1
Haleluya. Mshukuruni Bwana kwa kuwa ni mwema, Kwa maana fadhili zake ni za milele.
Hallelujah! Give thanks to the LORD, for He is good; His loving devotion endures forever.
2
Nani awezaye kuyanena matendo makuu ya Bwana, Kuzihubiri sifa zake zote?
Who can describe the mighty acts of the LORD or fully proclaim His praise?
3
Heri washikao hukumu, Na kutenda haki sikuzote.
Blessed are those who uphold justice, who practice righteousness at all times.
4
Ee Bwana, unikumbuke mimi, Kwa kibali uliyo nayo kwa watu wako. Unijilie kwa wokovu wako,
Remember me, O LORD, in Your favor to Your people; visit me with Your salvation,
5
Ili niuone wema wa wateule wako. Nipate kuifurahia furaha ya taifa lako, Na kujisifu pamoja na watu wako.
that I may see the prosperity of Your chosen ones, and rejoice in the gladness of Your nation, and give glory with Your inheritance.
6
Tumetenda dhambi pamoja na baba zetu, Tumetenda maovu, tumefanya ubaya.
We have sinned like our fathers; we have done wrong and acted wickedly.
7
Baba zetu katika Misri Hawakufikiri matendo yako ya ajabu; Hawakukumbuka wingi wa fadhili zako; Wakaasi penye bahari, bahari ya Shamu.
Our fathers in Egypt did not grasp Your wonders or remember Your abundant kindness; but they rebelled by the sea, there at the Red Sea.
8
Lakini akawaokoa kwa ajili ya jina lake, Ayadhihirishe matendo yake makuu.
Yet He saved them for the sake of His name, to make His power known.
9
Akaikemea bahari ya Shamu ikakauka, Akawaongoza vilindini kana kwamba ni uwanda.
He rebuked the Red Sea, and it dried up; He led them through the depths as through a desert.
10
Akawaokoa na mkono wa mtu aliyewachukia, Na kuwakomboa na mkono wa adui zao.
He saved them from the hand that hated them; He redeemed them from the hand of the enemy.
11
Maji yakawafunika watesi wao, Hakusalia hata mmoja wao.
The waters covered their foes; not one of them remained.
12
Ndipo walipoyaamini maneno yake, Waliziimba sifa zake.
Then they believed His promises and sang His praise.
13
Wakayasahau matendo yake kwa haraka, Hawakulingojea shauri lake.
Yet they soon forgot His works and failed to wait for His counsel.
14
Bali walitamani sana jangwani, Wakamjaribu Mungu nyikani.
They craved intensely in the wilderness and tested God in the desert.
15
Akawapa walichomtaka, Akawakondesha roho zao.
So He granted their request, but sent a wasting disease upon them.
16
Wakamhusudu Musa matuoni, Na Haruni, mtakatifu wa Bwana.
In the camp they envied Moses, as well as Aaron, the holy one of the LORD.
17
Nchi ikapasuka ikammeza Dathani, Ikaufunika mkutano wa Abiramu.
The earth opened up and swallowed Dathan; it covered the assembly of Abiram.
18
Moto ukawaka katika mkutano wao, Miali yake ikawateketeza wabaya.
Then fire blazed through their company; flames consumed the wicked.
19
Walifanya ndama huko Horebu, Wakaisujudia sanamu ya kuyeyuka.
At Horeb they made a calf and worshiped a molten image.
20
Wakaubadili utukufu wao Kuwa mfano wa ng'ombe mla majani.
They exchanged their Glory for the image of a grass-eating ox.
21
Wakamsahau Mungu, mwokozi wao, Aliyetenda makuu katika Misri.
They forgot God their Savior, who did great things in Egypt,
22
Matendo ya ajabu katika nchi ya Hamu, Mambo ya kutisha penye bahari ya Shamu.
wondrous works in the land of Ham, and awesome deeds by the Red Sea.
23
Akasema ya kuwa atawaangamiza Kama Musa, mteule wake, asingalisimama, Mbele zake kama mahali palipobomoka, Ili aigeuze hasira yake asije akawaharibu.
So He said He would destroy them—had not Moses His chosen one stood before Him in the breach to divert His wrath from destroying them.
24
Wakaidharau nchi ile ya kupendeza, Wala hawakuliamini neno lake.
They despised the pleasant land; they did not believe His promise.
25
Bali wakanung'unika hemani mwao, Wala hawakuisikiliza sauti ya Bwana.
They grumbled in their tents and did not listen to the voice of the LORD.
26
Ndipo alipowainulia mkono wake, Ya kuwa atawaangamiza jangwani,
So He raised His hand and swore to cast them down in the wilderness,
27
Na kuwatawanya wazao wao kati ya mataifa, Na kuwatapanya katika nchi mbali.
to disperse their offspring among the nations and scatter them throughout the lands.
28
Wakajiambatiza na Baal-Peori, Wakazila dhabihu za wafu.
They yoked themselves to Baal of Peor and ate sacrifices offered to lifeless gods.
29
Wakamkasirisha kwa matendo yao; Tauni ikawashambulia.
So they provoked the LORD to anger with their deeds, and a plague broke out among them.
30
Ndipo Finehasi akasimama akafanya hukumu; Tauni ikazuiliwa.
But Phinehas stood and intervened, and the plague was restrained.
31
Akahesabiwa kuwa ana haki Kizazi baada ya kizazi hata milele.
It was credited to him as righteousness for endless generations to come.
32
Wakamghadhibisha penye maji ya Meriba, Hasara ikampata Musa kwa ajili yao,
At the waters of Meribah they angered the LORD, and trouble came to Moses because of them.
33
Kwa sababu waliiasi roho yake, Akasema yasiyofaa kwa midomo yake.
For they rebelled against His Spirit, and Moses spoke rashly with his lips.
34
Hawakuwaharibu watu wa nchi Kama Bwana alivyowaambia;
They did not destroy the peoples as the LORD had commanded them,
35
Bali walijichanganya na mataifa, Wakajifunza matendo yao.
but they mingled with the nations and adopted their customs.
36
Wakazitumikia sanamu zao, Nazo zikawa mtego kwao.
They worshiped their idols, which became a snare to them.
37
Naam, walitoa wana wao na binti zao Kuwa dhabihu kwa mashetani.
They sacrificed their sons and their daughters to demons.
38
Wakamwaga damu isiyo na hatia, Damu ya wana wao na binti zao, Waliowatoa dhabihu kwa sanamu za Kanaani; Nchi ikatiwa unajisi kwa damu.
They shed innocent blood—the blood of their sons and daughters, whom they sacrificed to the idols of Canaan, and the land was polluted with blood.
39
Ndivyo walivyotiwa uchafu kwa kazi zao, Wakafanya uasherati kwa matendo yao.
They defiled themselves by their actions and prostituted themselves by their deeds.
40
Hasira ya Bwana ikawaka juu ya watu wake, Akauchukia urithi wake.
So the anger of the LORD burned against His people, and He abhorred His own inheritance.
41
Akawatia mikononi mwa mataifa, Nao waliowachukia wakawatawala.
He delivered them into the hand of the nations, and those who hated them ruled over them.
42
Adui zao wakawaonea, Wakatiishwa chini ya mkono wao.
Their enemies oppressed them and subdued them under their hand.
43
Mara nyingi aliwaponya, Bali walikuwa wakimwasi kwa mashauri yao, Wakadhilika katika uovu wao.
Many times He rescued them, but they were bent on rebellion and sank down in their iniquity.
44
Lakini aliyaangalia mateso yao, Aliposikia kilio chao.
Nevertheless He heard their cry; He took note of their distress.
45
Akawakumbukia agano lake; Akawahurumia kwa wingi wa fadhili zake;
And He remembered His covenant with them, and relented by the abundance of His loving devotion.
46
Akawajalia kuhurumiwa Na watu wote waliowateka.
He made them objects of compassion to all who held them captive.
47
Ee Bwana, Mungu wetu, utuokoe, Utukusanye kwa kututoa katika mataifa, Tulishukuru jina lako takatifu, Tuzifanyie shangwe sifa zako.
Save us, O LORD our God, and gather us from the nations, that we may give thanks to Your holy name, that we may glory in Your praise.
48
Na ahimidiwe Bwana, Mungu wa Israeli, Tangu milele hata milele. Watu wote na waseme, Amina. Haleluya.
Blessed be the LORD, the God of Israel, from everlasting to everlasting. Let all the people say, “Amen!” Hallelujah!
Chagua Sura
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28
29
30
31
32
33
34
35
36
37
38
39
40
41
42
43
44
45
46
47
48
49
50
51
52
53
54
55
56
57
58
59
60
61
62
63
64
65
66
67
68
69
70
71
72
73
74
75
76
77
78
79
80
81
82
83
84
85
86
87
88
89
90
91
92
93
94
95
96
97
98
99
100
101
102
103
104
105
106
107
108
109
110
111
112
113
114
115
116
117
118
119
120
121
122
123
124
125
126
127
128
129
130
131
132
133
134
135
136
137
138
139
140
141
142
143
144
145
146
147
148
149
150