1
Na wana wa Isakari; Tola, na Puva, na Yashubu, na Shimroni, wanne.
The sons of Issachar: Tola, Puah, Jashub, and Shimron—four in all.
2
Na wana wa Tola; Uzi, na Refaya, na Yerieli, na Yamai, na Ibsamu, na Shemueli, wakuu wa mbari za baba zao, yaani, wa Tola; watu hodari wa vita katika vizazi vyao; hesabu yao katika siku za Daudi ilikuwa watu ishirini na mbili elfu na mia sita.
The sons of Tola: Uzzi, Rephaiah, Jeriel, Jahmai, Ibsam, and Shemuel, the heads of their families. In the days of David, 22,600 descendants of Tola were numbered in their genealogies as mighty men of valor.
3
Na wana wa Uzi; Izrahia; na wana wa Izrahia; Mikaeli, na Obadia, na Yoeli, na Ishia, watano; wote wakuu.
The son of Uzzi: Izrahiah. The sons of Izrahiah: Michael, Obadiah, Joel, and Isshiah. All five of them were chiefs.
4
Na pamoja nao, katika vizazi vyao, sawasawa na mbari za baba zao, walikuwapo vikosi vya jeshi la vita, watu thelathini na sita elfu; kwa kuwa wake zao na watoto wao walikuwa wengi.
In addition to them, according to their genealogy, they had 36,000 troops for battle, for they had many wives and children.
5
Na ndugu zao katika jamaa zote za Isakari, watu hodari wa vita, wakihesabiwa kwa vizazi vyao, walikuwa watu themanini na saba elfu.
Their kinsmen belonging to all the families of Issachar who were mighty men of valor totaled 87,000, as listed in their genealogies.
6
Wana wa Benyamini; Bela, na Bekeri, na Yediaeli, watatu.
The three sons of Benjamin: Bela, Becher, and Jediael.
7
Na wana wa Bela; Esboni, na Uzi, na Uzieli, na Yerimothi, na Iri, watano; wakuu wa mbari za baba zao, watu hodari wa vita; nao wakahesabiwa kwa vizazi vyao watu ishirini na mbili elfu na thelathini na wanne.
The sons of Bela: Ezbon, Uzzi, Uzziel, Jerimoth, and Iri, heads of their families—five in all. There were 22,034 mighty men of valor listed in their genealogies.
8
Na wana wa Bekeri; Zemira, na Yoashi, na Eliezeri, na Elioenai, na Omri, na Yeremothi, na Abiya, na Anathothi, na Alemethi. Hao wote ndio wana wa Bekeri.
The sons of Becher: Zemirah, Joash, Eliezer, Elioenai, Omri, Jeremoth, Abijah, Anathoth, and Alemeth; all these were Becher’s sons.
9
Nao wakahesabiwa kwa vizazi vyao, katika vizazi vyao, wakuu wa mbari za baba zao, watu hodari wa vita, jumla yao watu ishirini elfu na mia mbili.
Their genealogies were recorded according to the heads of their families—20,200 mighty men of valor.
10
Na wana wa Yediaeli; Bilhani; na wana wa Bilhani; Yeushi, na Benyamini, na Ehudi, na Kenaana, na Zethani, na Tarshishi, na Ahishahari.
The son of Jediael: Bilhan. The sons of Bilhan: Jeush, Benjamin, Ehud, Chenaanah, Zethan, Tarshish, and Ahishahar.
11
Hao wote ndio wana wa Yediaeli, sawasawa na wakuu wa mbari za baba zao, watu hodari wa vita, kumi na saba elfu na mia mbili, wawezao kwenda vitani katika jeshi.
All these sons of Jediael were heads of their families, mighty men of valor; there were 17,200 fit for battle.
12
Tena Shupimu, na Hupimu, wana wa Iri; na Hushimu, wana wa Aheri.
The Shuppites and Huppites were descendants of Ir, and the Hushites were descendants of Aher.
13
Wana wa Naftali; Yaseeli, na Guni, na Yeseri, na Shilemu; wana wa Bilha.
The sons of Naphtali: Jahziel, Guni, Jezer, and Shallum—the descendants of Bilhah.
14
Wana wa Manase; Asrieli, ambaye suria yake, Mwarami, alimzalia, akamzalia na Makiri babaye Gileadi;
The descendants of Manasseh: Asriel through his Aramean concubine. She also gave birth to Machir the father of Gilead.
15
naye Makiri akatwaa mke kwa Hupimu na Shupimu, ambao umbu lao aliitwa Maaka; na wa pili akaitwa jina lake Selofehadi; na Selofehadi alikuwa na binti.
Machir took a wife from among the Huppites and Shuppites. The name of his sister was Maacah. Another descendant was named Zelophehad, who had only daughters.
16
Na Maaka mkewe Makiri, akamzalia mwana, akamwita jina lake Pereshi; na jina la nduguye aliitwa Shereshi; na wanawe walikuwa Ulamu, na Rakemu.
Machir’s wife Maacah gave birth to a son, and she named him Peresh. His brother was named Sheresh, and his sons were Ulam and Rekem.
17
Na wana wa Ulamu; Bedani. Hao ndio wana wa Gileadi, mwana wa Makiri, mwana wa Manase.
The son of Ulam: Bedan. These were the sons of Gilead son of Machir, the son of Manasseh.
18
Na umbu lake, Hamolekethi, akamzaa Ish-hodu, na Abiezeri, na Mala.
His sister Hammolecheth gave birth to Ishhod, Abiezer, and Mahlah.
19
Na wana wa Shemida walikuwa Ahiani, na Shekemu, na Liki, na Aniamu.
And these were the sons of Shemida: Ahian, Shechem, Likhi, and Aniam.
20
Na wana wa Efraimu; Shuthela, na mwanawe huyo ni Beredi, na mwanawe huyo ni Tahathi, na mwanawe huyo ni Ekada, na mwanawe huyo ni Tahathi;
The descendants of Ephraim: Shuthelah, Bered his son, Tahath his son, Eleadah his son, Tahath his son,
21
na mwanawe huyo ni Zabadi, na mwanawe huyo ni Shuthela; na Ezeri na Ekadi, ambao watu wa Gathi, wenyeji wa nchi, waliwaua, kwa sababu walishuka ili kuzipokonya ng'ombe zao.
Zabad his son, and Shuthelah his son. Ezer and Elead were killed by the natives of Gath, because they went down to steal their livestock.
22
Na Efraimu, baba yao, akaomboleza siku nyingi, wakaja nduguze ili kumfariji.
Their father Ephraim mourned for many days, and his relatives came to comfort him.
23
Naye akamwingilia mkewe, naye akachukua mimba na kuzaa mwana, akamwita jina lake Beria, kwa sababu mna mabaya nyumbani mwake.
And again he slept with his wife, and she conceived and gave birth to a son. So he named him Beriah, because tragedy had come upon his house.
24
Na binti yake alikuwa Sheera, ambaye alijenga Beth-horoni, wa chini na wa juu, na Uzen-sheera.
His daughter was Sheerah, who built Lower and Upper Beth-horon, as well as Uzzen-sheerah.
25
Mwanawe ni Refa, na Reshefu, na mwanawe huyo ni Tela, na mwanawe huyo ni Tahani;
Additionally, Rephah was his son, Resheph his son, Telah his son, Tahan his son,
26
na mwanawe huyo ni Ladani, na mwanawe huyo ni Amihudi, na mwanawe huyo ni Elishama;
Ladan his son, Ammihud his son, Elishama his son,
27
na mwanawe huyo ni Nuni, na mwanawe huyo ni Yoshua.
Nun his son, and Joshua his son.
28
Na hizi ndizo hozi zao na makao yao; Betheli na vijiji vyake, na upande wa mashariki Naara, na upande wa magharibi Gezeri na vijiji vyake; na Shekemu pia na vijiji vyake, hata Aza na vijiji vyake;
Their holdings and settlements included Bethel and its villages, Naaran to the east, Gezer and its villages to the west, and Shechem and its villages as far as Ayyah and its villages.
29
na mipakani mwa wana wa Manase; Beth-sheani na vijiji vyake; na Taanaki na vijiji vyake; na Megido na vijiji vyake; na Dori na vijiji vyake. Katika miji hiyo walikaa wana wa Yusufu, mwana wa Israeli.
And along the borders of Manasseh were Beth-shean, Taanach, Megiddo, and Dor, together with their villages. The descendants of Joseph son of Israel lived in these towns.
30
Wana wa Asheri; Imna, na Ishva, na Ishvi, na Beria, na umbu lao, Sera.
The children of Asher: Imnah, Ishvah, Ishvi, Beriah, and their sister Serah.
31
Na wana wa Beria; Heberi, na Malkieli, aliyekuwa babaye Birzaithi.
The sons of Beriah: Heber, as well as Malchiel, who was the father of Birzaith.
32
Na Heberi akamzaa Yafleti, na Shomeri, na Hothamu, na umbu lao, Shua.
Heber was the father of Japhlet, Shomer, and Hotham, and of their sister Shua.
33
Na wana wa Yafleti; Pasaki, na Bimhali, na Ashvathi. Hao ndio wana wa Yafleti.
The sons of Japhlet: Pasach, Bimhal, and Ashvath. These were Japhlet’s sons.
34
Na wana wa Shomeri; Ahi, na Roga, na Yehuba, na Aramu.
The sons of Shemer: Ahi, Rohgah, Hubbah, and Aram.
35
Na wana wa nduguye Helemu; Sofa, na Imna, na Sheleshi, na Amali.
The sons of his brother Helem: Zophah, Imna, Shelesh, and Amal.
36
Wana wa Sofa; Sua, na Harneferi, na Shuali, na Beri, na Imra;
The sons of Zophah: Suah, Harnepher, Shual, Beri, Imrah,
37
na Bezeri, na Hodu, na Shama, na Shilsha, na Ithrani, na Beera.
Bezer, Hod, Shamma, Shilshah, Ithran, and Beera.
38
Na wana wa Yetheri; Yefune, na Pispa, na Ara.
The sons of Jether: Jephunneh, Pispa, and Ara.
39
Na wana wa Ula; Ara, na Hanieli na Risia.
The sons of Ulla: Arah, Hanniel, and Rizia.
40
Hao wote ndio wana wa Asheri, wakuu wa mbari za baba zao, watu wateule, hodari wa vita, wakuu wa mashehe. Na hesabu yao waliojumlishwa kwa vizazi vyao kwenda vitani walikuwa watu ishirini na sita elfu.</p>
All these were the descendants of Asher—heads of their families, choice and mighty men of valor, and chiefs among the leaders. The number of men fit for battle, recorded in their genealogies, was 26,000.