Zaburi 48

Psalms Chapter 48

Download Audio (Pakua)
« Orodha ya Sura
English Translation
1
Bwana ndiye aliye mkuu, Na mwenye kusifiwa sana. Katika mji wa Mungu wetu, Katika mlima wake mtakatifu.
> Great is Yahweh, and greatly to be praised, In the city of our God, in his holy mountain.
2
Kuinuka kwake ni mzuri sana, Ni furaha ya dunia yote. Mlima Sayuni pande za kaskazini, Mji wa Mfalme mkuu.
Beautiful in elevation, the joy of the whole earth, Is Mount Zion, on the north sides, The city of the great King.
3
Mungu katika majumba yake Amejijulisha kuwa ngome.
God has shown himself in her citadels as a refuge.
4
Maana, tazama, wafalme walikusanyika; Walipita wote pamoja.
For, behold, the kings assembled themselves, They passed by together.
5
Waliona, mara wakashangaa; Wakafadhaika na kukimbia.
They saw it, then they were amazed. They were dismayed, They hurried away.
6
Papo hapo tetemeko liliwashika, Utungu kama wa mwanamke azaaye.
Trembling took hold of them there, Pain, as of a woman in travail.
7
Kwa upepo wa mashariki Wavunja jahazi za Tarshishi.
With the east wind, you break the ships of Tarshish.
8
Kama tulivyosikia, ndivyo tulivyoona, Katika mji wa Bwana wa majeshi. Mji wa Mungu wetu; Mungu ataufanya imara hata milele.
As we have heard, so we have seen, In the city of Yahweh of Hosts, in the city of our God. God will establish it forever. Selah.
9
Tumezitafakari fadhili zako, Ee Mungu, Katikati ya hekalu lako.
We have thought about your loving kindness, God, In the midst of your temple.
10
Kama lilivyo jina lako, Ee Mungu, Ndivyo na sifa yako hata miisho ya dunia. Mkono wako wa kuume umejaa haki;
As is your name, God, So is your praise to the ends of the earth. Your right hand is full of righteousness.
11
Na ufurahi mlima Sayuni. Binti za Yuda na washangilie Kwa sababu ya hukumu zako.
Let Mount Zion be glad! Let the daughters of Judah rejoice, Because of your judgments.
12
Tembeeni katika Sayuni, Uzungukeni mji, Ihesabuni minara yake,
Walk about Zion, and go around her. Number its towers;
13
Tieni moyoni boma zake, Yafikirini majumba yake, Mpate kuwaambia kizazi kitakachokuja.
Mark well her bulwarks. Consider her palaces, That you may tell it to the next generation.
14
Kwa maana ndivyo alivyo MUNGU, Mungu wetu. Milele na milele Yeye ndiye atakayetuongoza.
For this God is our God forever and ever. He will be our guide even to death.
« 47 49 »

Chagua Sura Nyingine (Select Chapter)