Haleluya. Enyi watumishi wa Bwana, sifuni, Lisifuni jina la Bwana.
Praise Yah! Praise, you servants of Yahweh, Praise the name of Yahweh.
Jina la Bwana lihimidiwe Tangu leo na hata milele.
Blessed be the name of Yahweh, From this time forth and forevermore.
Toka maawio ya jua hata machweo yake Jina la Bwana husifiwa.
From the rising of the sun to the going down of the same, Yahweh's name is to be praised.
Bwana ni mkuu juu ya mataifa yote, Na utukufu wake ni juu ya mbingu.
Yahweh is high above all nations, His glory above the heavens.
Ni nani aliye mfano wa Bwana, Mungu wetu aketiye juu;
Who is like Yahweh, our God, Who has his seat on high,
Anyenyekeaye kutazama, Mbinguni na duniani?
Who stoops down to see in heaven and in the earth?
Humwinua mnyonge kutoka mavumbini, Na kumpandisha maskini kutoka jaani.
He raises up the poor out of the dust. Lifts up the needy from the ash heap;
Amketishe pamoja na wakuu, Pamoja na wakuu wa watu wake.
That he may set him with princes, Even with the princes of his people.
Huweka nyumbani mwanamke aliye tasa, Awe mama ya watoto mwenye furaha.
He settles the barren woman in her home, As a joyful mother of children. Praise Yah!