Zaburi 96 Swahili & English

Listen/Download Audio
Zaburi 96 (Swahili) Psalms 96 (English)

Mwimbieni Bwana wimbo mpya, Mwimbieni Bwana, nchi yote. Zaburi 96:1

Sing to Yahweh a new song! Sing to Yahweh, all the earth.

Mwimbieni Bwana, libarikini jina lake, Tangazeni wokovu wake siku kwa siku. Zaburi 96:2

Sing to Yahweh! Bless his name! Proclaim his salvation from day to day!

Wahubirini mataifa habari za utukufu wake, Na watu wote habari za maajabu yake. Zaburi 96:3

Declare his glory among the nations, His marvelous works among all the peoples.

Kwa kuwa Bwana ni mkuu mwenye kusifiwa sana. Na wa kuhofiwa kuliko miungu yote. Zaburi 96:4

For great is Yahweh, and greatly to be praised! He is to be feared above all gods.

Maana miungu yote ya watu si kitu, Lakini Bwana ndiye aliyezifanya mbingu. Zaburi 96:5

For all the gods of the peoples are idols, But Yahweh made the heavens.

Heshima na adhama ziko mbele zake, Nguvu na uzuri zimo katika patakatifu pake. Zaburi 96:6

Honor and majesty are before him. Strength and beauty are in his sanctuary.

Mpeni Bwana, enyi jamaa za watu, Mpeni Bwana utukufu na nguvu. Zaburi 96:7

Ascribe to Yahweh, you families of nations, Ascribe to Yahweh glory and strength.

Mpeni Bwana utukufu wa jina lake, Leteni sadaka mkaziingie nyua zake. Zaburi 96:8

Ascribe to Yahweh the glory due to his name. Bring an offering, and come into his courts.

Mwabuduni Bwana kwa uzuri wa utakatifu, Tetemekeni mbele zake, nchi yote. Zaburi 96:9

Worship Yahweh in holy array. Tremble before him, all the earth.

Semeni katika mataifa, Bwana ametamalaki; Naam, ulimwengu umethibitika usitikisike, Atawahukumu watu kwa adili. Zaburi 96:10

Say among the nations, "Yahweh reigns." The world is also established. It can't be moved. He will judge the peoples with equity.

Mbingu na zifurahi, nchi na ishangilie, Bahari na ivume na vyote viijazavyo, Zaburi 96:11

Let the heavens be glad, and let the earth rejoice. Let the sea roar, and it's fullness!

Mashamba na yashangilie, na vyote vilivyomo, Ndipo miti yote ya mwituni iimbe kwa furaha; Zaburi 96:12

Let the field and all that is in it exult! Then all the trees of the woods shall sing for joy

Mbele za Bwana, kwa maana anakuja, Kwa maana anakuja aihukumu nchi. Atauhukumu ulimwengu kwa haki, Na mataifa kwa uaminifu wake. Zaburi 96:13

Before Yahweh; for he comes, For he comes to judge the earth. He will judge the world with righteousness, The peoples with his truth.