Zaburi BSB

Zaburi 141

Psalms Chapter 141

1
Ee Bwana, nimekuita, unijie hima, Uisikie sauti yangu nikuitapo.
A Psalm of David. I call upon You, O LORD; come quickly to me. Hear my voice when I call to You.
2
Sala yangu ipae mbele zako kama uvumba, Kuinuliwa mikono yangu kama dhabihu ya jioni.
May my prayer be set before You like incense; my uplifted hands, like the evening offering.
3
Ee Bwana, uweke mlinzi kinywani pangu, Mngojezi mlangoni pa midomo yangu.
Set a guard, O LORD, over my mouth; keep watch at the door of my lips.
4
Usiuelekeze moyo wangu kunako jambo baya, Nisiyazoelee matendo yasiyofaa, Pamoja na watu watendao maovu; Wala nisile vyakula vyao vya anasa.
Do not let my heart be drawn to any evil thing or take part in works of wickedness with men who do iniquity; let me not feast on their delicacies.
5
Mwenye haki na anipige, itakuwa fadhili; Anikemee, itakuwa kama mafuta kichwani; Kichwa changu kisikatae, Maana siachi kusali kati ya mabaya yao.
Let the righteous man strike me; let his rebuke be an act of loving devotion. It is oil for my head; let me not refuse it. For my prayer is ever against the deeds of the wicked.
6
Makadhi wao wakiangushwa kando ya genge, Watayasikia maneno yangu, maana ni matamu.
When their rulers are thrown down from the cliffs, the people will listen to my words, for they are pleasant.
7
Kama kupasua kuni na kuzichanja juu ya nchi, Ndivyo ilivyo mifupa yetu mdomoni pa kuzimu.
As when one plows and breaks up the soil, so our bones have been scattered at the mouth of Sheol.
8
Macho yangu yanakuelekea Wewe, MUNGU Bwana, Nimekukimbilia Wewe, usiniache nafsi yangu.
But my eyes are fixed on You, O GOD the Lord. In You I seek refuge; do not leave my soul defenseless.
9
Unilinde na mtego walionitegea, Na matanzi yao watendao maovu.
Keep me from the snares they have laid for me, and from the lures of evildoers.
10
Wabaya na waanguke katika nyavu zao wenyewe, Pindi mimi ninapopita salama.
Let the wicked fall into their own nets, while I pass by in safety.

Chagua Sura