Zaburi 29 Swahili & English

Listen/Download Audio
Zaburi 29 (Swahili) Psalms 29 (English)

Mpeni Bwana, enyi wana wa Mungu, Mpeni Bwana utukufu na nguvu; Zaburi 29:1

> Ascribe to Yahweh, you sons of the mighty, Ascribe to Yahweh glory and strength.

Mpeni Bwana utukufu wa jina lake; Mwabuduni Bwana kwa uzuri wa utakatifu. Zaburi 29:2

Ascribe to Yahweh the glory due to his name. Worship Yahweh in holy array.

Sauti ya Bwana i juu ya maji; Mungu wa utukufu alipiga radi; Bwana yu juu ya maji mengi. Zaburi 29:3

Yahweh's voice is on the waters. The God of glory thunders, even Yahweh on many waters.

Sauti ya Bwana ina nguvu; Sauti ya Bwana ina adhama; Zaburi 29:4

Yahweh's voice is powerful. Yahweh's voice is full of majesty.

Sauti ya Bwana yaivunja mierezi; Naam, Bwana aivunja-vunja mierezi ya Lebanoni; Zaburi 29:5

The voice of Yahweh breaks the cedars. Yes, Yahweh breaks in pieces the cedars of Lebanon.

Airusha-rusha kama ndama wa ng'ombe; Lebanoni na Sirioni kama mwana-nyati. Zaburi 29:6

He makes them also to skip like a calf; Lebanon and Sirion like a young, wild ox.

Sauti ya Bwana yaipasua miali ya moto; Zaburi 29:7

Yahweh's voice strikes with flashes of lightning.

Sauti ya Bwana yalitetemesha jangwa; Bwana alitetemesha jangwa la Kadeshi. Zaburi 29:8

Yahweh's voice shakes the wilderness. Yahweh shakes the wilderness of Kadesh.

Sauti ya Bwana yawazalisha ayala, Na kuifichua misitu; Na ndani ya hekalu lake Wanasema wote, Utukufu. Zaburi 29:9

Yahweh's voice makes the deer calve, And strips the forests bare. In his temple everything says, "Glory!"

Bwana aliketi juu ya Gharika; Naam, Bwana ameketi hali ya mfalme milele. Zaburi 29:10

Yahweh sat enthroned at the Flood. Yes, Yahweh sits as King forever.

Bwana atawapa watu wake nguvu; Bwana atawabariki watu wake kwa amani. Zaburi 29:11

Yahweh will give strength to his people. Yahweh will bless his people with peace.