Mungu, uisikie sauti yangu katika malalamiko yangu; Unilinde uhai wangu na hofu ya adui.
> Hear my voice, God, in my complaint. Preserve my life from fear of the enemy.
Utanificha mbali na shauri la siri la watenda mabaya, Mbali na ghasia ya watu wafanyao maovu;
Hide me from the conspiracy of the wicked, From the noisy crowd of the ones doing evil;
Waliounoa ulimi wao kama upanga, Wameielekeza mishale yao, maneno ya uchungu,
Who sharpen their tongue like a sword, And aim their arrows, deadly words,
Wapate kumpiga mkamilifu faraghani, Kwa ghafula humpiga wala hawaogopi.
To shoot innocent men from ambushes. They shoot at him suddenly and fearlessly.
Walijifanya hodari katika jambo baya; Hushauriana juu ya kutega mitego; Husema, Ni nani atakayeiona?
They encourage themselves in evil plans. They talk about laying snares secretly. They say, "Who will see them?"
Hutunga maovu; husema, Tumefanya shauri kamili; Na mawazo ya ndani ya kila mmoja wao, Na moyo wake, huwa siri kabisa.
They plot injustice, saying, "We have made a perfect plan!" Surely man's mind and heart are cunning.
Kwa hiyo Mungu atawapiga shabaha, Kwa mshale mara watapigwa.
But God will shoot at them. They will be suddenly struck down with an arrow.
Ndivyo watakavyokwazwa, Ulimi wao wenyewe ukishindana nao. Wote wawaonao watatikisa kichwa.
Their own tongues shall ruin them. All who see them will shake their heads.
Na watu wote wataogopa, Wataitangaza kazi ya Mungu, Na kuyafahamu matendo yake.
All mankind shall be afraid. They shall declare the work of God, And shall wisely ponder what he has done.
Mwenye haki atamfurahia Bwana na kumkimbilia, Na wote wenye moyo wa adili watajisifu.
The righteous shall be glad in Yahweh, And shall take refuge in him. All the upright in heart shall praise him!