Zaburi BSB

Zaburi 72

Psalms Chapter 72

1
Ee Mungu, mpe mfalme hukumu zako, Na mwana wa mfalme haki yako.
Of Solomon. Endow the king with Your justice, O God, and the son of the king with Your righteousness.
2
Atawaamua watu wako kwa haki, Na watu wako walioonewa kwa hukumu.
May he judge Your people with righteousness and Your afflicted with justice.
3
Milima itawazalia watu amani, Na vilima navyo kwa haki.
May the mountains bring peace to the people, and the hills bring righteousness.
4
Atawahukumu walioonewa wa watu, Atawaokoa wahitaji, atamseta mwenye kuonea.
May he vindicate the afflicted among the people; may he save the children of the needy and crush the oppressor.
5
Watakuogopa wakati wote wa kudumu jua, Na wakati wa kung'aa mwezi kizazi hata kizazi.
May they fear him as long as the sun shines, as long as the moon remains, through all generations.
6
Atashuka kama mvua juu ya majani yaliyokatwa, Kama manyunyu yainyweshayo nchi.
May he be like rain that falls on freshly cut grass, like spring showers that water the earth.
7
Siku zake yeye, mtu mwenye haki atasitawi, Na wingi wa amani hata mwezi utakapokoma.
May the righteous flourish in his days and prosperity abound until the moon is no more.
8
Na awe na enzi toka bahari hata bahari, Toka Mto hata miisho ya dunia.
May he rule from sea to sea, and from the Euphrates to the ends of the earth.
9
Wakaao jangwani na wainame mbele zake; Adui zake na warambe mavumbi.
May the nomads bow before him, and his enemies lick the dust.
10
Wafalme wa Tarshishi na visiwa na walete kodi; Wafalme wa Sheba na Seba na watoe vipawa.
May the kings of Tarshish and distant shores bring tribute; may the kings of Sheba and Seba offer gifts.
11
Naam, wafalme wote na wamsujudie; Na mataifa yote wamtumikie.
May all kings bow down to him and all nations serve him.
12
Kwa maana atamkomboa mhitaji aliapo, Na mtu aliyeonewa iwapo hana msaidizi.
For he will deliver the needy who cry out and the afflicted who have no helper.
13
Atamhurumia aliye dhaifu na maskini, Na nafsi za wahitaji ataziokoa.
He will take pity on the poor and needy and save the lives of the oppressed.
14
Atawakomboa nafsi zao na kuonewa na udhalimu, Na damu yao ina thamani machoni pake.
He will redeem them from oppression and violence, for their blood is precious in his sight.
15
Basi na aishi; Na wampe dhahabu ya Sheba; Na wamwombee daima; Na kumbariki mchana kutwa.
Long may he live! May gold from Sheba be given him. May people ever pray for him; may they bless him all day long.
16
Na uwepo wingi wa nafaka Katika ardhi juu ya milima; Matunda yake na yawaye-waye kama Lebanoni, Na watu wa mjini wasitawi kama majani ya nchi.
May there be an abundance of grain in the land; may it sway atop the hills. May its fruit trees flourish like the forests of Lebanon, the people of its cities like the grass of the field.
17
Jina lake na lidumu milele, Pindi ling'aapo jua jina lake liwe na wazao; Mataifa yote na wajibariki katika yeye, Na kumwita heri.
May his name endure forever; may his name continue as long as the sun shines. In him may all nations be blessed; may they call him blessed.
18
Na ahimidiwe Bwana, Mungu, Mungu wa Israeli, Atendaye miujiza Yeye peke yake;
Blessed be the LORD God, the God of Israel, who alone does marvelous deeds.
19
Jina lake tukufu na lihimidiwe milele; Dunia yote na ijae utukufu wake. Amina na Amina.
And blessed be His glorious name forever; may all the earth be filled with His glory. Amen and amen.
20
Maombi ya Daudi mwana wa Yese yamekwisha.
Thus conclude the prayers of David son of Jesse.

Chagua Sura