Zaburi 26 Swahili & English
Listen/Download AudioZaburi 26 (Swahili) | Psalms 26 (English) |
---|---|
Ee Bwana, unihukumu mimi, Maana nimekwenda kwa ukamilifu wangu, Nami nimemtumaini Bwana bila wasiwasi. Zaburi 26:1 |
> Judge me, Yahweh, for I have walked in my integrity. I have trusted also in Yahweh without wavering. |
Ee Bwana, unijaribu na kunipima; Unisafishe mtima wangu na moyo wangu. Zaburi 26:2 |
Examine me, Yahweh, and prove me. Try my heart and my mind. |
Maana fadhili zako zi mbele ya macho yangu, Nami nimekwenda katika kweli yako. Zaburi 26:3 |
For your loving kindness is before my eyes. I have walked in your truth. |
Sikuketi pamoja na watu wa ubatili, Wala sitaingia mnamo wanafiki. Zaburi 26:4 |
I have not sat with deceitful men, Neither will I go in with hypocrites. |
Nimelichukia kusanyiko la watenda mabaya, Wala sitaketi pamoja na watu waovu. Zaburi 26:5 |
I hate the assembly of evil-doers, And will not sit with the wicked. |
Nitanawa mikono yangu kwa kutokuwa na hatia, Na kuizunguka madhabahu yako, Ee Bwana Zaburi 26:6 |
I will wash my hands in innocence, So I will go about your altar, Yahweh; |
Ili niitangaze sauti ya kushukuru, Na kuzisimulia kazi zako za ajabu. Zaburi 26:7 |
That I may make the voice of thanksgiving to be heard, And tell of all your wondrous works. |
Bwana, nimependa makao ya nyumba yako, Na mahali pa maskani ya utukufu wako. Zaburi 26:8 |
Yahweh, I love the habitation of your house, The place where your glory dwells. |
Usiiondoe nafsi yangu pamoja na wakosaji, Wala uhai wangu pamoja na watu wa damu. Zaburi 26:9 |
Don't gather my soul with sinners, Nor my life with bloodthirsty men; |
Mikononi mwao mna madhara, Na mkono wao wa kuume umejaa rushwa. Zaburi 26:10 |
In whose hands is wickedness, Their right hand is full of bribes. |
Ila mimi nitakwenda kwa ukamilifu wangu; Unikomboe, unifanyie fadhili. Zaburi 26:11 |
But as for me, I will walk in my integrity. Redeem me, and be merciful to me. |
Mguu wangu umesimama palipo sawa; Katika makusanyiko nitamhimidi Bwana. Zaburi 26:12 |
My foot stands in an even place. In the congregations I will bless Yahweh. |