Zaburi 88 Swahili & English
Listen/Download AudioZaburi 88 (Swahili) | Psalms 88 (English) |
---|---|
Ee Bwana, Mungu wa wokovu wangu Mchana na usiku nimelia mbele zako. Zaburi 88:1 |
> Yahweh, the God of my salvation, I have cried day and night before you. |
Maombi yangu yafike mbele zako, Uutegee ukelele wangu sikio lako. Zaburi 88:2 |
Let my prayer enter into your presence. Turn your ear to my cry. |
Maana nafsi yangu imeshiba taabu, Na uhai wangu umekaribia kuzimu. Zaburi 88:3 |
For my soul is full of troubles. My life draws near to Sheol. |
Nimehesabiwa pamoja nao washukao shimoni; Nimekuwa kama mtu asiye na msaada. Zaburi 88:4 |
I am counted among those who go down into the pit. I am like a man who has no help, |
Miongoni mwao waliokufa nimetupwa, Kama waliouawa walalao makaburini. Hao ambao Wewe huwakumbuki tena, Wametengwa mbali na mkono wako. Zaburi 88:5 |
Set apart among the dead, Like the slain who lie in the grave, Whom you remember no more. They are cut off from your hand. |
Mimi umenilaza katika shimo la chini, Katika mahali penye giza vilindini. Zaburi 88:6 |
You have laid me in the lowest pit, In the darkest depths. |
Ghadhabu yako imenilemea, Umenitesa kwa mawimbi yako yote. Zaburi 88:7 |
Your wrath lies heavily on me. You have afflicted me with all your waves. Selah. |
Wanijuao umewatenga nami; Umenifanya kuwa chukizo kwao; Nimefungwa wala siwezi kutoka. Zaburi 88:8 |
You have taken my friends from me. You have made me an abomination to them. I am confined, and I can't escape. |
Jicho langu limefifia kwa ajili ya mateso Bwana, nimekuita kila siku; Nimekunyoshea Wewe mikono yangu. Zaburi 88:9 |
My eyes are dim from grief. I have called on you daily, Yahweh. I have spread out my hands to you. |
Wafu je! Utawafanyia miujiza? Au waliofariki watasimama na kukuhimidi? Zaburi 88:10 |
Do you show wonders to the dead? Do the dead rise up and praise you? Selah. |
Fadhili zako zitasimuliwa kaburini? Au uaminifu wako katika uharibifu? Zaburi 88:11 |
Is your loving kindness declared in the grave? Or your faithfulness in Destruction? |
Miujiza yako itajulikana gizani? Au haki yako katika nchi ya usahaulifu? Zaburi 88:12 |
Are your wonders made known in the dark? Or your righteousness in the land of forgetfulness? |
Lakini mimi nimekulilia Wewe, Bwana, Na asubuhi maombi yangu yatakuwasilia. Zaburi 88:13 |
But to you, Yahweh, I have cried. In the morning, my prayer comes before you. |
Bwana, kwa nini kuitupa nafsi yangu, Na kunificha uso wako? Zaburi 88:14 |
Yahweh, why do you reject my soul? Why do you hide your face from me? |
Nateswa mimi hali ya kufa tangu ujana, Nimevumilia vitisho vyako na kufadhaika. Zaburi 88:15 |
I am afflicted and ready to die from my youth up. While I suffer your terrors, I am distracted. |
Hasira zako kali zimepita juu yangu, Maogofyo yako yameniangamiza. Zaburi 88:16 |
Your fierce wrath has gone over me. Your terrors have cut me off. |
Yamenizunguka kama maji mchana kutwa, Yamenisonga yote pamoja. Zaburi 88:17 |
They came around me like water all day long. They completely engulfed me. |
Mpenzi na rafiki umewatenga nami, Nao wanijuao wamo gizani. Zaburi 88:18 |
You have put lover and friend far from me, And my friends into darkness. |