Zaburi 88 Swahili & English

Listen/Download Audio
Zaburi 88 (Swahili) Psalms 88 (English)

Ee Bwana, Mungu wa wokovu wangu Mchana na usiku nimelia mbele zako. Zaburi 88:1

> Yahweh, the God of my salvation, I have cried day and night before you.

Maombi yangu yafike mbele zako, Uutegee ukelele wangu sikio lako. Zaburi 88:2

Let my prayer enter into your presence. Turn your ear to my cry.

Maana nafsi yangu imeshiba taabu, Na uhai wangu umekaribia kuzimu. Zaburi 88:3

For my soul is full of troubles. My life draws near to Sheol.

Nimehesabiwa pamoja nao washukao shimoni; Nimekuwa kama mtu asiye na msaada. Zaburi 88:4

I am counted among those who go down into the pit. I am like a man who has no help,

Miongoni mwao waliokufa nimetupwa, Kama waliouawa walalao makaburini. Hao ambao Wewe huwakumbuki tena, Wametengwa mbali na mkono wako. Zaburi 88:5

Set apart among the dead, Like the slain who lie in the grave, Whom you remember no more. They are cut off from your hand.

Mimi umenilaza katika shimo la chini, Katika mahali penye giza vilindini. Zaburi 88:6

You have laid me in the lowest pit, In the darkest depths.

Ghadhabu yako imenilemea, Umenitesa kwa mawimbi yako yote. Zaburi 88:7

Your wrath lies heavily on me. You have afflicted me with all your waves. Selah.

Wanijuao umewatenga nami; Umenifanya kuwa chukizo kwao; Nimefungwa wala siwezi kutoka. Zaburi 88:8

You have taken my friends from me. You have made me an abomination to them. I am confined, and I can't escape.

Jicho langu limefifia kwa ajili ya mateso Bwana, nimekuita kila siku; Nimekunyoshea Wewe mikono yangu. Zaburi 88:9

My eyes are dim from grief. I have called on you daily, Yahweh. I have spread out my hands to you.

Wafu je! Utawafanyia miujiza? Au waliofariki watasimama na kukuhimidi? Zaburi 88:10

Do you show wonders to the dead? Do the dead rise up and praise you? Selah.

Fadhili zako zitasimuliwa kaburini? Au uaminifu wako katika uharibifu? Zaburi 88:11

Is your loving kindness declared in the grave? Or your faithfulness in Destruction?

Miujiza yako itajulikana gizani? Au haki yako katika nchi ya usahaulifu? Zaburi 88:12

Are your wonders made known in the dark? Or your righteousness in the land of forgetfulness?

Lakini mimi nimekulilia Wewe, Bwana, Na asubuhi maombi yangu yatakuwasilia. Zaburi 88:13

But to you, Yahweh, I have cried. In the morning, my prayer comes before you.

Bwana, kwa nini kuitupa nafsi yangu, Na kunificha uso wako? Zaburi 88:14

Yahweh, why do you reject my soul? Why do you hide your face from me?

Nateswa mimi hali ya kufa tangu ujana, Nimevumilia vitisho vyako na kufadhaika. Zaburi 88:15

I am afflicted and ready to die from my youth up. While I suffer your terrors, I am distracted.

Hasira zako kali zimepita juu yangu, Maogofyo yako yameniangamiza. Zaburi 88:16

Your fierce wrath has gone over me. Your terrors have cut me off.

Yamenizunguka kama maji mchana kutwa, Yamenisonga yote pamoja. Zaburi 88:17

They came around me like water all day long. They completely engulfed me.

Mpenzi na rafiki umewatenga nami, Nao wanijuao wamo gizani. Zaburi 88:18

You have put lover and friend far from me, And my friends into darkness.