1 Mambo ya Nyakati 23 Swahili & English

Listen/Download Audio
1 Mambo ya Nyakati 23 (Swahili) 1st Chronicles 23 (English)

Basi Daudi alikuwa mzee, ameshiba siku; akamtawaza mwanawe Sulemani awe mfalme juu ya Israeli. 1 Mambo ya Nyakati 23:1

Now David was old and full of days; and he made Solomon his son king over Israel.

Akawakusanya wakuu wote wa Israeli, pamoja na makuhani na Walawi. 1 Mambo ya Nyakati 23:2

He gathered together all the princes of Israel, with the priests and the Levites.

Nao wakahesabiwa Walawi wenye miaka thelathini na zaidi; na jumla yao kwa vichwa, mtu kwa mtu, ikapata thelathini na nane elfu. 1 Mambo ya Nyakati 23:3

The Levites were numbered from thirty years old and upward: and their number by their polls, man by man, was thirty-eight thousand.

Katika hao ishirini na nne elfu walikuwa wa kusimamia kazi ya nyumba ya Bwana; na sita elfu walikuwa maakida na makadhi; 1 Mambo ya Nyakati 23:4

Of these, twenty-four thousand were to oversee the work of the house of Yahweh; and six thousand were officers and judges;

na elfu nne walikuwa mabawabu; na elfu nne walimsifu Bwana kwa vinanda, nilivyovifanya, alisema Daudi, vya kumsifia. 1 Mambo ya Nyakati 23:5

and four thousand were doorkeepers; and four thousand praised Yahweh with the instruments which I made, [said David], for giving praise.

Basi Daudi akawagawanya kuwa zamu zao sawasawa na wana wa Lawi; Gershoni, Kohathi, na Merari. 1 Mambo ya Nyakati 23:6

David divided them into divisions according to the sons of Levi: Gershon, Kohath, and Merari.

Wa Wagershoni; Ladani, na Shimei. 1 Mambo ya Nyakati 23:7

Of the Gershonites: Ladan and Shimei.

Wana wa Ladani; Yehieli mkuu wao, na Zethamu, na Yoeli, watu watatu. 1 Mambo ya Nyakati 23:8

The sons of Ladan: Jehiel the chief, and Zetham, and Joel, three.

Wana wa Shimei; Shelomothi, na Hazieli, na Harani, watatu. Hao walikuwa vichwa vya mbari za baba za Ladani. 1 Mambo ya Nyakati 23:9

The sons of Shimei: Shelomoth, and Haziel, and Haran, three. These were the heads of the fathers' [houses] of Ladan.

Na wana wa Shimei; Yahathi, na Zina, na Yeushi, na Beria. Hao wanne walikuwa wana wa Shimei. 1 Mambo ya Nyakati 23:10

The sons of Shimei: Jahath, Zina, and Jeush, and Beriah. These four were the sons of Shimei.

Naye Yahathi alikuwa mkubwa wao, na Zina alikuwa wa pili; lakini Yeushi na Beria hawakuwa na wana wengi; basi wakawa mbari ya baba kwa kuhesabiwa pamoja. 1 Mambo ya Nyakati 23:11

Jahath was the chief, and Zizah the second: but Jeush and Beriah didn't have many sons; therefore they became a fathers' house in one reckoning.

Wana wa Kohathi; Amramu, Ishari, Hebroni, na Uzieli, watu wanne. 1 Mambo ya Nyakati 23:12

The sons of Kohath: Amram, Izhar, Hebron, and Uzziel, four.

Wana wa Amramu; Haruni na Musa; naye Haruni akatengwa, ili ayatakase yaliyo matakatifu sana, yeye na wanawe milele, ili kufukiza uvumba mbele za Bwana, kumtumikia, na kubariki kwa jina lake, milele. 1 Mambo ya Nyakati 23:13

The sons of Amram: Aaron and Moses; and Aaron was separated, that he should sanctify the most holy things, he and his sons, forever, to burn incense before Yahweh, to minister to him, and to bless in his name, forever.

Lakini kwa habari za Musa, mtu wa Mungu, wanawe hutajwa miongoni mwa kabila ya Lawi. 1 Mambo ya Nyakati 23:14

But as for Moses the man of God, his sons were named among the tribe of Levi.

Wana wa Musa; Gershomu na Eliezeri. 1 Mambo ya Nyakati 23:15

The sons of Moses: Gershom and Eliezer.

Wana wa Gershomu; Shebueli mkuu wao. 1 Mambo ya Nyakati 23:16

The sons of Gershom: Shebuel the chief.

Na wana wa Eliezeri; Rehabia mkuu wao. Yeye Eliezeri hakuwa na wana wengine; lakini wana wa Rehabia walikuwa wengi sana. 1 Mambo ya Nyakati 23:17

The sons of Eliezer were: Rehabiah the chief; and Eliezer had no other sons; but the sons of Rehabiah were very many.

Wana wa Ishari; Shelomithi mkuu wao. 1 Mambo ya Nyakati 23:18

The sons of Izhar: Shelomith the chief.

Wana wa Hebroni; Yeria mkuu wao, Amaria wa pili, Yahazieli wa tatu, na Yekameamu wa nne. 1 Mambo ya Nyakati 23:19

The sons of Hebron: Jeriah the chief, Amariah the second, Jahaziel the third, and Jekameam the fourth.

Wana wa Uzieli; Mika mkuu wao, na Ishia wa pili. 1 Mambo ya Nyakati 23:20

The sons of Uzziel: Micah the chief, and Isshiah the second.

Wana wa Merari; Mali na Mushi. Wana wa Mali; Eleazari, na Kishi. 1 Mambo ya Nyakati 23:21

The sons of Merari: Mahli and Mushi. The sons of Mahli: Eleazar and Kish.

Akafa Eleazari, wala hakuwa na wana, ila binti tu; na ndugu zao, wana wa Kishi, wakawaoa. 1 Mambo ya Nyakati 23:22

Eleazar died, and had no sons, but daughters only: and their brothers the sons of Kish took them [to wife].

Wana wa Mushi; Mali, na Ederi, na Yeremothi, watu watatu. 1 Mambo ya Nyakati 23:23

The sons of Mushi: Mahli, and Eder, and Jeremoth, three.

Hao walikuwa wana wa Lawi, kwa kufuata mbari za baba zao, yaani, vichwa vya mbari za baba zao waliohesabiwa, kwa hiyo hesabu ya majina yao kwa vichwa, hao walioifanya kazi ya utumishi wa nyumba ya Bwana, wenye miaka ishirini na zaidi. 1 Mambo ya Nyakati 23:24

These were the sons of Levi after their fathers' houses, even the heads of the fathers' [houses] of those of those who were counted, in the number of names by their polls, who did the work for the service of the house of Yahweh, from twenty years old and upward.

Kwa kuwa Daudi alisema, Bwana, Mungu wa Israeli, amewastarehesha watu wake; naye hukaa Yerusalemu milele; 1 Mambo ya Nyakati 23:25

For David said, Yahweh, the God of Israel, has given rest to his people; and he dwells in Jerusalem forever:

wala Walawi hawahitaji tena kuichukua maskani, na vyombo vyake vyote kwa utumishi wake. 1 Mambo ya Nyakati 23:26

and also the Levites shall no more have need to carry the tent and all the vessels of it for the service of it.

Maana kwa maneno ya mwisho ya Daudi, hao wana wa Lawi walihesabiwa, wenye miaka ishirini na zaidi. 1 Mambo ya Nyakati 23:27

For by the last words of David the sons of Levi were numbered, from twenty years old and upward.

Kwani kazi yao ilikuwa kuwangojea wana wa Haruni katika utumishi wa nyumba ya Bwana, nyuani, na vyumbani, na kwa kuvisafisha vitakatifu vyote, ndiyo kazi ya utumishi wa nyumba ya Mungu; 1 Mambo ya Nyakati 23:28

For their office was to wait on the sons of Aaron for the service of the house of Yahweh, in the courts, and in the chambers, and in the purifying of all holy things, even the work of the service of the house of God;

tena kazi ya mikate ya wonyesho, na ya unga mwembamba wa sadaka ya unga; ikiwa ni wa maandazi yasiyochachwa, au wa yale yaliyotokoswa, au wa yale yaliyookwa; na kazi ya kila namna ya kipimo na cheo; 1 Mambo ya Nyakati 23:29

for the show bread also, and for the fine flour for a meal-offering, whether of unleavened wafers, or of that which is baked in the pan, or of that which is soaked, and for all manner of measure and size;

nao wasimame kila asubuhi kumshukuru na kumsifu Bwana, na jioni vivyo hivyo; 1 Mambo ya Nyakati 23:30

and to stand every morning to thank and praise Yahweh, and likewise in the evening;

na kumtolea Bwana sadaka zote za kuteketezwa, katika siku za sabato, za mwezi mpya, na za sikukuu zilizoagizwa, kwa hesabu kadiri ya agizo lake, daima mbele za Bwana; 1 Mambo ya Nyakati 23:31

and to offer all burnt offerings to Yahweh, on the Sabbaths, on the new moons, and on the set feasts, in number according to the ordinance concerning them, continually before Yahweh;

tena walinde ulinzi wa hema ya kukutania, na ulinzi wa patakatifu, na ulinzi wa wana wa Haruni, ndugu zao, katika utumishi wa nyumba ya Bwana. 1 Mambo ya Nyakati 23:32

and that they should keep the charge of the tent of meeting, and the charge of the holy place, and the charge of the sons of Aaron their brothers, for the service of the house of Yahweh.