Zaburi 52 Swahili & English

Listen/Download Audio
Zaburi 52 (Swahili) Psalms 52 (English)

Kwa nini kujisifia uovu, Ewe jabari? Wema wa Mungu upo sikuzote. Zaburi 52:1

> Why do you boast of mischief, mighty man? God's loving kindness endures continually.

Ulimi wako watunga madhara, Kama wembe mkali, Ewe mwenye hila Zaburi 52:2

Your tongue plots destruction, Like a sharp razor, working deceitfully.

Umependa mabaya kuliko mema, Na uongo kuliko kusema kweli. Zaburi 52:3

You love evil more than good, Lying rather than speaking the truth. Selah.

Umependa maneno yote ya kupoteza watu, Ewe ulimi wenye hila. Zaburi 52:4

You love all devouring words, You deceitful tongue.

Lakini Mungu atakuharibu hata milele; Atakuondolea mbali; Atakunyakua hemani mwako; Atakung'oa katika nchi ya walio hai. Zaburi 52:5

God will likewise destroy you forever. He will take you up, and pluck you out of your tent, And root you out of the land of the living. Selah.

Nao wenye haki wataona; Wataingiwa na hofu na kumcheka; Zaburi 52:6

The righteous also will see it, and fear, And laugh at him, saying,

Kumbe! Huyu ndiye mtu yule, Asiyemfanya Mungu kuwa nguvu zake. Aliutumainia wingi wa mali zake, Na kujifanya hodari kwa madhara yake. Zaburi 52:7

"Behold, this is the man who didn't make God his strength, But trusted in the abundance of his riches, And strengthened himself in his wickedness."

Bali mimi ni kama mzeituni Umeao katika nyumba ya Mungu. Nazitumainia fadhili za Mungu milele na milele. Zaburi 52:8

But as for me, I am like a green olive tree in God's house. I trust in God's loving kindness forever and ever.

Nitakushukuru milele kwa maana umetenda; Nitalingojea jina lako kwa kuwa ni jema; Mbele ya wacha Mungu wako. Zaburi 52:9

I will give you thanks forever, because you have done it. I will hope in your name, for it is good, In the presence of your saints.