Zaburi 76 Swahili & English

Listen/Download Audio
Zaburi 76 (Swahili) Psalms 76 (English)

Katika Yuda Mungu amejulikana, Katika Israeli jina lake ni kuu. Zaburi 76:1

> In Judah, God is known. His name is great in Israel.

Kibanda chake pia kiko Salemu, Na maskani yake iko Sayuni. Zaburi 76:2

His tent is also in Salem; His dwelling place in Zion.

Huko ndiko alikoivunja mishale ya uta, Ngao, na upanga, na zana za vita. Zaburi 76:3

There he broke the flaming arrows of the bow, The shield, and the sword, and the weapons of war. Selah.

Wewe U mwenye fahari na adhama, Toka milima ya mateka. Zaburi 76:4

Glorious are you, and excellent, More than mountains of game.

Wametekwa wenye moyo thabiti; Wamelala usingizi; Wala hawakuiona mikono yao Watu wote walio hodari. Zaburi 76:5

Valiant men lie plundered, They have slept their last sleep. None of the men of war can lift their hands.

Kwa kukemea kwako, Ee Mungu wa Yakobo, Gari na farasi wameshikwa na usingizi mzito. Zaburi 76:6

At your rebuke, God of Jacob, Both chariot and horse are cast into a deep sleep.

Wewe ndiwe utishaye, naam, Wewe; Naye ni nani awezaye kusimama ufanyapo hasira? Zaburi 76:7

You, even you, are to be feared. Who can stand in your sight when you are angry?

Toka mbinguni ulitangaza hukumu; Nchi iliogopa, ikakaa kimya. Zaburi 76:8

You pronounced judgment from heaven. The earth feared, and was silent,

Mungu aliposimama ili kuhukumu Na kuwaokoa wapole wa dunia wote pia. Zaburi 76:9

When God arose to judgment, To save all the afflicted ones of the earth. Selah.

Maana hasira ya binadamu itakusifu, Masalio ya hasira utajifunga kama mshipi. Zaburi 76:10

Surely the wrath of man praises you. The survivors of your wrath are restrained.

Wekeni nadhiri, mkaziondoe Kwa Bwana, Mungu wenu. Wote wanaomzunguka wamletee hedaya, Yeye astahiliye kuogopwa. Zaburi 76:11

Make vows to Yahweh your God, and fulfill them! Let all of his neighbors bring presents to him who is to be feared.

Yeye huzikata roho za wakuu; Na kuwatisha wafalme wa dunia. Zaburi 76:12

He will cut off the spirit of princes. He is feared by the kings of the earth.