Na zamu za wana wa Haruni ni hizi. Wana wa Haruni; Nadabu, na Abihu, na Eleazari, na Ithamari.
Thes were the divisions of the sons of Aaron. The sons of Aaron: Nadab and Abihu, Eleazar and Ithamar.
Lakini hao Nadabu na Abihu walikufa kabla ya baba yao, wala hawakuwa na watoto; kwa hiyo Eleazari na Ithamari wakafanya ukuhani.
But Nadab and Abihu died before their father, and had no children: therefore Eleazar and Ithamar executed the priest's office.
Akawagawanya Daudi, na Sadoki wa wana wa Eleazari, na Ahimeleki wa wana wa Ithamari, katika utumishi kwa kadiri ya usimamizi wao.
David with Zadok of the sons of Eleazar, and Ahimelech of the sons of Ithamar, divided them according to their ordering in their service.
Wakaonekana wakuu wengi wa wana wa Eleazari kuliko wa wana wa Ithamari; wakagawanyika hivi; wa wana wa Eleazari kulikuwa na kumi na sita, waliokuwa wakuu wa mbari za baba zao; na wa wana wa Ithamari, sawasawa na mbari za baba zao, wanane.
There were more chief men found of the sons of Eleazar than of the sons of Ithamar; and [thus] were they divided: of the sons of Eleazar there were sixteen, heads of fathers' houses; and of the sons of Ithamar, according to their fathers' houses, eight.
Ndivyo walivyogawanyika kwa kura, wao kwa wao; kwani kulikuwa na wakuu wa patakatifu, na wakuu wa Mungu, wa wana wa Eleazari, na wa wana wa Ithamari pia.
Thus were they divided impartially by drawing lots; for there were princes of the sanctuary, and princes of God, both of the sons of Eleazar, and of the sons of Ithamar.
Naye Shemaya, mwana wa Nethaneli, mwandishi, aliyekuwa wa Walawi, akawaandika mbele ya mfalme, na mbele ya wakuu, na Sadoki kuhani, na Ahimeleki, mwana wa Abiathari, na wakuu wa mbari za baba za makuhani, na za Walawi; ikatwaliwa ya Eleazari mbari moja ya baba, na moja ikatwaliwa ya Ithamari.
Shemaiah the son of Nethanel the scribe, who was of the Levites, wrote them in the presence of the king, and the princes, and Zadok the priest, and Ahimelech the son of Abiathar, and the heads of the fathers' [houses] of the priests and of the Levites; one fathers' house being taken for Eleazar, and one taken for Ithamar.
Kura ya kwanza ikamtokea Yehoiaribu, na ya pili Yedaya;
Now the first lot came forth to Jehoiarib, the second to Jedaiah,
ya tatu Harimu, ya nne Seorimu;
the third to Harim, the fourth to Seorim,
ya tano Malkia, ya sita Miyamini;
the fifth to Malchijah, the sixth to Mijamin,
ya saba Hakosi, ya nane Abia;
the seventh to Hakkoz, the eighth to Abijah,
ya kenda Yeshua, ya kumi Shekania;
the ninth to Jeshua, the tenth to Shecaniah,
ya kumi na moja Eliashibu, ya kumi na mbili Yakimu;
the eleventh to Eliashib, the twelfth to Jakim,
ya kumi na tatu Hupa, ya kumi na nne Yeshebeabu;
the thirteenth to Huppah, the fourteenth to Jeshebeab,
ya kumi na tano Bilga, ya kumi na sita Imeri;
the fifteenth to Bilgah, the sixteenth to Immer,
ya kumi na saba Heziri, ya kumi na nane Hapisesi;
the seventeenth to Hezir, the eighteenth to Happizzez,
ya kumi na kenda Pethahia, ya ishirini Ezekieli;
the nineteenth to Pethahiah, the twentieth to Jehezkel,
ya ishirini na moja Yakini, ya ishirini na mbili Gamuli;
the twenty-first to Jachin, the twenty-second to Gamul,
ya ishirini na tatu Delaya, ya ishirini na nne Maazia.
the twenty-third to Delaiah, the twenty-fourth to Maaziah.
Huu ndio usimamizi wao katika huduma yao, waingie nyumbani mwa Bwana kwa kadiri ya agizo lao, kwa mkono wa Haruni baba yao, kama Bwana, Mungu wa Israeli, alivyomwamuru.
This was the ordering of them in their service, to come into the house of Yahweh according to the ordinance [given] to them by Aaron their father, as Yahweh, the God of Israel, had commanded him.
Na wa wana wa Lawi, waliosalia; wa wana wa Amramu, Shebueli; wa wana wa Shebueli, Yedeya.
Of the rest of the sons of Levi: of the sons of Amram, Shubael; of the sons of Shubael, Jehdeiah.
Wa Rehabia; wa wana wa Rehabia, Ishia mkuu wao.
Of Rehabiah: of the sons of Rehabiah, Isshiah the chief.
Wa Waishari, Shelomothi; wa wana wa Shelomothi, Yahathi.
Of the Izharites, Shelomoth; of the sons of Shelomoth, Jahath.
Na wana wa Hebroni; Yeria mkuu wao, Amaria wa pili, Yahazieli wa tatu, Yekameamu wa nne.
The sons [of Hebron]: Jeriah [the chief], Amariah the second, Jahaziel the third, Jekameam the fourth.
Wana wa Uzieli, Mika; wa wana wa Mika, Shamiri.
The sons of Uzziel, Micah; of the sons of Micah, Shamir.
Nduguye Mika, Ishia; wa wana wa Ishia, Zekaria.
The brother of Micah, Isshiah; of the sons of Isshiah, Zechariah.
Wana wa Merari; Mali na Mushi; wana wa Yaazia; Beno.
The sons of Merari: Mahli and Mushi; the sons of Jaaziah: Beno.
Wana wa Merari; wa Yaazia; Beno, na Shohamu, na Zakuri, na Ibri.
The sons of Merari: of Jaaziah, Beno, and Shoham, and Zaccur, and Ibri.
Wa Mali; Eleazari, asiyekuwa na wana.
Of Mahli: Eleazar, who had no sons.
Wa Kishi; wana wa Kishi; Yerameeli.
Of Kish; the sons of Kish: Jerahmeel.
Na wana wa Mushi; Mali, na Ederi, na Yeremothi. Hao ndio wana wa Walawi, kwa kufuata mbari za baba zao.
The sons of Mushi: Mahli, and Eder, and Jerimoth. These were the sons of the Levites after their fathers' houses.
Hao nao wakatupiwa kura vile vile, kama ndugu zao wana wa Haruni, machoni pa Daudi mfalme, na Sadoki, na Ahimeleki, na wakuu wa mbari za baba za makuhani na za Walawi; mbari za baba za mkuu, vile vile kama za nduguye mdogo.
These likewise cast lots even as their brothers the sons of Aaron in the presence of David the king, and Zadok, and Ahimelech, and the heads of the fathers' [houses] of the priests and of the Levites; the fathers' [houses] of the chief even as those of his younger brother.