Zaburi 29 Swahili & English
Listen/Download AudioZaburi 29 (Swahili) | Psalms 29 (English) |
---|---|
Mpeni Bwana, enyi wana wa Mungu, Mpeni Bwana utukufu na nguvu; Zaburi 29:1 |
> Ascribe to Yahweh, you sons of the mighty, Ascribe to Yahweh glory and strength. |
Mpeni Bwana utukufu wa jina lake; Mwabuduni Bwana kwa uzuri wa utakatifu. Zaburi 29:2 |
Ascribe to Yahweh the glory due to his name. Worship Yahweh in holy array. |
Sauti ya Bwana i juu ya maji; Mungu wa utukufu alipiga radi; Bwana yu juu ya maji mengi. Zaburi 29:3 |
Yahweh's voice is on the waters. The God of glory thunders, even Yahweh on many waters. |
Sauti ya Bwana ina nguvu; Sauti ya Bwana ina adhama; Zaburi 29:4 |
Yahweh's voice is powerful. Yahweh's voice is full of majesty. |
Sauti ya Bwana yaivunja mierezi; Naam, Bwana aivunja-vunja mierezi ya Lebanoni; Zaburi 29:5 |
The voice of Yahweh breaks the cedars. Yes, Yahweh breaks in pieces the cedars of Lebanon. |
Airusha-rusha kama ndama wa ng'ombe; Lebanoni na Sirioni kama mwana-nyati. Zaburi 29:6 |
He makes them also to skip like a calf; Lebanon and Sirion like a young, wild ox. |
Sauti ya Bwana yaipasua miali ya moto; Zaburi 29:7 |
Yahweh's voice strikes with flashes of lightning. |
Sauti ya Bwana yalitetemesha jangwa; Bwana alitetemesha jangwa la Kadeshi. Zaburi 29:8 |
Yahweh's voice shakes the wilderness. Yahweh shakes the wilderness of Kadesh. |
Sauti ya Bwana yawazalisha ayala, Na kuifichua misitu; Na ndani ya hekalu lake Wanasema wote, Utukufu. Zaburi 29:9 |
Yahweh's voice makes the deer calve, And strips the forests bare. In his temple everything says, "Glory!" |
Bwana aliketi juu ya Gharika; Naam, Bwana ameketi hali ya mfalme milele. Zaburi 29:10 |
Yahweh sat enthroned at the Flood. Yes, Yahweh sits as King forever. |
Bwana atawapa watu wake nguvu; Bwana atawabariki watu wake kwa amani. Zaburi 29:11 |
Yahweh will give strength to his people. Yahweh will bless his people with peace. |