Zaburi 113

Psalms Chapter 113

Download Audio (Pakua)
« Orodha ya Sura
English Translation
1
Haleluya. Enyi watumishi wa Bwana, sifuni, Lisifuni jina la Bwana.
Praise Yah! Praise, you servants of Yahweh, Praise the name of Yahweh.
2
Jina la Bwana lihimidiwe Tangu leo na hata milele.
Blessed be the name of Yahweh, From this time forth and forevermore.
3
Toka maawio ya jua hata machweo yake Jina la Bwana husifiwa.
From the rising of the sun to the going down of the same, Yahweh's name is to be praised.
4
Bwana ni mkuu juu ya mataifa yote, Na utukufu wake ni juu ya mbingu.
Yahweh is high above all nations, His glory above the heavens.
5
Ni nani aliye mfano wa Bwana, Mungu wetu aketiye juu;
Who is like Yahweh, our God, Who has his seat on high,
6
Anyenyekeaye kutazama, Mbinguni na duniani?
Who stoops down to see in heaven and in the earth?
7
Humwinua mnyonge kutoka mavumbini, Na kumpandisha maskini kutoka jaani.
He raises up the poor out of the dust. Lifts up the needy from the ash heap;
8
Amketishe pamoja na wakuu, Pamoja na wakuu wa watu wake.
That he may set him with princes, Even with the princes of his people.
9
Huweka nyumbani mwanamke aliye tasa, Awe mama ya watoto mwenye furaha.
He settles the barren woman in her home, As a joyful mother of children. Praise Yah!
« 112 114 »

Chagua Sura Nyingine (Select Chapter)