Zaburi BSB

Zaburi 76

Psalms Chapter 76

1
Katika Yuda Mungu amejulikana, Katika Israeli jina lake ni kuu.
For the choirmaster. With stringed instruments. A Psalm of Asaph. A song. God is known in Judah; His name is great in Israel.
2
Kibanda chake pia kiko Salemu, Na maskani yake iko Sayuni.
His tent is in Salem, His dwelling place in Zion.
3
Huko ndiko alikoivunja mishale ya uta, Ngao, na upanga, na zana za vita.
There He shattered the flaming arrows, the shield and sword and weapons of war. Selah
4
Wewe U mwenye fahari na adhama, Toka milima ya mateka.
You are resplendent with light, more majestic than mountains filled with game.
5
Wametekwa wenye moyo thabiti; Wamelala usingizi; Wala hawakuiona mikono yao Watu wote walio hodari.
The valiant lie plundered; they sleep their last sleep. No men of might could lift a hand.
6
Kwa kukemea kwako, Ee Mungu wa Yakobo, Gari na farasi wameshikwa na usingizi mzito.
At Your rebuke, O God of Jacob, both horse and rider lie stunned.
7
Wewe ndiwe utishaye, naam, Wewe; Naye ni nani awezaye kusimama ufanyapo hasira?
You alone are to be feared. When You are angry, who can stand before You?
8
Toka mbinguni ulitangaza hukumu; Nchi iliogopa, ikakaa kimya.
From heaven You pronounced judgment, and the earth feared and was still
9
Mungu aliposimama ili kuhukumu Na kuwaokoa wapole wa dunia wote pia.
when God rose up to judge, to save all the lowly of the earth. Selah
10
Maana hasira ya binadamu itakusifu, Masalio ya hasira utajifunga kama mshipi.
Even the wrath of man shall praise You; with the survivors of wrath You will clothe Yourself.
11
Wekeni nadhiri, mkaziondoe Kwa Bwana, Mungu wenu. Wote wanaomzunguka wamletee hedaya, Yeye astahiliye kuogopwa.
Make and fulfill your vows to the LORD your God; let all the neighboring lands bring tribute to Him who is to be feared.
12
Yeye huzikata roho za wakuu; Na kuwatisha wafalme wa dunia.
He breaks the spirits of princes; He is feared by the kings of the earth.

Chagua Sura