Zaburi 125 Swahili & English

Listen/Download Audio
Zaburi 125 (Swahili) Psalms 125 (English)

Wamtumainio Bwana ni kama mlima Sayuni, Ambao hautatikisika, wakaa milele. Zaburi 125:1

> Those who trust in Yahweh are as Mount Zion, Which can't be moved, but remains forever.

Kama milima inavyouzunguka Yerusalemu, Ndivyo Bwana anavyowazunguka watu wake, Tangu sasa na hata milele. Zaburi 125:2

As the mountains surround Jerusalem, So Yahweh surrounds his people from this time forth and forevermore.

Kwa maana fimbo ya udhalimu Haitakaa juu ya fungu la wenye haki; Wenye haki wasije wakainyosha Mikono yao kwenye upotovu. Zaburi 125:3

For the scepter of wickedness won't remain over the allotment of the righteous; So that the righteous won't use their hands to do evil.

Ee Bwana, uwatendee mema walio wema, Nao walio wanyofu wa moyo. Zaburi 125:4

Do good, Yahweh, to those who are good, To those who are upright in their hearts.

Bali wao wanaozigeukia njia zao zilizopotoka, Bwana atawaondoa pamoja na watenda maovu. Amani ikae na Israeli. Zaburi 125:5

But as for those who turn aside to their crooked ways, Yahweh will lead them away with the workers of iniquity. Peace be on Israel.