Zaburi 45 Swahili & English

Listen/Download Audio
Zaburi 45 (Swahili) Psalms 45 (English)

Moyo wangu umefurika kwa neno jema, Mimi nasema niliyomfanyizia mfalme; Ulimi wangu ni kalamu ya mwandishi mstadi. Zaburi 45:1

> My heart overflows with a noble theme. I recite my verses for the king. My tongue is like the pen of a skillful writer.

Wewe u mzuri sana kuliko wanadamu; Neema imemiminiwa midomoni mwako, Kwa hiyo Mungu amekubariki hata milele. Zaburi 45:2

You are the most excellent of the sons of men. Grace has anointed your lips, Therefore God has blessed you forever.

Jifungie upanga wako pajani, wewe uliye hodari, Utukufu ni wako na fahari ni yako. Zaburi 45:3

Gird your sword on your thigh, mighty one: Your splendor and your majesty.

Katika fahari yako usitawi uendelee Kwa ajili ya kweli na upole na haki Na mkono wako wa kuume Utakufundisha mambo ya kutisha. Zaburi 45:4

In your majesty ride on victoriously on behalf of truth, humility, and righteousness. Let your right hand display awesome deeds.

Mishale yako ni mikali, watu huanguka chini yako; Imo mioyoni mwa adui za mfalme. Zaburi 45:5

Your arrows are sharp. The nations fall under you, with arrows in the heart of the king's enemies.

Kiti chako cha enzi, Mungu, ni cha milele na milele, Fimbo ya ufalme wako ni fimbo ya adili. Zaburi 45:6

Your throne, God, is forever and ever. A scepter of equity is the scepter of your kingdom.

Umeipenda haki; Umeichukia dhuluma. Kwa hiyo MUNGU, Mungu wako, amekupaka mafuta, Mafuta ya furaha kuliko wenzako. Zaburi 45:7

You have loved righteousness, and hated wickedness. Therefore God, your God, has anointed you with the oil of gladness above your fellows.

Mavazi yako yote hunukia manemane Na udi na mdalasini. Katika majumba ya pembe Vinubi vimekufurahisha. Zaburi 45:8

All your garments smell like myrrh, aloes, and cassia. Out of ivory palaces stringed instruments have made you glad.

Binti za wafalme wamo Miongoni mwa akina bibi wako wastahiki. Mkono wako wa kuume amesimama malkia Amevaa dhahabu ya Ofiri. Zaburi 45:9

Kings' daughters are among your honorable women. At your right hand the queen stands in gold of Ophir.

Sikia, binti, utazame, utege sikio lako, Uwasahau watu wako na nyumba ya baba yako. Zaburi 45:10

Listen, daughter, consider, and turn your ear. Forget your own people, and also your father's house.

Naye mfalme atautamani uzuri wako, Maana ndiye bwana wako, nawe umsujudie. Zaburi 45:11

So the king will desire your beauty, Honor him, for he is your lord.

Na binti Tiro analeta kipawa chake, Nao matajiri wa watu watajipendekeza kwako. Zaburi 45:12

The daughter of Tyre comes with a gift. The rich among the people entreat your favor.

Binti mfalme yumo ndani ana fahari tupu, Mavazi yake ni ya nyuzi za dhahabu. Zaburi 45:13

The princess inside is all glorious. Her clothing is interwoven with gold.

Atapelekwa kwa mfalme Na mavazi yaliyofumwa kwa uzuri. Wanawali wenzake wanaomfuata, Watapelekwa kwako. Zaburi 45:14

She shall be led to the king in embroidered work. The virgins, her companions who follow her, shall be brought to you.

Watapelekwa kwa furaha na shangwe, Na kuingia katika nyumba ya mfalme. Zaburi 45:15

With gladness and rejoicing they shall be led. They shall enter into the king's palace.

Badala ya baba zako watakuwapo watoto wako, Utawafanya kuwa wakuu katika nchi zote. Zaburi 45:16

Your sons will take the place of your fathers. You shall make them princes in all the earth.

Jina lako nitalifanya kuwa kumbukumbu Katika vizazi vyote. Kwa hiyo mataifa watakushukuru Milele na milele. Zaburi 45:17

I will make your name to be remembered in all generations. Therefore the peoples shall give you thanks forever and ever. {}