Zaburi 22 Swahili & English

Listen/Download Audio
Zaburi 22 (Swahili) Psalms 22 (English)

Mungu wangu, Mungu wangu, Mbona umeniacha? Mbona U mbali na wokovu wangu, Na maneno ya kuugua kwangu? Zaburi 22:1

> My God, my God, why have you forsaken me? Why are you so far from helping me, and from the words of my groaning?

Ee Mungu wangu, nalia mchana lakini hujibu Na wakati wa usiku lakini sipati raha. Zaburi 22:2

My God, I cry in the daytime, but you don't answer; In the night season, and am not silent.

Na Wewe U Mtakatifu, Uketiye juu ya sifa za Israeli. Zaburi 22:3

But you are holy, You who inhabit the praises of Israel.

Baba zetu walikutumaini Wewe, Walitumaini, na Wewe ukawaokoa. Zaburi 22:4

Our fathers trusted in you. They trusted, and you delivered them.

Walikulilia Wewe wakaokoka, Walikutumaini wasiaibike. Zaburi 22:5

They cried to you, and were delivered. They trusted in you, and were not disappointed.

Lakini mimi ni mdudu wala si mtu, Laumu ya wanadamu na mzaha wa watu. Zaburi 22:6

But I am a worm, and no man; A reproach of men, and despised by the people.

Wote wanionao hunicheka sana, Hunifyonya, wakitikisa vichwa vyao; Zaburi 22:7

All those who see me mock me. They insult me with their lips. They shake their heads, saying,

Husema, Umtegemee Bwana; na amponye; Na amwokoe sasa, maana apendezwa naye. Zaburi 22:8

"He trusts in Yahweh; Let him deliver him; Let him rescue him, since he delights in him."

Naam, Wewe ndiwe uliyenitoa tumboni, Ulinitumainisha matitini mwa mama yangu. Zaburi 22:9

But you brought me out of the womb. You made me trust at my mother's breasts.

Kwako nalitupwa tangu tumboni, Toka tumboni mwa mamangu ndiwe Mungu wangu. Zaburi 22:10

I was thrown on you from my mother's womb. You are my God since my mother bore me.

Usiwe mbali nami maana taabu i karibu, Kwa maana hakuna msaidizi. Zaburi 22:11

Don't be far from me, for trouble is near. For there is none to help.

Mafahali wengi wamenizunguka, Walio hodari wa Bashani wamenisonga; Zaburi 22:12

Many bulls have surrounded me. Strong bulls of Bashan have encircled me.

Wananifumbulia vinywa vyao, Kama simba apapuraye na kunguruma. Zaburi 22:13

They open their mouths wide against me, Lions tearing prey and roaring.

Nimemwagika kama maji, Mifupa yangu yote imeteguka, Moyo wangu umekuwa kama nta, Na kuyeyuka ndani ya mtima wangu. Zaburi 22:14

I am poured out like water. All my bones are out of joint. My heart is like wax; It is melted within me.

Nguvu zangu zimekauka kama gae, Ulimi wangu waambatana na taya zangu; Unaniweka katika mavumbi ya mauti Zaburi 22:15

My strength is dried up like a potsherd. My tongue sticks to the roof of my mouth. You have brought me into the dust of death.

Kwa maana mbwa wamenizunguka; Kusanyiko la waovu wamenisonga; Wamenizua mikono na miguu. Zaburi 22:16

For dogs have surrounded me. A company of evil-doers have enclosed me. They pierced my hands and my feet.

Naweza kuihesabu mifupa yangu yote; Wao wananitazama na kunikodolea macho. Zaburi 22:17

I can count all of my bones. They look and stare at me.

Wanagawanya nguo zangu, Na vazi langu wanalipigia kura. Zaburi 22:18

They divide my garments among them. They cast lots for my clothing.

Nawe, Bwana, usiwe mbali, Ee Nguvu zangu, fanya haraka kunisaidia. Zaburi 22:19

But don't be far off, Yahweh. You are my help: hurry to help me.

Uniponye nafsi yangu na upanga, Mpenzi wangu na nguvu za mbwa. Zaburi 22:20

Deliver my soul from the sword, My precious life from the power of the dog.

Kinywani mwa simba uniokoe; Naam, toka pembe za nyati umenijibu. Zaburi 22:21

Save me from the lion's mouth; Yes, from the horns of the wild oxen you have answered me.

Nitalihubiri jina lako kwa ndugu zangu, Katikati ya kusanyiko nitakusifu. Zaburi 22:22

I will declare your name to my brothers. In the midst of the assembly, I will praise you.

Ninyi mnaomcha Bwana, msifuni, Enyi nyote mlio wazao wa Yakobo, mtukuzeni, Mcheni, enyi nyote mlio wazao wa Israeli. Zaburi 22:23

You who fear Yahweh, praise him! All you descendants of Jacob, glorify him! Stand in awe of him, all you descendants of Israel!

Maana hakulidharau teso la mteswa, Wala hakuchukizwa nalo; Wala hakumficha uso wake, Bali alipomlilia akamsikia. Zaburi 22:24

For he has not despised nor abhorred the affliction of the afflicted, Neither has he hidden his face from him; But when he cried to him, he heard.

Kwako zinatoka sifa zangu Katika kusanyiko kubwa. Nitaziondoa nadhiri zangu Mbele yao wamchao. Zaburi 22:25

Of you comes my praise in the great assembly. I will pay my vows before those who fear him.

Wapole watakula na kushiba, Wamtafutao Bwana watamsifu; Mioyo yenu na iishi milele. Zaburi 22:26

The humble shall eat and be satisfied. They shall praise Yahweh who seek after him. Let your hearts live forever.

Miisho yote ya dunia itakumbuka, Na watu watamrejea Bwana; Jamaa zote za mataifa watamsujudia. Zaburi 22:27

All the ends of the earth shall remember and turn to Yahweh. All the relatives of the nations shall worship before you.

Maana ufalme una Bwana, Naye ndiye awatawalaye mataifa. Zaburi 22:28

For the kingdom is Yahweh's. He is the ruler over the nations.

Wakwasi wote wa dunia watakula na kusujudu, Humwinamia wote washukao mavumbini; Naam, yeye asiyeweza kujihuisha nafsi yake, Zaburi 22:29

All the rich ones of the earth shall eat and worship. All those who go down to the dust shall bow before him, Even he who can't keep his soul alive.

Wazao wake watamtumikia. Zitasimuliwa habari za Bwana, Kwa kizazi kitakachokuja, Zaburi 22:30

Posterity shall serve him. Future generations shall be told about the Lord.

Nao watawahubiri watakaozaliwa haki yake, Ya kwamba ndiye aliyeyafanya. Zaburi 22:31

They shall come and shall declare his righteousness to a people that shall be born, For he has done it.