Mwanzo 50 Swahili & English

Listen/Download Audio
Mwanzo 50 (Swahili) Genesis 50 (English)

Yusufu akamwangukia babaye usoni, akamlilila, akambusu. Mwanzo 50:1

Joseph fell on his father's face, wept on him, and kissed him.

Yusufu akawaagiza watumishi wake waganga, kwamba wampake baba yake dawa asioze. Waganga wakampaka dawa Israeli. Mwanzo 50:2

Joseph commanded his servants, the physicians, to embalm his father; and the physicians embalmed Israel.

Siku zake arobaini zikaisha, maana hivyo hutimizwa siku za kupaka dawa. Wamisri wakamlilia siku sabini. Mwanzo 50:3

Forty days were fulfilled for him, for that is how many the days it takes to embalm. The Egyptians wept for him for seventy days.

Siku za kumlilia zilipopita, Yusufu alisema na watu wa nyumba ya Farao, akinena, Kama nimeona neema machoni penu, tafadhalini mkaseme masikioni mwa Farao, mkinena, Baba yangu aliniapisha, akisema, Mwanzo 50:4

When the days of weeping for him were past, Joseph spoke to the house of Pharaoh, saying, "If now I have found favor in your eyes, please speak in the ears of Pharaoh, saying,

Mimi ni katika kufa, unizike katika kaburi langu nililojichimbia katika nchi ya Kanaani. Basi tafadhali uniruhusu niende sasa nikamzike babangu, nami nitarudi. Mwanzo 50:5

'My father made me swear, saying, "Behold, I am dying. Bury me in my grave which I have dug for myself in the land of Canaan." Now therefore, please let me go up and bury my father, and I will come again.'"

Farao akasema, Uende, ukamzike baba yako, kama alivyokuapisha. Mwanzo 50:6

Pharaoh said, "Go up, and bury your father, just like he made you swear."

Basi Yusufu akaenda amzike babaye, na watumwa wote wa Farao wakaenda pamoja naye, wazee wa nyumbani mwake, na wazee wote wa nchi ya Misri. Mwanzo 50:7

Joseph went up to bury his father; and with him went up all the servants of Pharaoh, the elders of his house, all the elders of the land of Egypt,

Na nyumba yote ya Yusufu, na nduguze, na nyumba ya babaye; wakawaacha watoto wao tu, na kondoo zao, na ng'ombe zao, katika nchi ya Gosheni. Mwanzo 50:8

all the house of Joseph, his brothers, and his father's house. Only their little ones, their flocks, and their herds, they left in the land of Goshen.

Kisha wakaenda pamoja naye wapanda farasi, na magari; wakawa jeshi kubwa sana. Mwanzo 50:9

There went up with him both chariots and horsemen. It was a very great company.

Wakaja mpaka sakafu ya Atadi, iliyo ng'ambo ya Yordani. Wakaomboleza huko maombolezo makuu, mazito sana. Akafanya matanga ya babaye siku saba. Mwanzo 50:10

They came to the threshing floor of Atad, which is beyond the Jordan, and there they lamented with a very great and sore lamentation. He mourned for his father seven days.

Nao waliokaa katika nchi, wale Wakanaani, walipoyaona matanga katika sakafu ya Atadi, wakasema, Matanga haya ya Wamisri ni makuu kwa hiyo mahali pale paliitwa Abel-Misri, iliyo ng'ambo ya Yordani. Mwanzo 50:11

When the inhabitants of the land, the Canaanites, saw the mourning in the floor of Atad, they said, "This is a grievous mourning by the Egyptians." Therefore, the name of it was called Abel Mizraim, which is beyond the Jordan.

Wanawe wakamfanyia kama alivyo waagiza; Mwanzo 50:12

His sons did to him just as he commanded them,

kwa kuwa wanawe wakamchukuwa mpaka nchi ya Kanaani, nao wakamzika katika pango ya shamba la Makpela, iliyo mbele ya Mamre, aliyoinunua Ibrahimu pamoja na shamba kwa Efroni Mhiti, pawe milki yake pa kuzikia. Mwanzo 50:13

for his sons carried him into the land of Canaan, and buried him in the cave of the field of Machpelah, which Abraham bought with the field, for a possession of a burying-place, from Ephron the Hittite, before Mamre.

Yusufu akarudi Misri, yeye na ndugu zake, na wote waliyokwenda pamoja naye kumzika babaye, baada ya kumzika babaye. Mwanzo 50:14

Joseph returned into Egypt--he, and his brothers, and all that went up with him to bury his father, after he had buried his father.

Ndugu zake Yusufu walipoona ya kwamba baba yao amekufa, walisema, Labda Yusufu atatuchukia; naye atatulipa maovu yetu tuliyomtenda. Mwanzo 50:15

When Joseph's brothers saw that their father was dead, they said, "It may be that Joseph will hate us, and will fully pay us back for all of the evil which we did to him.

Wakapeleka watu kwa Yusufu, kunena, Baba yako alitoa amri kabla ya kufa kwake, akasema, Mwanzo 50:16

They sent a message to Joseph, saying, "Your father commanded before he died, saying,

Mwambieni Yusufu hivi, Naomba uwaachilie ndugu zako kosa lao na dhambi yao, maana walikutenda mabaya; sasa twakuomba utuachilie kosa la watumwa wa Mungu wa baba yako. Yusufu akalia waliposema naye. Mwanzo 50:17

"So you shall tell Joseph, 'Now please forgive the disobedience of your brothers, and their sin, because they did evil to you.' Now, please forgive the disobedience of the servants of the God of your father." Joseph wept when they spoke to him.

Nduguze wakaenda tena, wakamwangukia miguu, wakasema, Tazama, sisi tu watumwa wako. Mwanzo 50:18

His brothers also went and fell down before his face; and they said, "Behold, we are your servants."

Yusufu akawaambia, Msiogope, je! Mimi ni badala ya Mungu? Mwanzo 50:19

Joseph said to them, "Don't be afraid, for am I in the place of God?

Nanyi kweli mlinikusudia mabaya, bali Mungu aliyakusudia kuwa mema, ili itokee kuokoa taifa kubwa, kama ilivyo leo. Mwanzo 50:20

As for you, you meant evil against me, but God meant it for good, to bring to pass, as it is this day, to save many people alive.

Basi sasa msiogope; mimi nitawalisha na watoto wenu. Akawafariji, na kusema nao vema. Mwanzo 50:21

Now therefore don't be afraid. I will nourish you and your little ones." He comforted them, and spoke kindly to them.

Akakaa Yusufu katika Misri, yeye na nyumba ya babaye. Akaishi Yusufu miaka mia na kumi. Mwanzo 50:22

Joseph lived in Egypt, he, and his father's house. Joseph lived one hundred ten years.

Yusufu akaona wana wa Efraimu hata kizazi cha tatu; na wana wa Makiri, mwana wa Manase, walizaliwa magotini mwa Yusufu. Mwanzo 50:23

Joseph saw Ephraim's children to the third generation. The children also of Machir, the son of Manasseh, were born on Joseph's knees.

Yusufu akawaambia nduguze, Mimi ninakufa, lakini Mungu atawajia ninyi bila shaka, atawapandisha toka nchi hii, mpaka nchi aliyowaapia Ibrahimu, na Isaka, na Yakobo. Mwanzo 50:24

Joseph said to his brothers, "I am dying, but God will surely visit you, and bring you up out of this land to the land which he swore to Abraham, to Isaac, and to Jacob."

Yusufu akawaapisha wana wa Israeli, akasema, Bila shaka Mungu atawajia ninyi, nanyi mtaipandisha huko mifupa yangu. Mwanzo 50:25

Joseph took an oath of the children of Israel, saying, "God will surely visit you, and you shall carry up my bones from here."

Basi Yusufu akafa, mwenye miaka mia na kumi; wakampaka dawa, wakamtia katika sanduku, huko Misri.

Mwanzo 50:26

So Joseph died, being one hundred ten years old, and they embalmed him, and he was put in a coffin in Egypt.