Zaburi 45 Swahili & English
Listen/Download AudioZaburi 45 (Swahili) | Psalms 45 (English) |
---|---|
Moyo wangu umefurika kwa neno jema, Mimi nasema niliyomfanyizia mfalme; Ulimi wangu ni kalamu ya mwandishi mstadi. Zaburi 45:1 |
> My heart overflows with a noble theme. I recite my verses for the king. My tongue is like the pen of a skillful writer. |
Wewe u mzuri sana kuliko wanadamu; Neema imemiminiwa midomoni mwako, Kwa hiyo Mungu amekubariki hata milele. Zaburi 45:2 |
You are the most excellent of the sons of men. Grace has anointed your lips, Therefore God has blessed you forever. |
Jifungie upanga wako pajani, wewe uliye hodari, Utukufu ni wako na fahari ni yako. Zaburi 45:3 |
Gird your sword on your thigh, mighty one: Your splendor and your majesty. |
Katika fahari yako usitawi uendelee Kwa ajili ya kweli na upole na haki Na mkono wako wa kuume Utakufundisha mambo ya kutisha. Zaburi 45:4 |
In your majesty ride on victoriously on behalf of truth, humility, and righteousness. Let your right hand display awesome deeds. |
Mishale yako ni mikali, watu huanguka chini yako; Imo mioyoni mwa adui za mfalme. Zaburi 45:5 |
Your arrows are sharp. The nations fall under you, with arrows in the heart of the king's enemies. |
Kiti chako cha enzi, Mungu, ni cha milele na milele, Fimbo ya ufalme wako ni fimbo ya adili. Zaburi 45:6 |
Your throne, God, is forever and ever. A scepter of equity is the scepter of your kingdom. |
Umeipenda haki; Umeichukia dhuluma. Kwa hiyo MUNGU, Mungu wako, amekupaka mafuta, Mafuta ya furaha kuliko wenzako. Zaburi 45:7 |
You have loved righteousness, and hated wickedness. Therefore God, your God, has anointed you with the oil of gladness above your fellows. |
Mavazi yako yote hunukia manemane Na udi na mdalasini. Katika majumba ya pembe Vinubi vimekufurahisha. Zaburi 45:8 |
All your garments smell like myrrh, aloes, and cassia. Out of ivory palaces stringed instruments have made you glad. |
Binti za wafalme wamo Miongoni mwa akina bibi wako wastahiki. Mkono wako wa kuume amesimama malkia Amevaa dhahabu ya Ofiri. Zaburi 45:9 |
Kings' daughters are among your honorable women. At your right hand the queen stands in gold of Ophir. |
Sikia, binti, utazame, utege sikio lako, Uwasahau watu wako na nyumba ya baba yako. Zaburi 45:10 |
Listen, daughter, consider, and turn your ear. Forget your own people, and also your father's house. |
Naye mfalme atautamani uzuri wako, Maana ndiye bwana wako, nawe umsujudie. Zaburi 45:11 |
So the king will desire your beauty, Honor him, for he is your lord. |
Na binti Tiro analeta kipawa chake, Nao matajiri wa watu watajipendekeza kwako. Zaburi 45:12 |
The daughter of Tyre comes with a gift. The rich among the people entreat your favor. |
Binti mfalme yumo ndani ana fahari tupu, Mavazi yake ni ya nyuzi za dhahabu. Zaburi 45:13 |
The princess inside is all glorious. Her clothing is interwoven with gold. |
Atapelekwa kwa mfalme Na mavazi yaliyofumwa kwa uzuri. Wanawali wenzake wanaomfuata, Watapelekwa kwako. Zaburi 45:14 |
She shall be led to the king in embroidered work. The virgins, her companions who follow her, shall be brought to you. |
Watapelekwa kwa furaha na shangwe, Na kuingia katika nyumba ya mfalme. Zaburi 45:15 |
With gladness and rejoicing they shall be led. They shall enter into the king's palace. |
Badala ya baba zako watakuwapo watoto wako, Utawafanya kuwa wakuu katika nchi zote. Zaburi 45:16 |
Your sons will take the place of your fathers. You shall make them princes in all the earth. |
Jina lako nitalifanya kuwa kumbukumbu Katika vizazi vyote. Kwa hiyo mataifa watakushukuru Milele na milele. Zaburi 45:17 |
I will make your name to be remembered in all generations. Therefore the peoples shall give you thanks forever and ever. {} |