Zaburi 19

Psalms Chapter 19

Download Audio (Pakua)
« Orodha ya Sura
English Translation
1
Mbingu zauhubiri utukufu wa Mungu, Na anga laitangaza kazi ya mikono yake.
> The heavens declare the glory of God. The expanse shows his handiwork.
2
Mchana husemezana na mchana, Usiku hutolea usiku maarifa.
Day after day they pour forth speech, And night after night they display knowledge.
3
Hakuna lugha wala maneno, Sauti yao haisikilikani.
There is no speech nor language, Where their voice is not heard.
4
Sauti yao imeenea duniani mwote, Na maneno yao hata miisho ya ulimwengu. Katika hizo ameliwekea jua hema,
Their voice has gone out through all the earth, Their words to the end of the world. In them he has set a tent for the sun,
5
Kama bwana arusi akitoka chumbani mwake, Lafurahi kama mtu aliye hodari Kwenda mbio katika njia yake.
Which is as a bridegroom coming out of his chamber, Like a strong man rejoicing to run his course.
6
Kutoka kwake lautoka mwisho wa mbingu, Na kuzunguka kwake hata miisho yake, Wala kwa hari yake Hakuna kitu kilichositirika.
His going forth is from the end of the heavens, His circuit to its ends; There is nothing hidden from its heat.
7
Sheria ya Bwana ni kamilifu, Huiburudisha nafsi. Ushuhuda wa Bwana ni amini, Humtia mjinga hekima.
Yahweh's law is perfect, restoring the soul. Yahweh's testimony is sure, making wise the simple.
8
Maagizo ya Bwana ni ya adili, Huufurahisha moyo. Amri ya Bwana ni safi, Huyatia macho nuru.
Yahweh's precepts are right, rejoicing the heart. Yahweh's commandment is pure, enlightening the eyes.
9
Kicho cha Bwana ni kitakatifu, Kinadumu milele. Hukumu za Bwana ni kweli, Zina haki kabisa.
The fear of Yahweh is clean, enduring forever. Yahweh's ordinances are true, and righteous altogether.
10
Ni za kutamanika kuliko dhahabu, Kuliko wingi wa dhahabu safi. Nazo ni tamu kuliko asali, Kuliko sega la asali.
More to be desired are they than gold, yes, than much fine gold; Sweeter also than honey and the extract of the honeycomb.
11
Tena mtumishi wako huonywa kwazo, Katika kuzishika kuna thawabu nyingi.
Moreover by them is your servant warned. In keeping them there is great reward.
12
Ni nani awezaye kuyatambua makosa yake? Unitakase na mambo ya siri.
Who can discern his errors? Forgive me from hidden errors.
13
Umzuie mtumishi wako asitende mambo ya kiburi, Yasinitawale mimi. Ndipo nitakapokuwa kamili, Nami nitakuwa safi, sina kosa lililo kubwa.
Keep back your servant also from presumptuous sins. Let them not have dominion over me. Then I will be upright, I will be blameless and innocent of great transgression.
14
Maneno ya kinywa changu, Na mawazo ya moyo wangu, Yapate kibali mbele zako, Ee Bwana, Mwamba wangu, na mwokozi wangu.
Let the words of my mouth and the meditation of my heart Be acceptable in your sight, Yahweh, my rock, and my redeemer.
« 18 20 »

Chagua Sura Nyingine (Select Chapter)