Nitamhimidi Bwana kila wakati, Sifa zake zi kinywani mwangu daima.
> I will bless Yahweh at all times. His praise will always be in my mouth.
Katika Bwana nafsi yangu itajisifu, Wanyenyekevu wasikie wakafurahi.
My soul shall boast in Yahweh. The humble shall hear of it, and be glad.
Mtukuzeni Bwana pamoja nami, Na tuliadhimishe jina lake pamoja.
Oh magnify Yahweh with me. Let us exalt his name together.
Nalimtafuta Bwana akanijibu, Akaniponya na hofu zangu zote.
I sought Yahweh, and he answered me, And delivered me from all my fears.
Wakamwelekea macho wakatiwa nuru, Wala nyuso zao hazitaona haya.
They looked to him, and were radiant. Their faces shall never be covered with shame.
Maskini huyu aliita, Bwana akasikia, Akamwokoa na taabu zake zote.
This poor man cried, and Yahweh heard him, And saved him out of all his troubles.
Malaika wa Bwana hufanya kituo, Akiwazungukia wamchao na kuwaokoa.
The angel of Yahweh encamps round about those who fear him, And delivers them.
Onjeni mwone ya kuwa Bwana yu mwema; Heri mtu yule anayemtumaini.
Oh taste and see that Yahweh is good. Blessed is the man who takes refuge in him.
Mcheni Bwana, enyi watakatifu wake, Yaani, wamchao hawahitaji kitu.
Oh fear Yahweh, you his saints, For there is no lack with those who fear him.
Wana-simba hutindikiwa, huona njaa; Bali wamtafutao Bwana hawatahitaji kitu cho chote kilicho chema.
The young lions do lack, and suffer hunger, But those who seek Yahweh shall not lack any good thing.
Njoni, enyi wana, mnisikilize, Nami nitawafundisha kumcha Bwana.
Come, you children, listen to me. I will teach you the fear of Yahweh.
Ni nani mtu yule apendezwaye na uzima, Apendaye siku nyingi apate kuona mema?
Who is someone who desires life, And loves many days, that he may see good?
Uuzuie ulimi wako na mabaya, Na midomo yako na kusema hila.
Keep your tongue from evil, And your lips from speaking lies.
Uache mabaya ukatende mema, Utafute amani ukaifuatie.
Depart from evil, and do good. Seek peace, and pursue it.
Macho ya Bwana huwaelekea wenye haki, Na masikio yake hukielekea kilio chao.
Yahweh's eyes are toward the righteous. His ears listen to their cry.
Uso wa Bwana ni juu ya watenda mabaya, Aliondoe kumbukumbu lao duniani.
Yahweh's face is against those who do evil, To cut off the memory of them from the earth.
Walilia, naye Bwana akasikia, Akawaponya na taabu zao zote.
The righteous cry, and Yahweh hears, And delivers them out of all their troubles.
Bwana yu karibu nao waliovunjika moyo, Na waliopondeka roho huwaokoa.
Yahweh is near to those who have a broken heart, And saves those who have a crushed spirit.
Mateso ya mwenye haki ni mengi, Lakini Bwana humponya nayo yote.
Many are the afflictions of the righteous, But Yahweh delivers him out of them all.
Huihifadhi mifupa yake yote, Haukuvunjika hata mmoja.
He protects all of his bones. Not one of them is broken.
Uovu utamwua asiye haki, Nao wamchukiao mwenye haki watahukumiwa.
Evil shall kill the wicked. Those who hate the righteous shall be condemned.
Bwana huzikomboa nafsi za watumishi wake, Wala hawatahukumiwa wote wamkimbiliao.
Yahweh redeems the soul of his servants. None of those who take refuge in him shall be condemned.