1 Mambo ya Nyakati BSB

1 Mambo ya Nyakati 6

1st Chronicles Chapter 6

1
Wana wa Lawi; Gershoni, na Kohathi, na Merari.
The sons of Levi: Gershon, Kohath, and Merari.
2
Na wana wa Kohathi; Amramu, na Ishari, na Hebroni, na Uzieli.
The sons of Kohath: Amram, Izhar, Hebron, and Uzziel.
3
Na wana wa Amramu; Haruni, na Musa, na Miriamu. Na wana wa Haruni; Nadabu, na Abihu, na Eleazari, na Ithamari.
The children of Amram: Aaron, Moses, and Miriam. The sons of Aaron: Nadab, Abihu, Eleazar, and Ithamar.
4
Eleazari akamzaa Finehasi; na Finehasi akamzaa Abishua;
Eleazar was the father of Phinehas, Phinehas was the father of Abishua,
5
na Abishua akamzaa Buki; na Buki akamzaa Uzi;
Abishua was the father of Bukki, Bukki was the father of Uzzi,
6
na Uzi akamzaa Zerahia; na Zerahia akamzaa Merayothi,
Uzzi was the father of Zerahiah, Zerahiah was the father of Meraioth,
7
na Merayothi akamzaa Amaria; na Amaria akamzaa Ahitubu;
Meraioth was the father of Amariah, Amariah was the father of Ahitub,
8
na Ahitubu akamzaa Sadoki; na Sadoki akamzaa Ahimaasi;
Ahitub was the father of Zadok, Zadok was the father of Ahimaaz,
9
na Ahimaasi akamzaa Azaria; na Azaria akamzaa Yohana;
Ahimaaz was the father of Azariah, Azariah was the father of Johanan,
10
na Yohana akamzaa Azaria (ndiye huyo aliyefanya kazi ya ukuhani katika nyumba aliyoijenga Sulemani huko Yerusalemu)
Johanan was the father of Azariah, who served as priest in the temple that Solomon built in Jerusalem,
11
na Azaria akamzaa Amaria; na Amaria akamzaa Ahitubu;
Azariah was the father of Amariah, Amariah was the father of Ahitub,
12
na Ahitubu akamzaa Sadoki; na Sadoki akamzaa Meshulamu;
Ahitub was the father of Zadok, Zadok was the father of Shallum,
13
na Meshulamu akamzaa Hilkia; na Hilkia akamzaa Azaria;
Shallum was the father of Hilkiah, Hilkiah was the father of Azariah,
14
na Azaria akamzaa Seraya; na Seraya akamzaa Yehosadaki;
Azariah was the father of Seraiah, and Seraiah was the father of Jehozadak.
15
na Yehosadaki akachukuliwa mateka, hapo Bwana alipowachukua mateka Yuda na Yerusalemu, kwa mkono wa Nebukadreza.
Jehozadak went into captivity when the LORD sent Judah and Jerusalem into exile by the hand of Nebuchadnezzar.
16
Wana wa Lawi; Gershoni, na Kohathi, na Merari.
The sons of Levi: Gershom, Kohath, and Merari.
17
Na haya ndiyo majina ya wana wa Gershoni; Libni, na Shimei.
These are the names of the sons of Gershom: Libni and Shimei.
18
Na wana wa Kohathi walikuwa Amramu, na Ishari, na Hebroni, na Uzieli.
The sons of Kohath: Amram, Izhar, Hebron, and Uzziel.
19
Wana wa Merari; Mali, na Mushi. Na hizi ndizo jamaa za Walawi, sawasawa na mbari za baba zao.
The sons of Merari: Mahli and Mushi. These are the clans of the Levites listed according to their fathers:
20
Wa Gershoni; mwanawe huyo ni Libni, na mwanawe huyo ni Yahathi, na mwanawe huyo ni Zima;
Of Gershom: Libni his son, Jahath his son, Zimmah his son,
21
na mwanawe huyo ni Yoa, na mwanawe huyo ni Ido, na mwanawe huyo ni Zera, na mwanawe huyo ni Yeatherai.
Joah his son, Iddo his son, Zerah his son, and Jeatherai his son.
22
Wana wa Kohathi; mwanawe huyo ni Ishari, na mwanawe huyo ni Kora, na mwanawe huyo ni Asiri;
The descendants of Kohath: Amminadab his son, Korah his son, Assir his son,
23
na mwanawe huyo ni Elkana, na mwanawe huyo ni Ebiasafu, na mwanawe huyo ni Asiri;
Elkanah his son, Ebiasaph his son, Assir his son,
24
na mwanawe huyo ni Tahathi, na mwanawe huyo ni Urieli, na mwanawe huyo ni Uzia, na mwanawe huyo ni Shauli.
Tahath his son, Uriel his son, Uzziah his son, and Shaul his son.
25
Na wana wa Elkana; Amasai, na Ahimothi.
The descendants of Elkanah: Amasai, Ahimoth,
26
Kwa habari za Elkana; wana wa Elkana; mwanawe huyo ni Sufu, na mwanawe huyo ni Tohu;
Elkanah his son, Zophai his son, Nahath his son,
27
na mwanawe huyo ni Elihu, na mwanawe huyo ni Yerohamu, na mwanawe huyo ni Elkana.
Eliab his son, Jeroham his son, and Elkanah his son.
28
Na wana wa Samweli; Yoeli, mzaliwa wa kwanza, na wa pili Abia.
The sons of Samuel: Joel his firstborn and Abijah his second son.
29
Wana wa Merari; Mali, na mwanawe huyo ni Libni, na mwanawe huyo ni Shimei, na mwanawe huyo ni Uza;
The descendants of Merari: Mahli, Libni his son, Shimei his son, Uzzah his son,
30
na mwanawe huyo ni Shimea, na mwanawe huyo ni Hagla, na mwanawe huyo ni Asaya.
Shimea his son, Haggiah his son, and Asaiah his son.
31
Na hawa ndio watu aliowaweka Daudi juu ya kazi ya kuimba katika nyumba ya Bwana, sanduku lile lilipokwisha pata mahali pa kustarehe.
These are the men David put in charge of the music in the house of the LORD after the ark rested there.
32
Nao wakafanya kazi yao ya kuimba mbele ya maskani ya hema ya kukutania, hata Sulemani alipokuwa amejenga ile nyumba ya Bwana huko Yerusalemu; pia wakaisimamia huduma yao sawasawa na zamu zao.
They ministered with song before the tabernacle, the Tent of Meeting, until Solomon built the house of the LORD in Jerusalem. And they performed their duties according to the regulations given them.
33
Na hawa ndio waliofanya huduma pamoja na wana wao. Katika wana wa Wakohathi; Hemani mwimbaji, mwana wa Yoeli, mwana wa Samweli;
These are the men who served, together with their sons. From the Kohathites: Heman the singer, the son of Joel, the son of Samuel,
34
mwana wa Elkana, mwana wa Yerohamu, mwana wa Elihu, mwana wa Tohu;
the son of Elkanah, the son of Jeroham, the son of Eliel, the son of Toah,
35
mwana wa Sufu, mwana wa Elkana, mwana wa Mahathi, mwana wa Amasai;
the son of Zuph, the son of Elkanah, the son of Mahath, the son of Amasai,
36
mwana wa Elkana, mwana wa Shauli, mwana wa Uzia, mwana wa Urieli;
the son of Elkanah, the son of Joel, the son of Azariah, the son of Zephaniah,
37
mwana wa Tahathi, mwana wa Asiri, mwana wa Ebiasafu, mwana wa Kora;
the son of Tahath, the son of Assir, the son of Ebiasaph, the son of Korah,
38
mwana wa Ishari, mwana wa Kohathi, mwana wa Lawi, mwana wa Israeli.
the son of Izhar, the son of Kohath, the son of Levi, the son of Israel.
39
Na nduguye Asafu, aliyesimama upande wake wa kuume, huyo Asafu alikuwa mwana wa Berekia, mwana wa Shimea;
Heman’s kinsman was Asaph, who served at his right hand: Asaph the son of Berechiah, the son of Shimea,
40
mwana wa Mikaeli, mwana wa Baaseya, mwana wa Malkiya;
the son of Michael, the son of Baaseiah, the son of Malchijah,
41
mwana wa Yeatherai, mwana wa Zera, mwana wa Ido;
the son of Ethni, the son of Zerah, the son of Adaiah,
42
mwana wa Yoa, mwana wa Zima, mwana wa Shimei;
the son of Ethan, the son of Zimmah, the son of Shimei,
43
mwana wa Yahathi, mwana wa Gershoni, mwana wa Lawi.
the son of Jahath, the son of Gershom, the son of Levi.
44
Na upande wa kushoto ndugu zao, wana wa Merari; Ethani, mwana wa Kishi, mwana wa Abdi, mwana wa Maluki;
On the left were their kinsmen, the sons of Merari: Ethan the son of Kishi, the son of Abdi, the son of Malluch,
45
mwana wa Hashabia, mwana wa Amazia, mwana wa Hilkia;
the son of Hashabiah, the son of Amaziah, the son of Hilkiah,
46
mwana wa Amzi, mwana wa Bani, mwana wa Shemeri;
the son of Amzi, the son of Bani, the son of Shemer,
47
mwana wa Mali, mwana wa Mushi, mwana wa Merari, mwana wa Lawi.
the son of Mahli, the son of Mushi, the son of Merari, the son of Levi.
48
Na ndugu zao, Walawi, ndio waliowekwa ili kufanya huduma yote ya maskani ya nyumba ya Mungu.
Their fellow Levites were assigned to every kind of service of the tabernacle, the house of God.
49
Lakini Haruni na wanawe ndio waliokuwa wakitoa sadaka juu ya madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa, na juu ya madhabahu ya kufukizia uvumba, kwa ajili ya kazi yote ya Patakatifu pa Patakatifu, ili kufanya upatanisho kwa Israeli, sawasawa na yote aliyokuwa ameyaamuru Musa, mtumishi wa Mungu.
But Aaron and his sons did all the work of the Most Holy Place. They presented the offerings on the altar of burnt offering and on the altar of incense to make atonement for Israel, according to all that Moses the servant of God had commanded.
50
Na hawa ndio wana wa Haruni; mwanawe huyo ni Eleazari, na mwanawe huyo ni Finehasi, na mwanawe huyo ni Abishua;
These were the descendants of Aaron: Eleazar his son, Phinehas his son, Abishua his son,
51
na mwanawe huyo ni Buki, na mwanawe huyo ni Uzi, na mwanawe huyo ni Serahia;
Bukki his son, Uzzi his son, Zerahiah his son,
52
na mwanawe huyo ni Merayothi, na mwanawe huyo ni Amaria, na mwanawe huyo Ahitubu;
Meraioth his son, Amariah his son, Ahitub his son,
53
na mwanawe huyo ni Sadoki, na mwanawe huyo ni Ahimaasi.
Zadok his son, and Ahimaaz his son.
54
Basi haya ndiyo makao yao, sawasawa na marago yao mipakani mwao; wana wa Haruni, katika jamaa za Wakohathi; kwani walikuwa na kura ya kwanza;
Now these were the territories assigned to the descendants of Aaron from the Kohathite clan for their settlements, because the first lot fell to them:
55
wakapewa Hebroni, katika nchi ya Yuda, na vijiji vyake vilivyouzunguka;
They were given Hebron in the land of Judah and its surrounding pasturelands.
56
bali mashamba ya mji huo, na vijiji vyake, alipewa Kalebu, mwana wa Yefune.
But the fields and villages around the city were given to Caleb son of Jephunneh.
57
Na wana wa Haruni wakapewa miji ile ya kukimbilia, nayo ni Hebroni, tena Libna pamoja na viunga vyake, na Yatiri, na Eshtemoa pamoja na viunga vyake;
So the descendants of Aaron were given Hebron (a city of refuge), Libnah, Jattir, Eshtemoa,
58
na Holoni pamoja na viunga vyake, na Debiri pamoja na viunga vyake;
Hilen, Debir,
59
na Ashani pamoja na viunga vyake, na Beth-shemeshi pamoja na viunga vyake;
Ashan, Juttah, and Beth-shemesh, together with their pasturelands.
60
tena katika kabila ya Benyamini; Geba pamoja na viunga vyake, na Alemethi pamoja na viunga vyake, na Anathothi pamoja na viunga vyake. Miji yao yote katika jamaa zao ilikuwa miji kumi na mitatu.
And from the tribe of Benjamin they were given Gibeon, Geba, Alemeth, and Anathoth, together with their pasturelands. So they had thirteen cities in all among their families.
61
Nao waliobaki wa wana wa Kohathi walipewa kwa kura miji kumi, katika jamaa ya kabila hiyo, yaani, nusu-kabila, nusu ya Manase.
To the rest of the Kohathites, ten cities were allotted from the half-tribe of Manasseh.
62
Na wana wa Gershoni walipewa kwa kura miji kumi na mitatu, sawasawa na jamaa zao, katika kabila ya Isakari, na katika kabila ya Asheri, na katika kabila ya Naftali, na katika kabila ya Manase waliokaa Bashani.
The Gershomites, according to their clans, were allotted thirteen cities from the tribes of Issachar, Asher, Naphtali, and Manasseh in Bashan.
63
Na wana wa Merari walipewa kwa kura miji kumi na miwili, sawasawa na jamaa zao, katika kabila ya Reubeni, na katika kabila ya Gadi, na katika kabila ya Zabuloni.
The Merarites, according to their clans, were allotted twelve cities from the tribes of Reuben, Gad, and Zebulun.
64
Na wana wa Israeli waliwapa Walawi miji hiyo pamoja na viunga vyake.
So the Israelites gave to the Levites these cities and their pasturelands.
65
Tena wakawapa kwa kura miji hiyo iliyotajwa majina yake, katika kabila ya wana wa Yuda, na katika kabila ya wana wa Simeoni, na katika kabila ya wana wa Benyamini.
They assigned by lot the cities named above from the tribes of Judah, Simeon, and Benjamin.
66
Na jamaa nyingine za wana wa Kohathi walikuwa na miji ya mipakani mwao katika kabila ya Efraimu.
And some of the clans of the Kohathites were given cities from the tribe of Ephraim for their territory:
67
Basi wakapewa miji ya kukimbilia, yaani, Shekemu pamoja na viunga vyake katika nchi ya milima milima ya Efraimu; na Gezeri pamoja na viunga vyake;
They were given Shechem (a city of refuge) with its pasturelands in the hill country of Ephraim, and Gezer,
68
na Yokmeamu pamoja na viunga vyake, na Beth-horoni pamoja na viunga vyake;
Jokmeam, Beth-horon,
69
na Aiyaloni pamoja na viunga vyake, na Gath-rimoni pamoja na viunga vyake;
Aijalon, and Gath-rimmon, together with their pasturelands.
70
na katika nusu-kabila ya Manase; Taanaki pamoja na viunga vyake, na Ibleamu pamoja na viunga vyake; kwa mabaki ya jamaa ya wana wa Kohathi.
And from the half-tribe of Manasseh the rest of the clans of the Kohathites were given Aner and Bileam, together with their pasturelands.
71
Na wana wa Gershoni wakapewa, katika jamaa ya nusu-kabila ya Manase; Golani katika Bashani pamoja na viunga vyake, na Ashtarothi pamoja na viunga vyake;
The Gershomites received the following: From the clan of the half-tribe of Manasseh they were given Golan in Bashan and also Ashtaroth, together with their pasturelands.
72
na katika kabila ya Isakari; Kishioni pamoja na viunga vyake, na Daberathi pamoja na viunga vyake;
From the tribe of Issachar they were given Kedesh, Daberath,
73
na Remethi pamoja na viunga vyake, na En-gaminu pamoja na viunga vyake;
Ramoth, and Anem, together with their pasturelands.
74
na katika kabila ya Asheri; Mishali pamoja na viunga vyake, na Abdoni pamoja na viunga vyake;
From the tribe of Asher they were given Mashal, Abdon,
75
na Helkathi pamoja na viunga vyake, na Rehobu pamoja na viunga vyake;
Hukok, and Rehob, together with their pasturelands.
76
na katika kabila ya Naftali; Kedeshi katika Galilaya pamoja na viunga vyake, na Hamothi pamoja na viunga vyake, na Kiriathaimu pamoja na viunga vyake.
And from the tribe of Naphtali they were given Kedesh in Galilee, Hammon, and Kiriathaim, together with their pasturelands.
77
Nao mabaki ya Walawi, wana wa Merari, wakapewa, katika kabila ya Zabuloni; Rimona pamoja na viunga vyake, na Tabori pamoja na viunga vyake;
The Merarites (the rest of the Levites) received the following: From the tribe of Zebulun they were given Rimmono and Tabor, together with their pasturelands.
78
na ng'ambo ya mto wa Yordani huko Yeriko, upande wa mashariki wa Yordani, katika kabila ya Reubeni; Bezeri katika nyika pamoja na viunga vyake, na Yahasa pamoja na viunga vyake,
From the tribe of Reuben east of the Jordan opposite Jericho they were given Bezer in the wilderness, Jahzah,
79
na Kedemothi pamoja na viunga vyake, na Mefaathi pamoja na viunga vyake;
Kedemoth, and Mephaath, together with their pasturelands.
80
na katika kabila ya Gadi; Ramothi katika Gileadi pamoja na viunga vyake, na Mahanaimu pamoja na viunga vyake;
And from the tribe of Gad they were given Ramoth in Gilead, Mahanaim,
81
na Heshboni pamoja na viunga vyake, na Yazeri pamoja na viunga vyake.
Heshbon, and Jazer, together with their pasturelands.

Chagua Sura