Zaburi 96 Swahili & English
Listen/Download AudioZaburi 96 (Swahili) | Psalms 96 (English) |
---|---|
Mwimbieni Bwana wimbo mpya, Mwimbieni Bwana, nchi yote. Zaburi 96:1 |
Sing to Yahweh a new song! Sing to Yahweh, all the earth. |
Mwimbieni Bwana, libarikini jina lake, Tangazeni wokovu wake siku kwa siku. Zaburi 96:2 |
Sing to Yahweh! Bless his name! Proclaim his salvation from day to day! |
Wahubirini mataifa habari za utukufu wake, Na watu wote habari za maajabu yake. Zaburi 96:3 |
Declare his glory among the nations, His marvelous works among all the peoples. |
Kwa kuwa Bwana ni mkuu mwenye kusifiwa sana. Na wa kuhofiwa kuliko miungu yote. Zaburi 96:4 |
For great is Yahweh, and greatly to be praised! He is to be feared above all gods. |
Maana miungu yote ya watu si kitu, Lakini Bwana ndiye aliyezifanya mbingu. Zaburi 96:5 |
For all the gods of the peoples are idols, But Yahweh made the heavens. |
Heshima na adhama ziko mbele zake, Nguvu na uzuri zimo katika patakatifu pake. Zaburi 96:6 |
Honor and majesty are before him. Strength and beauty are in his sanctuary. |
Mpeni Bwana, enyi jamaa za watu, Mpeni Bwana utukufu na nguvu. Zaburi 96:7 |
Ascribe to Yahweh, you families of nations, Ascribe to Yahweh glory and strength. |
Mpeni Bwana utukufu wa jina lake, Leteni sadaka mkaziingie nyua zake. Zaburi 96:8 |
Ascribe to Yahweh the glory due to his name. Bring an offering, and come into his courts. |
Mwabuduni Bwana kwa uzuri wa utakatifu, Tetemekeni mbele zake, nchi yote. Zaburi 96:9 |
Worship Yahweh in holy array. Tremble before him, all the earth. |
Semeni katika mataifa, Bwana ametamalaki; Naam, ulimwengu umethibitika usitikisike, Atawahukumu watu kwa adili. Zaburi 96:10 |
Say among the nations, "Yahweh reigns." The world is also established. It can't be moved. He will judge the peoples with equity. |
Mbingu na zifurahi, nchi na ishangilie, Bahari na ivume na vyote viijazavyo, Zaburi 96:11 |
Let the heavens be glad, and let the earth rejoice. Let the sea roar, and it's fullness! |
Mashamba na yashangilie, na vyote vilivyomo, Ndipo miti yote ya mwituni iimbe kwa furaha; Zaburi 96:12 |
Let the field and all that is in it exult! Then all the trees of the woods shall sing for joy |
Mbele za Bwana, kwa maana anakuja, Kwa maana anakuja aihukumu nchi. Atauhukumu ulimwengu kwa haki, Na mataifa kwa uaminifu wake. Zaburi 96:13 |
Before Yahweh; for he comes, For he comes to judge the earth. He will judge the world with righteousness, The peoples with his truth. |