Mwanzo BSB

Mwanzo 10

Genesis Chapter 10

1
Hivi ndivyo vizazi vya wana wa Nuhu, Shemu, na Hamu, na Yafethi. Na kwao walizaliwa wana wa kiume baada ya gharika.
This is the account of Noah’s sons Shem, Ham, and Japheth, who also had sons after the flood.
2
Wana wa Yafethi ni Gomeri, na Magogu, na Madai, na Yavani, na Tubali, na Mesheki, na Tirasi.
The sons of Japheth: Gomer, Magog, Madai, Javan, Tubal, Meshech, and Tiras.
3
Na wana wa Gomeri ni Ashkenazi, na Rifathi, na Togama.
The sons of Gomer: Ashkenaz, Riphath, and Togarmah.
4
Na wana wa Yavani ni Elisha, Tarshishi, Kitimu, na Warodani.
And the sons of Javan: Elishah, Tarshish, the Kittites, and the Rodanites.
5
Kwa hao nchi za pwani za mataifa ziligawanyikana kuwa nchi zao, kila moja kwa lugha yake, kwa jamaa zao, kufuata mataifa yao.
From these, the maritime peoples separated into their territories, according to their languages, by clans within their nations.
6
Na wana wa Hamu ni Kushi, na Misri, na Putu, na Kanaani.
The sons of Ham: Cush, Mizraim, Put, and Canaan.
7
Na wana wa Kushi ni Seba, na Havila, na Sabta, na Raama, na Sabteka. Na wana wa Raama ni Sheba, na Dedani.
The sons of Cush: Seba, Havilah, Sabtah, Raamah, and Sabteca. And the sons of Raamah: Sheba and Dedan.
8
Kushi akamzaa Nimrodi, akaanza kuwa mtu hodari katika nchi.
Cush was the father of Nimrod, who began to be a mighty one on the earth.
9
Alikuwa hodari kuwinda wanyama mbele za Bwana. Kwa hiyo watu hunena, Kama Nimrodi, hodari wa kuwinda wanyama mbele za Bwana.
He was a mighty hunter before the LORD; so it is said, “Like Nimrod, a mighty hunter before the LORD.”
10
Mwanzo wa ufalme wake ulikuwa Babeli na Ereku, na Akadi, na Kalne, katika nchi ya Shinari.
His kingdom began in Babylon, Erech, Accad, and Calneh, in the land of Shinar.
11
Akatoka katika nchi ile akaenda mpaka Ashuru, akajenga Ninawi, na Rehoboth-iri, na Kala;
From that land he went forth into Assyria, where he built Nineveh, Rehoboth-Ir, Calah,
12
na Reseni, kati ya Ninawi na Kala, nao ni mji mkubwa.
and Resen, which is between Nineveh and the great city of Calah.
13
Misri akazaa Waludi, na Waanami, na Walehabi, na Wanaftuhi,
Mizraim was the father of the Ludites, the Anamites, the Lehabites, the Naphtuhites,
14
na Wapathrusi, na Wakasluhi; huko ndiko walikotoka Wafilisti na Wakaftori.
the Pathrusites, the Casluhites (from whom the Philistines came), and the Caphtorites.
15
Kanaani akamzaa Sidoni, mwanawe wa kwanza, na Hethi,
And Canaan was the father of Sidon his firstborn, and of the Hittites,
16
na Myebusi, na Mwamori, na Mgirgashi,
the Jebusites, the Amorites, the Girgashites,
17
na Mhivi, na Mwarki, na Msini,
the Hivites, the Arkites, the Sinites,
18
na Mwarvadi, na Msemari, na Mhamathi. Baadaye jamaa za Wakanaani walitawanyikana.
the Arvadites, the Zemarites, and the Hamathites. Later the Canaanite clans were scattered,
19
Na mpaka wa Wakanaani ulianza kutoka Sidoni kwa njia ya Gerari hata Gaza; tena kwa njia ya Sodoma, na Gomora, na Adma, na Seboimu, hata Lasha.
and the borders of Canaan extended from Sidon toward Gerar as far as Gaza, and then toward Sodom, Gomorrah, Admah, and Zeboiim, as far as Lasha.
20
Hao ndio wana wa Hamu, kufuata jamaa zao, kwa lugha zao, katika nchi zao, kufuata mataifa yao.
These are the sons of Ham according to their clans, languages, lands, and nations.
21
Naye Shemu ambaye ni baba wa wana wote wa Eberi, na ndugu mkubwa wa Yafethi, akazaliwa wana.
And sons were also born to Shem, the older brother of Japheth; Shem was the forefather of all the sons of Eber.
22
Wana wa Shemu ni Elamu, na Ashuru, na Arfaksadi, na Ludi, na Aramu.
The sons of Shem: Elam, Asshur, Arphaxad, Lud, and Aram.
23
Na wana wa Aramu ni Usi, na Huli, na Getheri, na Mashi.
The sons of Aram: Uz, Hul, Gether, and Mash.
24
Arfaksadi akamzaa Sela, Sela akamzaa Eberi.
Arphaxad was the father of Shelah, and Shelah was the father of Eber.
25
Eberi akazaliwa wana wawili wa kiume; jina la wa kwanza ni Pelegi maana katika siku zake nchi iligawanyika; na jina la nduguye ni Yoktani.
Two sons were born to Eber: One was named Peleg, because in his days the earth was divided, and his brother was named Joktan.
26
Yoktani akamzaa Almodadi, na Shelefu, na Hasarmawethi, na Yera,
And Joktan was the father of Almodad, Sheleph, Hazarmaveth, Jerah,
27
na Hadoramu, na Uzali, na Dikla,
Hadoram, Uzal, Diklah,
28
na Obali, na Abimaeli, na Seba,
Obal, Abimael, Sheba,
29
na Ofiri, na Havila, na Yobabi. Hao wote ndio wana wa Yoktani.
Ophir, Havilah, and Jobab. All these were sons of Joktan.
30
Makao yao yalikuwa kutoka Mesha kwa njia ya Sefari, mlima wa mashariki.
Their territory extended from Mesha to Sephar, in the eastern hill country.
31
Hao ndio wana wa Shemu, kufuata jamaa zao, na lugha zao, katika nchi zao, kufuata mataifa yao.
These are the sons of Shem, according to their clans, languages, lands, and nations.
32
Hizo ndizo jamaa za wana wa Nuhu, kufuata vizazi vyao, katika mataifa yao; na kwa hao mataifa yaligawanyika katika nchi baada ya gharika.
All these are the clans of Noah’s sons, according to their generations and nations. From these the nations of the earth spread out after the flood.

Chagua Sura