten oppression.
9
Wameweka kinywa chao mbinguni, Na ulimi wao hutanga-tanga duniani.
They set their mouths against the heavens, and their tongues strut across the earth.
10
Kwa hiyo watu wake hugeuka huko, Na maji yaliyojaa humezwa nao.
So their people return to this place and drink up waters in abundance.
11
Nao husema, Mungu ajuaje? Yako maarifa kwake aliye juu?
The wicked say, “How can God know? Does the Most High have knowledge?”
12
Fahamu, ndivyo walivyo wasio haki, Na kwa kustarehe sikuzote wamepata mali nyingi.
Behold, these are the wicked—always carefree as they increase their wealth.
13
Hakika nimejisafisha moyo wangu bure, Nimenawa mikono yangu kwa kutokukosa.
Surely in vain I have kept my heart pure; in innocence I have washed my hands.
14
Maana mchana kutwa nimepigwa, Na kuadhibiwa kila asubuhi.
For I am afflicted all day long and punished every morning.
15
Kama ningalisema, Nitasimulia kama hayo; Kumbe! Ningaliwadanganya kizazi cha wana wako.
If I had said, “I will speak this way,” then I would have betrayed Your children.
16
Nami nalifikiri jinsi ya kufahamu hayo; Ikawa taabu machoni pangu;
When I tried to understand all this, it was troublesome in my sight
17
Hata nilipoingia katika patakatifu pa Mungu, Nikautafakari mwisho wao.
until I entered God’s sanctuary; then I discerned their end.
18
Hakika Wewe huwaweka penye utelezi, Huwaangusha mpaka palipoharibika.
Surely You set them on slick ground; You cast them down into ruin.
19
Namna gani wamekuwa ukiwa mara! Wametokomea na kutoweshwa kwa utisho.
How suddenly they are laid waste, completely swept away by terrors!
20
Ee Bwana, kama ndoto wakati wa kuamka, Uondokapo utaidharau sanamu yao.
Like one waking from a dream, so You, O Lord, awaken and despise their form.
21
Moyo wangu ulipoona uchungu, Viuno vyangu viliponichoma,
When my heart was grieved and I was pierced within,
22
Nalikuwa kama mjinga, sijui neno; Nalikuwa kama mnyama tu mbele zako.
I was senseless and ignorant; I was a brute beast before You.
23
Walakini mimi ni pamoja nawe daima, Umenishika mkono wa kuume.
Yet I am always with You; You hold my right hand.
24
Utaniongoza kwa shauri lako, Na baadaye utanikaribisha kwa utukufu.
You guide me with Your counsel, and later receive me in glory.
25
Ni nani niliye naye mbinguni, Wala duniani sina cha kupendeza ila Wewe.
Whom have I in heaven but You? And on earth I desire no one besides You.
26
Mwili wangu na moyo wangu hupunguka, Bali Mungu ni mwamba wa moyo wangu Na sehemu yangu milele.
My flesh and my heart may fail, but God is the strength of my heart and my portion forever.
27
Maana wajitengao nawe watapotea; Umewaangamiza wote waliokuacha Wewe.
Those far from You will surely perish; You destroy all who are unfaithful to You.
28
Nami kumkaribia Mungu ni kwema kwangu; Nimefanya kimbilio kwa Bwana MUNGU, Niyahubiri matendo yako yote.
But as for me, it is good to draw near to God. I have made the Lord GOD my refuge, that I may proclaim all Your works.
Chagua Sura
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28
29
30
31
32
33
34
35
36
37
38
39
40
41
42
43
44
45
46
47
48
49
50
51
52
53
54
55
56
57
58
59
60
61
62
63
64
65
66
67
68
69
70
71
72
73
74
75
76
77
78
79
80
81
82
83
84
85
86
87
88
89
90
91
92
93
94
95
96
97
98
99
100
101
102
103
104
105
106
107
108
109
110
111
112
113
114
115
116
117
118
119
120
121
122
123
124
125
126
127
128
129
130
131
132
133
134
135
136
137
138
139
140
141
142
143
144
145
146
147
148
149
150