Zaburi 132

Psalms Chapter 132

Download Audio (Pakua)
« Orodha ya Sura
English Translation
1
Bwana, umkumbukie Daudi Taabu zake zote alizotaabika.
> Yahweh, remember David and all his affliction,
2
Ndiye aliyemwapia Bwana, Akaweka nadhiri kwa Shujaa wa Yakobo.
How he swore to Yahweh, And vowed to the Mighty One of Jacob:
3
Sitaingia hemani mwa nyumba yangu, Wala sitapanda matandiko ya kitanda changu;
"Surely I will not come into the structure of my house, Nor go up into my bed;
4
Sitaacha macho yangu kuwa na usingizi, Wala kope zangu kusinzia;
I will not give sleep to my eyes, Or slumber to my eyelids;
5
Hata nitakapompatia Bwana mahali, Na Shujaa wa Yakobo maskani.
Until I find out a place for Yahweh, A dwelling for the Mighty One of Jacob."
6
Tazama, tulisikia habari zake katika Efrata, Katika konde la Yearimu tuliiona.
Behold, we heard of it in Ephrathah. We found it in the field of Jaar:
7
Na tuingie katika maskani yake, Tusujudu penye kiti cha kuwekea miguu yake.
"We will go into his dwelling place. We will worship at his footstool.
8
Ee Bwana, uinuke, uende kwenye raha yako, Wewe na sanduku la nguvu zako.
Arise, Yahweh, into your resting place; You, and the ark of your strength.
9
Makuhani wako na wavikwe haki, Watauwa wako na washangilie.
Let your priest be clothed with righteousness. Let your saints shout for joy!"
10
Kwa ajili ya Daudi, mtumishi wako, Usiurudishe nyuma uso wa masihi
For your servant David's sake, Don't turn away the face of your anointed one.
11
Bwana amemwapia Daudi neno la kweli, Hatarudi nyuma akalihalifu, Baadhi ya wazao wa mwili wako Nitawaweka katika kiti chako cha enzi.
Yahweh has sworn to David in truth. He will not turn from it: "I will set the fruit of your body on your throne.
12
Wanao wakiyashika maagano yangu, Na shuhuda nitakazowafundisha; Watoto wao nao wataketi Katika kiti chako cha enzi milele.
If your children will keep my covenant, My testimony that I will teach them, Their children also will sit on your throne forevermore."
13
Kwa kuwa Bwana ameichagua Sayuni, Ameitamani akae ndani yake.
For Yahweh has chosen Zion. He has desired it for his habitation.
14
Hapo ndipo mahali pangu pa raha milele, Hapo nitakaa kwa maana nimepatamani.
"This is my resting place forever. Here I will live, for I have desired it.
15
Hakika nitavibariki vyakula vyake Wahitaji wake nitawashibisha chakula.
I will abundantly bless her provision. I will satisfy her poor with bread.
16
Na makuhani wake nitawavika wokovu, Na watauwa wake watashangilia.
Her priests I will also clothe with salvation. Her saints will shout aloud for joy.
17
Hapo nitamchipushia Daudi pembe, Na taa nimemtengenezea masihi wangu.
There I will make the horn of David to bud. I have ordained a lamp for my anointed.
18
Adui zake nitawavika aibu, Bali juu yake taji yake itasitawi.
I will clothe his enemies with shame, But on himself, his crown will be resplendant."
« 131 133 »

Chagua Sura Nyingine (Select Chapter)