Zaburi 113 Swahili & English

Listen/Download Audio
Zaburi 113 (Swahili) Psalms 113 (English)

Haleluya. Enyi watumishi wa Bwana, sifuni, Lisifuni jina la Bwana. Zaburi 113:1

Praise Yah! Praise, you servants of Yahweh, Praise the name of Yahweh.

Jina la Bwana lihimidiwe Tangu leo na hata milele. Zaburi 113:2

Blessed be the name of Yahweh, From this time forth and forevermore.

Toka maawio ya jua hata machweo yake Jina la Bwana husifiwa. Zaburi 113:3

From the rising of the sun to the going down of the same, Yahweh's name is to be praised.

Bwana ni mkuu juu ya mataifa yote, Na utukufu wake ni juu ya mbingu. Zaburi 113:4

Yahweh is high above all nations, His glory above the heavens.

Ni nani aliye mfano wa Bwana, Mungu wetu aketiye juu; Zaburi 113:5

Who is like Yahweh, our God, Who has his seat on high,

Anyenyekeaye kutazama, Mbinguni na duniani? Zaburi 113:6

Who stoops down to see in heaven and in the earth?

Humwinua mnyonge kutoka mavumbini, Na kumpandisha maskini kutoka jaani. Zaburi 113:7

He raises up the poor out of the dust. Lifts up the needy from the ash heap;

Amketishe pamoja na wakuu, Pamoja na wakuu wa watu wake. Zaburi 113:8

That he may set him with princes, Even with the princes of his people.

Huweka nyumbani mwanamke aliye tasa, Awe mama ya watoto mwenye furaha. Zaburi 113:9

He settles the barren woman in her home, As a joyful mother of children. Praise Yah!