Mwanzo 39 Swahili & English

Listen/Download Audio
Mwanzo 39 (Swahili) Genesis 39 (English)

Basi Yusufu akaletwa mpaka Misri naye Potifa, akida wa Farao, mkuu wa askari, mtu wa Misri, akamnunua mkononi mwa hao Waishmaeli waliomleta huko. Mwanzo 39:1

Joseph was brought down to Egypt. Potiphar, an officer of Pharaoh's, the captain of the guard, an Egyptian, bought him from the hand of the Ishmaelites that had brought him down there.

Bwana akawa pamoja na Yusufu, naye akasitawi; naye alikuwa katika nyumba ya bwana wake, yule Mmisri. Mwanzo 39:2

Yahweh was with Joseph, and he was a prosperous man. He was in the house of his master the Egyptian.

Bwana wake akaona ya kwamba Bwana yu pamoja naye, na ya kuwa Bwana anafanikisha mambo yote mkononi mwake. Mwanzo 39:3

His master saw that Yahweh was with him, and that Yahweh made all that he did prosper in his hand.

Yusufu akaona neema machoni pake, akamtumikia. Naye akamweka awe msimamizi juu ya nyumba yake, na yote yaliyomo akayaweka mkononi mwake. Mwanzo 39:4

Joseph found favor in his sight. He ministered to him, and he made him overseer over his house, and all that he had he put into his hand.

Ikawa tokea wakati alipomweka awe msimamizi juu ya nyumba yake, na vyote vilivyomo, Bwana akabariki nyumba ya yule Mmisri kwa ajili ya Yusufu. Mbaraka wa Bwana ukawa juu ya vyote alivyokuwa navyo katika nyumba, na katika shamba. Mwanzo 39:5

It happened from the time that he made him overseer in his house, and over all that he had, that Yahweh blessed the Egyptian's house for Joseph's sake; and the blessing of Yahweh was on all that he had, in the house and in the field.

Akayaacha yote aliyokuwa nayo mkononi mwa Yusufu; wala hakujua habari za kitu cho chote chake, ila hicho chakula alichokula tu. Mwanzo 39:6

He left all that he had in Joseph's hand. He didn't concern himself with anything, except for the food which he ate. Joseph was well-built and handsome.

Ikawa baada ya mambo hayo, mke wa bwana wake akamtamani Yusufu, akamwambia, Lala nami. Mwanzo 39:7

It happened after these things, that his master's wife cast her eyes on Joseph; and she said, "Lie with me."

Lakini akakataa, akamwambia mke wa bwana wake, Tazama, bwana wangu hajui kitu kilichowekwa kwangu nyumbani, na vyote alivyo navyo amevitia mkononi mwangu. Mwanzo 39:8

But he refused, and said to his master's wife, "Behold, my master doesn't know what is with me in the house, and he has put all that he has into my hand.

Hakuna mkuu katika nyumba hii kuliko mimi, wala hakunizuilia kitu cho chote ila wewe, kwa kuwa wewe u mkewe. Nifanyeje ubaya huu mkubwa nikamkose Mungu? Mwanzo 39:9

He isn't greater in this house than I, neither has he kept back anything from me but you, because you are his wife. How then can I do this great wickedness, and sin against God?"

Akawa akizidi kusema na Yusufu siku baada ya siku, lakini hakumsikia alale naye, wala aongee naye. Mwanzo 39:10

It happened that as she spoke to Joseph day by day, that he didn't listen to her, to lie by her, or to be with her.

Ikawa, siku moja, akaingia nyumbani atende kazi yake, wala hapakuwa na mtu katika watu wa nyumbani humo ndani; Mwanzo 39:11

It happened about this time, that he went into the house to do his work, and there were none of the men of the house inside.

huyo mwanamke akamshika nguo zake, akisema, Lala nami. Yusufu akaiacha nguo yake mkononi mwake, akakimbia, akatoka nje. Mwanzo 39:12

She caught him by his garment, saying, "Lie with me!" He left his garment in her hand, and ran outside.

Ikawa alipoona ya kwamba amemwachilia nguo yake mkononi mwake, naye amekimbia nje, Mwanzo 39:13

It happened, when she saw that he had left his garment in her hand, and had run outside,

akawaita watu wa nyumbani mwake, akasema nao, akinena, Angalieni, ametuletea mtu Mwebrania atufanyie dhihaka. Ameingia kwangu, ili alale nami, nikalia kwa sauti kuu. Mwanzo 39:14

that she called to the men of her house, and spoke to them, saying, "Behold, he has brought in a Hebrew to us to mock us. He came in to me to lie with me, and I cried with a loud voice.

Ikawa, aliposikia ya kuwa nimepaza sauti yangu na kulia, aliiacha nguo yake kwangu, akakimbia, akatoka nje. Mwanzo 39:15

It happened, when he heard that I lifted up my voice and cried, that he left his garment by me, and ran outside."

Basi akaiweka ile nguo kwake hata bwana wake aje nyumbani. Mwanzo 39:16

She laid up his garment by her, until his master came home.

Naye akamwambia kama maneno hayo, akisema, Yule mtumwa Mwebrania uliyemleta kwetu, aliingia kwangu anidhihaki. Mwanzo 39:17

She spoke to him according to these words, saying, "The Hebrew servant, whom you have brought to us, came in to me to mock me,

Ikawa nilipopaza sauti yangu, nikalia, akaacha nguo yake kwangu akakimbia nje. Mwanzo 39:18

and it happened, as I lifted up my voice and cried, that he left his garment by me, and ran outside."

Ikawa bwana wake aliposikia maneno ya mkewe aliyomwambia, akisema, Mtumwa wako amenitendea mambo kama haya, hasira yake ikawaka. Mwanzo 39:19

It happened, when his master heard the words of his wife, which she spoke to him, saying, "This is what your servant did to me," that his wrath was kindled.

Bwana wake akamtwaa Yusufu, akamtia gerezani, mahali walipofungwa wafungwa wa mfalme, naye akawamo humo gerezani. Mwanzo 39:20

Joseph's master took him, and put him into the prison, the place where the king's prisoners were bound, and he was there in custody.

Lakini Bwana akawa pamoja na Yusufu, akamfadhili, akampa kibali machoni pa mkuu wa gereza. Mwanzo 39:21

But Yahweh was with Joseph, and showed kindness to him, and gave him favor in the sight of the keeper of the prison.

Mkuu wa gereza akawatia mkononi mwa Yusufu watu wote waliofungwa, waliomo gerezani; na yote yaliyofanyika humo ndiye aliyeyafanya. Mwanzo 39:22

The keeper of the prison committed to Joseph's hand all the prisoners who were in the prison. Whatever they did there, he was the doer of it.

Wala mkuu wa gereza hakuangalia neno lililoko mkononi mwa Yusufu; kwa kuwa Bwana alikuwa pamoja naye. Bwana akayafanikisha yote aliyoyafanya.

Mwanzo 39:23

The keeper of the prison didn't look after anything that was under his hand, because Yahweh was with him; and that which he did, Yahweh made it prosper.