1
Na zamu za wana wa Haruni ni hizi. Wana wa Haruni; Nadabu, na Abihu, na Eleazari, na Ithamari.
These were the divisions of the descendants of Aaron. The sons of Aaron were Nadab, Abihu, Eleazar, and Ithamar.
2
Lakini hao Nadabu na Abihu walikufa kabla ya baba yao, wala hawakuwa na watoto; kwa hiyo Eleazari na Ithamari wakafanya ukuhani.
But Nadab and Abihu died before their father did, and they had no sons; so Eleazar and Ithamar served as priests.
3
Akawagawanya Daudi, na Sadoki wa wana wa Eleazari, na Ahimeleki wa wana wa Ithamari, katika utumishi kwa kadiri ya usimamizi wao.
With the help of Eleazar’s descendant Zadok and Ithamar’s descendant Ahimelech, David divided them according to the offices of their service.
4
Wakaonekana wakuu wengi wa wana wa Eleazari kuliko wa wana wa Ithamari; wakagawanyika hivi; wa wana wa Eleazari kulikuwa na kumi na sita, waliokuwa wakuu wa mbari za baba zao; na wa wana wa Ithamari, sawasawa na mbari za baba zao, wanane.
Since more leaders were found among Eleazar’s descendants than those of Ithamar, they were divided accordingly. There were sixteen heads of families from the descendants of Eleazar and eight from the descendants of Ithamar.
5
Ndivyo walivyogawanyika kwa kura, wao kwa wao; kwani kulikuwa na wakuu wa patakatifu, na wakuu wa Mungu, wa wana wa Eleazari, na wa wana wa Ithamari pia.
Thus they were divided by lot, for there were officers of the sanctuary and officers of God among both Eleazar’s and Ithamar’s descendants.
6
Naye Shemaya, mwana wa Nethaneli, mwandishi, aliyekuwa wa Walawi, akawaandika mbele ya mfalme, na mbele ya wakuu, na Sadoki kuhani, na Ahimeleki, mwana wa Abiathari, na wakuu wa mbari za baba za makuhani, na za Walawi; ikatwaliwa ya Eleazari mbari moja ya baba, na moja ikatwaliwa ya Ithamari.
The scribe, Shemaiah son of Nethanel, a Levite, recorded their names in the presence of the king and of the officers: Zadok the priest, Ahimelech son of Abiathar, and the heads of families of the priests and the Levites—one family being taken from Eleazar, and then one from Ithamar.
7
Kura ya kwanza ikamtokea Yehoiaribu, na ya pili Yedaya;
The first lot fell to Jehoiarib, the second to Jedaiah,
8
ya tatu Harimu, ya nne Seorimu;
the third to Harim, the fourth to Seorim,
9
ya tano Malkia, ya sita Miyamini;
the fifth to Malchijah, the sixth to Mijamin,
10
ya saba Hakosi, ya nane Abia;
the seventh to Hakkoz, the eighth to Abijah,
11
ya kenda Yeshua, ya kumi Shekania;
the ninth to Jeshua, the tenth to Shecaniah,
12
ya kumi na moja Eliashibu, ya kumi na mbili Yakimu;
the eleventh to Eliashib, the twelfth to Jakim,
13
ya kumi na tatu Hupa, ya kumi na nne Yeshebeabu;
the thirteenth to Huppah, the fourteenth to Jeshebeab,
14
ya kumi na tano Bilga, ya kumi na sita Imeri;
the fifteenth to Bilgah, the sixteenth to Immer,
15
ya kumi na saba Heziri, ya kumi na nane Hapisesi;
the seventeenth to Hezir, the eighteenth to Happizzez,
16
ya kumi na kenda Pethahia, ya ishirini Ezekieli;
the nineteenth to Pethahiah, the twentieth to Jehezkel,
17
ya ishirini na moja Yakini, ya ishirini na mbili Gamuli;
the twenty-first to Jachin, the twenty-second to Gamul,
18
ya ishirini na tatu Delaya, ya ishirini na nne Maazia.
the twenty-third to Delaiah, and the twenty-fourth to Maaziah.
19
Huu ndio usimamizi wao katika huduma yao, waingie nyumbani mwa Bwana kwa kadiri ya agizo lao, kwa mkono wa Haruni baba yao, kama Bwana, Mungu wa Israeli, alivyomwamuru.
This was their appointed order for service when they entered the house of the LORD, according to the regulations prescribed for them by their forefather Aaron, as the LORD, the God of Israel, had commanded him.
20
Na wa wana wa Lawi, waliosalia; wa wana wa Amramu, Shebueli; wa wana wa Shebueli, Yedeya.
Now these were the rest of the descendants of Levi: From the sons of Amram: Shubael; from the sons of Shubael: Jehdeiah.
21
Wa Rehabia; wa wana wa Rehabia, Ishia mkuu wao.
As for Rehabiah, from his sons: The first was Isshiah.
22
Wa Waishari, Shelomothi; wa wana wa Shelomothi, Yahathi.
From the Izharites: Shelomoth; from the sons of Shelomoth: Jahath.
23
Na wana wa Hebroni; Yeria mkuu wao, Amaria wa pili, Yahazieli wa tatu, Yekameamu wa nne.
From the sons of Hebron: Jeriah was the first, Amariah the second, Jahaziel the third, and Jekameam the fourth.
24
Wana wa Uzieli, Mika; wa wana wa Mika, Shamiri.
From the sons of Uzziel: Micah; from the sons of Micah: Shamir.
25
Nduguye Mika, Ishia; wa wana wa Ishia, Zekaria.
The brother of Micah: Isshiah; from the sons of Isshiah: Zechariah.
26
Wana wa Merari; Mali na Mushi; wana wa Yaazia; Beno.
The sons of Merari: Mahli and Mushi. The son of Jaaziah: Beno.
27
Wana wa Merari; wa Yaazia; Beno, na Shohamu, na Zakuri, na Ibri.
The descendants of Merari from Jaaziah: Beno, Shoham, Zaccur, and Ibri.
28
Wa Mali; Eleazari, asiyekuwa na wana.
From Mahli: Eleazar, who had no sons.
29
Wa Kishi; wana wa Kishi; Yerameeli.
From Kish: Jerahmeel the son of Kish.
30
Na wana wa Mushi; Mali, na Ederi, na Yeremothi. Hao ndio wana wa Walawi, kwa kufuata mbari za baba zao.
And the sons of Mushi: Mahli, Eder, and Jerimoth. These were the sons of the Levites, according to their families.
31
Hao nao wakatupiwa kura vile vile, kama ndugu zao wana wa Haruni, machoni pa Daudi mfalme, na Sadoki, na Ahimeleki, na wakuu wa mbari za baba za makuhani na za Walawi; mbari za baba za mkuu, vile vile kama za nduguye mdogo.
As their brothers the descendants of Aaron did, they also cast lots in the presence of King David and of Zadok, Ahimelech, and the heads of the families of the priests and Levites—the family heads and their younger brothers alike.