Mwanzo 10 Swahili & English
Listen/Download AudioMwanzo 10 (Swahili) | Genesis 10 (English) |
---|---|
Hivi ndivyo vizazi vya wana wa Nuhu, Shemu, na Hamu, na Yafethi. Na kwao walizaliwa wana wa kiume baada ya gharika. Mwanzo 10:1 |
Now this is the history of the generations of the sons of Noah and of Shem, Ham, and Japheth. Sons were born to them after the flood. |
Wana wa Yafethi ni Gomeri, na Magogu, na Madai, na Yavani, na Tubali, na Mesheki, na Tirasi. Mwanzo 10:2 |
The sons of Japheth: Gomer, Magog, Madai, Javan, Tubal, Meshech, and Tiras. |
Na wana wa Gomeri ni Ashkenazi, na Rifathi, na Togama. Mwanzo 10:3 |
The sons of Gomer: Ashkenaz, Riphath, and Togarmah. |
Na wana wa Yavani ni Elisha, Tarshishi, Kitimu, na Warodani. Mwanzo 10:4 |
The sons of Javan: Elishah, Tarshish, Kittim, and Dodanim. |
Kwa hao nchi za pwani za mataifa ziligawanyikana kuwa nchi zao, kila moja kwa lugha yake, kwa jamaa zao, kufuata mataifa yao. Mwanzo 10:5 |
Of these were the isles of the nations divided in their lands, everyone after his language, after their families, in their nations. |
Na wana wa Hamu ni Kushi, na Misri, na Putu, na Kanaani. Mwanzo 10:6 |
The sons of Ham: Cush, Mizraim, Put, and Canaan. |
Na wana wa Kushi ni Seba, na Havila, na Sabta, na Raama, na Sabteka. Na wana wa Raama ni Sheba, na Dedani. Mwanzo 10:7 |
The sons of Cush: Seba, Havilah, Sabtah, Raamah, and Sabteca. The sons of Raamah: Sheba and Dedan. |
Kushi akamzaa Nimrodi, akaanza kuwa mtu hodari katika nchi. Mwanzo 10:8 |
Cush became the father of Nimrod: he began to be a mighty one in the earth. |
Alikuwa hodari kuwinda wanyama mbele za Bwana. Kwa hiyo watu hunena, Kama Nimrodi, hodari wa kuwinda wanyama mbele za Bwana. Mwanzo 10:9 |
He was a mighty hunter before Yahweh. Therefore it is said, "Like Nimrod, a mighty hunter before Yahweh." |
Mwanzo wa ufalme wake ulikuwa Babeli na Ereku, na Akadi, na Kalne, katika nchi ya Shinari. Mwanzo 10:10 |
The beginning of his kingdom was Babel, Erech, Accad, and Calneh, in the land of Shinar. |
Akatoka katika nchi ile akaenda mpaka Ashuru, akajenga Ninawi, na Rehoboth-iri, na Kala; Mwanzo 10:11 |
Out of that land he went forth into Assyria, and built Nineveh, Rehoboth Ir, Calah, |
na Reseni, kati ya Ninawi na Kala, nao ni mji mkubwa. Mwanzo 10:12 |
and Resen between Nineveh and Calah (the same is the great city). |
Misri akazaa Waludi, na Waanami, na Walehabi, na Wanaftuhi, Mwanzo 10:13 |
Mizraim became the father of Ludim, Anamim, Lehabim, Naphtuhim, |
na Wapathrusi, na Wakasluhi; huko ndiko walikotoka Wafilisti na Wakaftori. Mwanzo 10:14 |
Pathrusim, Casluhim (which the Philistines descended from), and Caphtorim. |
Kanaani akamzaa Sidoni, mwanawe wa kwanza, na Hethi, Mwanzo 10:15 |
Canaan became the father of Sidon (his firstborn), Heth, |
na Myebusi, na Mwamori, na Mgirgashi, Mwanzo 10:16 |
the Jebusite, the Amorite, the Girgashite, |
na Mhivi, na Mwarki, na Msini, Mwanzo 10:17 |
the Hivite, the Arkite, the Sinite, |
na Mwarvadi, na Msemari, na Mhamathi. Baadaye jamaa za Wakanaani walitawanyikana. Mwanzo 10:18 |
the Arvadite, the Zemarite, and the Hamathite. Afterward the families of the Canaanites were spread abroad. |
Na mpaka wa Wakanaani ulianza kutoka Sidoni kwa njia ya Gerari hata Gaza; tena kwa njia ya Sodoma, na Gomora, na Adma, na Seboimu, hata Lasha. Mwanzo 10:19 |
The border of the Canaanites was from Sidon, as you go toward Gerar, to Gaza; as you go toward Sodom, Gomorrah, Admah, and Zeboiim, to Lasha. |
Hao ndio wana wa Hamu, kufuata jamaa zao, kwa lugha zao, katika nchi zao, kufuata mataifa yao. Mwanzo 10:20 |
These are the sons of Ham, after their families, after their languages, in their lands, in their nations. |
Naye Shemu ambaye ni baba wa wana wote wa Eberi, na ndugu mkubwa wa Yafethi, akazaliwa wana. Mwanzo 10:21 |
To Shem, the father of all the children of Eber, the elder brother of Japheth, to him also were children born. |
Wana wa Shemu ni Elamu, na Ashuru, na Arfaksadi, na Ludi, na Aramu. Mwanzo 10:22 |
The sons of Shem: Elam, Asshur, Arpachshad, Lud, and Aram. |
Na wana wa Aramu ni Usi, na Huli, na Getheri, na Mashi. Mwanzo 10:23 |
The sons of Aram: Uz, Hul, Gether, and Mash. |
Arfaksadi akamzaa Sela, Sela akamzaa Eberi. Mwanzo 10:24 |
Arpachshad became the father of Shelah. Shelah became the father of Eber. |
Eberi akazaliwa wana wawili wa kiume; jina la wa kwanza ni Pelegi maana katika siku zake nchi iligawanyika; na jina la nduguye ni Yoktani. Mwanzo 10:25 |
To Eber were born two sons. The name of the one was Peleg, for in his days was the earth divided. His brother's name was Joktan. |
Yoktani akamzaa Almodadi, na Shelefu, na Hasarmawethi, na Yera, Mwanzo 10:26 |
Joktan became the father of Almodad, Sheleph, Hazarmaveth, Jerah, |
na Hadoramu, na Uzali, na Dikla, Mwanzo 10:27 |
Hadoram, Uzal, Diklah, |
na Obali, na Abimaeli, na Seba, Mwanzo 10:28 |
Obal, Abimael, Sheba, |
na Ofiri, na Havila, na Yobabi. Hao wote ndio wana wa Yoktani. Mwanzo 10:29 |
Ophir, Havilah, and Jobab. All these were the sons of Joktan. |
Makao yao yalikuwa kutoka Mesha kwa njia ya Sefari, mlima wa mashariki. Mwanzo 10:30 |
Their dwelling was from Mesha, as you go toward Sephar, the mountain of the east. |
Hao ndio wana wa Shemu, kufuata jamaa zao, na lugha zao, katika nchi zao, kufuata mataifa yao. Mwanzo 10:31 |
These are the sons of Shem, after their families, after their languages, in their lands, after their nations. |
Hizo ndizo jamaa za wana wa Nuhu, kufuata vizazi vyao, katika mataifa yao; na kwa hao mataifa yaligawanyika katika nchi baada ya gharika. Mwanzo 10:32 |
These are the families of the sons of Noah, after their generations, in their nations. Of these were the nations divided in the earth after the flood. |