Zaburi 30 Swahili & English

Listen/Download Audio
Zaburi 30 (Swahili) Psalms 30 (English)

Ee Bwana, nitakutukuza kwa maana umeniinua, Wala hukuwafurahisha adui zangu juu yangu. Zaburi 30:1

> I will extol you, Yahweh, for you have raised me up, And have not made my foes to rejoice over me.

Ee Bwana, Mungu wangu, Nalikulilia ukaniponya. Zaburi 30:2

Yahweh my God, I cried to you, And you have healed me.

Umeniinua nafsi yangu, Ee Bwana, kutoka kuzimu. Umenihuisha na kunitoa Miongoni mwao washukao shimoni. Zaburi 30:3

Yahweh, you have brought up my soul from Sheol. You have kept me alive, that I should not go down to the pit.

Mwimbieni Bwana zaburi, Enyi watauwa wake. Na kufanya shukrani. Kwa kumbukumbu la utakatifu wake. Zaburi 30:4

Sing praise to Yahweh, you saints of his. Give thanks to his holy name.

Maana ghadhabu zake ni za kitambo kidogo, Katika radhi yake mna uhai. Huenda kilio huja kukaa usiku, Lakini asubuhi huwa furaha. Zaburi 30:5

For his anger is but for a moment; His favor is for a lifetime. Weeping may stay for the night, But joy comes in the morning.

Nami nilipofanikiwa nalisema, Sitaondoshwa milele. Zaburi 30:6

As for me, I said in my prosperity, "I shall never be moved."

Bwana, kwa radhi yako Wewe uliuimarisha mlima wangu. Uliuficha uso wako, Nami nikafadhaika. Zaburi 30:7

You, Yahweh, when you favored me, made my mountain to stand strong. But when you hid your face, I was troubled.

Ee Bwana, nalikulilia Wewe, Naam, kwa Bwana naliomba dua. Zaburi 30:8

I cried to you, Yahweh. To Yahweh I made supplication:

Mna faida gani katika damu yangu Nishukapo shimoni? Mavumbi yatakusifu? Yataitangaza kweli yako? Zaburi 30:9

"What profit is there in my destruction, if I go down to the pit? Shall the dust praise you? Shall it declare your truth?

Ee Bwana, usikie, unirehemu, Bwana, uwe msaidizi wangu. Zaburi 30:10

Hear, Yahweh, and have mercy on me. Yahweh, be my helper."

Uligeuza matanga yangu kuwa machezo; Ulinivua gunia, ukanivika furaha. Zaburi 30:11

You have turned my mourning into dancing for me. You have removed my sackcloth, and clothed me with gladness,

Ili utukufu wangu ukusifu, Wala usinyamaze. Ee Bwana, Mungu wangu, Nitakushukuru milele. Zaburi 30:12

To the end that my heart may sing praise to you, and not be silent. Yahweh my God, I will give thanks to you forever!