Zaburi 91

Psalms Chapter 91

Download Audio (Pakua)
« Orodha ya Sura
English Translation
1
Aketiye mahali pa siri pake Aliye juu Atakaa katika uvuli wake Mwenyezi.
He who dwells in the secret place of the Most High Will rest in the shadow of the Almighty.
2
Nitasema, Bwana ndiye kimbilio langu na ngome yangu, Mungu wangu nitakayemtumaini.
I will say of Yahweh, "He is my refuge and my fortress; My God, in whom I trust."
3
Maana Yeye atakuokoa na mtego wa mwindaji, Na katika tauni iharibuyo.
For he will deliver you from the snare of the fowler, And from the deadly pestilence.
4
Kwa manyoya yake atakufunika, Chini ya mbawa zake utapata kimbilio; Uaminifu wake ni ngao na kigao.
He will cover you with his feathers. Under his wings you will take refuge. His faithfulness is your shield and rampart.
5
Hutaogopa hofu ya usiku, Wala mshale urukao mchana,
You shall not be afraid of the terror by night, Nor of the arrow that flies by day;
6
Wala tauni ipitayo gizani, Wala uele uharibuo adhuhuri,
Nor of the pestilence that walks in darkness, Nor of the destruction that wastes at noonday.
7
Ijapo watu elfu waanguka ubavuni pako. Naam, kumi elfu mkono wako wa kuume! Hata hivyo hautakukaribia wewe.
A thousand may fall at your side, And ten thousand at your right hand; But it will not come near you.
8
Ila kwa macho yako utatazama, Na kuyaona malipo ya wasio haki.
You will only look with your eyes, And see the recompense of the wicked.
9
Kwa kuwa Wewe Bwana ndiwe kimbilio langu; Umemfanya Aliye juu kuwa makao yako.
Because you have made Yahweh your refuge, And the Most High your dwelling place,
10
Mabaya hayatakupata wewe, Wala tauni haitaikaribia hema yako.
No evil shall happen to you, Neither shall any plague come near your dwelling.
11
Kwa kuwa atakuagizia malaika zake Wakulinde katika njia zako zote.
For he will give his angels charge over you, To guard you in all your ways.
12
Mikononi mwao watakuchukua, Usije ukajikwaa mguu wako katika jiwe.
They will bear you up in their hands, So that you won't dash your foot against a stone.
13
Utawakanyaga simba na nyoka, Mwana-simba na joka utawaseta kwa miguu.
You will tread on the lion and cobra. You will trample the young lion and the serpent underfoot.
14
Kwa kuwa amekaza kunipenda Nitamwokoa; na kumweka palipo juu, Kwa kuwa amenijua Jina langu.
"Because he has set his love on me, therefore I will deliver him. I will set him on high, because he has known my name.
15
Ataniita nami nitamwitikia; Nitakuwa pamoja naye taabuni, Nitamwokoa na kumtukuza;
He will call on me, and I will answer him. I will be with him in trouble. I will deliver him, and honor him.
16
Kwa siku nyingi nitamshibisha, Nami nitamwonyesha wokovu wangu.
I will satisfy him with long life, And show him my salvation."
« 90 92 »

Chagua Sura Nyingine (Select Chapter)