1 Mambo ya Nyakati 9

1st Chronicles Chapter 9

Download Audio (Pakua)
« Orodha ya Sura
English Translation
1
Hivyo Israeli wote walihesabiwa kwa nasaba; na tazama, hizo zimeandikwa katika kitabu cha wafalme wa Israeli; na Yuda wakachukuliwa mateka mpaka Babeli, kwa sababu ya makosa yao.
So all Israel were reckoned by genealogies; and, behold, they are written in the book of the kings of Israel: and Judah was carried away captive to Babylon for their disobedience.
2
Basi wenyeji wa kwanza waliokaa katika hozi zao katika miji yao walikuwa Israeli, na makuhani, na Walawi, na Wanethini.
Now the first inhabitants who lived in their possessions in their cities were Israel, the priests, the Levites, and the Nethinim.
3
Na huko Yerusalemu walikuwa wakikaa baadhi ya wana wa Yuda, na wana wa Benyamini, na wana wa Efraimu na Manase;
In Jerusalem lived of the children of Judah, and of the children of Benjamin, and of the children of Ephraim and Manasseh:
4
Uthai, mwana wa Amihudi, mwana wa Omri, mwana wa Imli, mwana wa Bani, wa wana wa Peresi, mwana wa Yuda.
Uthai the son of Ammihud, the son of Omri, the son of Imri, the son of Bani, of the children of Perez the son of Judah.
5
Na wa Washiloni; Asaya, mzaliwa wa kwanza, na wanawe.
Of the Shilonites: Asaiah the firstborn, and his sons.
6
Na wa wana wa Zera; Yeueli, na ndugu zao; watu mia sita na tisini.
Of the sons of Zerah: Jeuel, and their brothers, six hundred ninety.
7
Na wa wana wa Benyamini; Salu, mwana wa Meshulamu, mwana wa Hodavia, mwana wa Hasenua;
Of the sons of Benjamin: Sallu the son of Meshullam, the son of Hodaviah, the son of Hassenuah,
8
na Ibneya, mwana wa Yerohamu; na Ela, mwana wa Uzi, mwana wa Mikri; na Meshulamu, mwana wa Shefatia, mwana wa Reueli, mwana wa Ibniya;
and Ibneiah the son of Jeroham, and Elah the son of Uzzi, the son of Michri, and Meshullam the son of Shephatiah, the son of Reuel, the son of Ibnijah;
9
na ndugu zao, sawasawa na vizazi vyao; watu mia kenda na hamsini na sita. Watu hao wote ndio waliokuwa wakuu wa mbari za baba zao, kwa kadiri ya mbari za baba zao.
and their brothers, according to their generations, nine hundred fifty-six. All these men were heads of fathers' [houses] by their fathers' houses.
10
Na katika makuhani; Yedaya, na Yehoyaribu, na Yakini;
Of the priests: Jedaiah, and Jehoiarib, Jachin,
11
na Azaria, mwana wa Hilkia, mwana wa Meshulamu, mwana wa Sadoki, mwana wa Merayothi, mwana wa Ahitubu, mkuu wa nyumba ya Mungu;
and Azariah the son of Hilkiah, the son of Meshullam, the son of Zadok, the son of Meraioth, the son of Ahitub, the ruler of the house of God;
12
na Adaya, mwana wa Yerohamu, mwana wa Pashuri, mwana wa Malkiya; na Maasai, mwana wa Adieli, mwana wa Yazera, mwana wa Meshulamu, mwana wa Meshilemithi, mwana wa Imeri;
and Adaiah the son of Jeroham, the son of Pashhur, the son of Malchijah, and Maasai the son of Adiel, the son of Jahzerah, the son of Meshullam, the son of Meshillemith, the son of Immer;
13
wakuu wa mbari za baba zao; pamoja na ndugu zao; watu elfu na mia saba na sitini; watu wenye ustadi waliofaa sana kwa kazi ya huduma ya nyumba ya Mungu.
and their brothers, heads of their fathers' houses, one thousand seven hundred sixty; very able men for the work of the service of the house of God.
14
Na katika Walawi; Shemaya, mwana wa Hashubu, mwana wa Azrikamu, mwana wa Hashabia, wa wana wa Merari;
Of the Levites: Shemaiah the son of Hasshub, the son of Azrikam, the son of Hashabiah, of the sons of Merari;
15
na Bakbakari, na Hereshi, na Galali, na Matania, mwana wa Mika, mwana wa Zikri, mwana wa Asafu;
and Bakbakkar, Heresh, and Galal, and Mattaniah the son of Mica, the son of Zichri, the son of Asaph,
16
na Obadia, mwana wa Shemaya, mwana wa Galali, mwana wa Yeduthuni; na Berekia, mwana wa Asa, mwana wa Elkana; waliokaa katika vijiji vya Wanetofathi.
and Obadiah the son of Shemaiah, the son of Galal, the son of Jeduthun, and Berechiah the son of Asa, the son of Elkanah, who lived in the villages of the Netophathites.
17
Na katika mabawabu; Shalumu, na Akubu, na Talmoni, na Ahimani, na ndugu zao; naye Shalumu alikuwa mkuu wao;
The porters: Shallum, and Akkub, and Talmon, and Ahiman, and their brothers (Shallum was the chief),
18
ambao tangu hapo walikuwa wakingojea penye lango la mfalme upande wa mashariki; hao ndio waliokuwa wangojezi wa rago la wana wa Lawi.
who hitherto [waited] in the king's gate eastward: they were the porters for the camp of the children of Levi.
19
Naye Shalumu, mwana wa Kore, mwana wa Ebiasafu, mwana wa Kora; pamoja na nduguze wa mbari ya babaye, Wakora; walikuwa wakiisimamia kazi hiyo ya huduma, wenye ungojezi wa malango ya maskani; na baba zao walikuwa wamesimamia matuo ya Bwana, wakiyalinda maingilio;
Shallum the son of Kore, the son of Ebiasaph, the son of Korah, and his brothers, of his father's house, the Korahites, were over the work of the service, keepers of the thresholds of the tent: and their fathers had been over the camp of Yahweh, keepers of the entry.
20
naye Finehasi, mwana wa Eleazari, alikuwa mkuu wao hapo zamani, naye Bwana alikuwa pamoja naye.
Phinehas the son of Eleazar was ruler over them in time past, [and] Yahweh was with him.
21
Zekaria, mwana wa Meshelemia, alikuwa bawabu mlangoni pa ile hema ya kukutania.
Zechariah the son of Meshelemiah was porter of the door of the tent of meeting.
22
Hao wote waliochaguliwa kuwa wangojezi wa malango walikuwa watu mia mbili na kumi na wawili. Nao wakahesabiwa kwa nasaba katika vijiji vyao, ambao Daudi na Samweli, huyo mwonaji, walikuwa wamewaweka katika kazi yao waliyoamaniwa.
All these who were chosen to be porters in the thresholds were two hundred and twelve. These were reckoned by genealogy in their villages, whom David and Samuel the seer did ordain in their office of trust.
23
Basi watu hao na wana wao walikuwa na usimamizi wa malango ya nyumba ya Bwana, yaani, nyumba ya maskani, kwa zamu.
So they and their children had the oversight of the gates of the house of Yahweh, even the house of the tent, by wards.
24
Hao wangojezi walikuwapo pande zote nne, kuelekea mashariki, na magharibi, na kaskazini, na kusini.
On the four sides were the porters, toward the east, west, north, and south.
25
Na ndugu zao, katika vijiji vyao, wakaamaniwa kuingia kila siku ya saba, zamu kwa zamu, ili kuwa pamoja nao;
Their brothers, in their villages, were to come in every seven days from time to time to be with them:
26
kwa maana wale wangojezi wanne, waliokuwa wakuu, nao ni Walawi, walikuwa na kazi ya kuamaniwa, tena walikuwa juu ya vyumba na juu ya hazina katika nyumba ya Mungu.
for the four chief porters, who were Levites, were in an office of trust, and were over the chambers and over the treasuries in the house of God.
27
Nao wakalala kandokando nyumbani mwa Mungu, kwa kuwa ulinzi wake ulikuwa juu yao, nayo ilikuwa kazi yao kuyafungua malango asubuhi baada ya asubuhi.
They lodged round about the house of God, because the charge [of it] was on them; and to them pertained the opening of it morning by morning.
28
Na baadhi yao walikuwa na ulinzi wa vyombo vya huduma; kwani huingizwa kwa hesabu, na kutolewa kwa hesabu vile vile.
Certain of them had charge of the vessels of service; for by count were these brought in and by count were these taken out.
29
Na baadhi yao waliamaniwa kuviangalia vyombo vya nyumbani, na vyombo vyote vya Patakatifu; na kuwa juu ya unga safi, na divai, na mafuta, na ubani, na manukato.
Some of them also were appointed over the furniture, and over all the vessels of the sanctuary, and over the fine flour, and the wine, and the oil, and the frankincense, and the spices.
30
Na baadhi ya wana wa makuhani waliweka tayari machanganyiko ya manukato.
Some of the sons of the priests prepared the confection of the spices.
31
Naye Matithia, Mlawi mmojawapo, aliyekuwa mzaliwa wa kwanza wa Shalumu, Mkora, aliamaniwa kazi ya kuviangalia vitu vile vilivyookwa kaangoni.
Mattithiah, one of the Levites, who was the firstborn of Shallum the Korahite, had the office of trust over the things that were baked in pans.
32
Na baadhi ya ndugu zao, wa wana wa Wakohathi, walikuwa juu ya mikate ile ya Wonyesho, ili kuiandaa kila sabato.
Some of their brothers, of the sons of the Kohathites, were over the show bread, to prepare it every Sabbath.
33
Tena hawa ndio waimbaji, wakuu wa mbari za baba zao katika Walawi, ambao walikaa vyumbani, kisha walikuwa hawana kazi nyingine; kwa kuwa walitumika katika kazi yao mchana na usiku.
These are the singers, heads of fathers' [houses] of the Levites, [who lived] in the chambers [and were] free [from other service]; for they were employed in their work day and night.
34
Hao walikuwa wakuu wa mbari za baba zao katika Walawi, katika vizazi vyao vyote, watu wakuu; nao walikuwa wakikaa huko Yerusalemu.
These were heads of fathers' [houses] of the Levites, throughout their generations, chief men: these lived at Jerusalem.
35
Basi huko Gibea alikaa babaye Gibea, jina lake Yeieli, na jina la mkewe aliitwa Maaka;
In Gibeon there lived the father of Gibeon, Jeiel, whose wife's name was Maacah:
36
na mwanawe, mzaliwa wake wa kwanza, alikuwa Abdoni; na Suri, na Kishi, na Baali, na Meri, na Nadabu;
and his firstborn son Abdon, and Zur, and Kish, and Baal, and Ner, and Nadab,
37
na Gedori, na Ahio, na Zekaria, na Miklothi.
and Gedor, and Ahio, and Zechariah, and Mikloth.
38
Na Miklothi akamzaa Shimea. Hao nao walikuwa wakikaa pamoja na ndugu zao huko Yerusalemu, kuwakabili ndugu zao.
Mikloth became the father of Shimeam. They also lived with their brothers in Jerusalem, over against their brothers.
39
Naye Neri akamzaa Kishi; na Kishi akamzaa Sauli; na Sauli akamzaa Yonathani, na Malkishua, na Abinadabu, na Eshbaali.
Ner became the father of Kish; and Kish became the father of Saul; and Saul became the father of Jonathan, and Malchishua, and Abinadab, and Eshbaal.
40
Na mwana wa Yonathani alikuwa Meribaali; na Meribaali akamzaa Mika.
The son of Jonathan was Merib Baal; and Merib Baal became the father of Micah.
41
Na wana wa Mika; Pithoni, na Meleki, na Tarea.
The sons of Micah: Pithon, and Melech, and Tahrea, [and Ahaz].
42
Na Ahazi akamzaa Yara; na Yara akamzaa Alemethi, na Azmawethi, na Zimri; na Zimri akamzaa Mosa;
Ahaz became the father of Jarah; and Jarah became the father of Alemeth, and Azmaveth, and Zimri; and Zimri became the father of Moza;
43
na Mosa akamzaa Binea; na mwanawe huyo alikuwa Refaya, na mwanawe huyo ni Eleasa, na mwanawe huyo ni Aseli;
and Moza became the father of Binea; and Rephaiah his son, Eleasah his son, Azel his son.
44
naye Aseli alikuwa na wana sita, ambao majina yao ni haya; Azrikamu, na Bokeru, na Ishmaeli, na Shearia, na Obadia, na Hanani. Hao wote walikuwa wana wa Aseli
Azel had six sons, whose names are these: Azrikam, Bocheru, and Ishmael, and Sheariah, and Obadiah, and Hanan: these were the sons of Azel.
« 8 10 »

Chagua Sura Nyingine (Select Chapter)