Ezekieli 1 Swahili & English

Listen/Download Audio
Ezekieli 1 (Swahili) Ezekiel 1 (English)

Ikawa katika mwaka wa thelathini, mwezi wa nne, siku ya tano ya mwezi, nilipokuwa pamoja na watu waliohamishwa, karibu na mto Kebari, mbingu zilifunuka, nikaona maono ya Mungu. Ezekieli 1:1

Now it happened in the thirtieth year, in the fourth [month], in the fifth [day] of the month, as I was among the captives by the river Chebar, that the heavens were opened, and I saw visions of God.

Siku ya tano ya mwezi, nao ulikuwa ni mwaka wa tano wa kuhamishwa kwake mfalme Yehoyakini, Ezekieli 1:2

In the fifth [day] of the month, which was the fifth year of king Jehoiachin's captivity,

neno la Bwana lilimjia Ezekielii, kuhani, mwana wa Buzi, kwa dhahiri, katika nchi ya Wakaldayo, karibu na mto Kebari; na mkono wa Bwana ulikuwa hapo juu yake. Ezekieli 1:3

the word of Yahweh came expressly to Ezekiel the priest, the son of Buzi, in the land of the Chaldeans by the river Chebar; and the hand of Yahweh was there on him.

Nikaona, na tazama, upepo wa dhoruba ulitoka upande wa kaskazini, wingu kubwa sana, pamoja na moto, ukifanya duara ya nuru, na mwangaza pande zote, na katikati yake kitu kama rangi ya kaharabu, katikati ya moto huo. Ezekieli 1:4

I looked, and, behold, a stormy wind came out of the north, a great cloud, with flashing lightning, and a brightness round about it, and out of the midst of it as it were glowing metal, out of the midst of the fire.

Kukatokea katikati yake mfano wa viumbe hai vinne. Kuonekana kwao kulikuwa hivi; walikuwa na sura ya mwanadamu. Ezekieli 1:5

Out of the midst of it came the likeness of four living creatures. This was their appearance: they had the likeness of a man.

Na kila mmoja alikuwa na nyuso nne, na kila mmoja alikuwa na mabawa manne. Ezekieli 1:6

Everyone had four faces, and everyone of them had four wings.

Na miguu yao ilikuwa miguu iliyonyoka; na nyayo za miguu yao zilikuwa kama nyayo za miguu ya ndama; zikimetameta kama rangi ya shaba iliyosuguliwa sana. Ezekieli 1:7

Their feet were straight feet; and the sole of their feet was like the sole of a calf's foot; and they sparkled like burnished brass.

Nao walikuwa na mikono ya mwanadamu chini ya mabawa yao, pande zote nne; na wote wanne walikuwa na nyuso zao na mabawa yao hivi; Ezekieli 1:8

They had the hands of a man under their wings on their four sides; and they four had their faces and their wings [thus]:

mabawa yao yaliungana, hili na hili; nao hawakugeuka walipokwenda, walikwenda kila mmoja kuelekea mbele. Ezekieli 1:9

their wings were joined one to another; they didn't turn when they went; they went everyone straight forward.

Kwa habari za mfano wa nyuso zao; walikuwa na uso wa mwanadamu; na hao wanne walikuwa na uso wa simba upande wa kuume; na hao wanne walikuwa na uso wa ng'ombe upande wa kushoto; na hao wanne walikuwa na uso wa tai pia. Ezekieli 1:10

As for the likeness of their faces, they had the face of a man; and they four had the face of a lion on the right side; and they four had the face of an ox on the left side; they four had also the face of an eagle.

Na nyuso zao na mabawa yao yalikuwa yametengana kwa juu; mabawa mawili ya kila mmoja yaliungana, hili na hili, na mawili yalifunika miili yao. Ezekieli 1:11

Their faces and their wings were separate above; two [wings] of everyone were joined one to another, and two covered their bodies.

Nao walikwenda kuelekea mbele, kila mmoja wao; roho ilikotaka kwenda ndiko walikokwenda; hawakugeuka walipokwenda. Ezekieli 1:12

They went everyone straight forward: where the spirit was to go, they went; they didn't turn when they went.

Kwa habari za kuonekana kwao vile viumbe hai; kuonekana kwao kulikuwa kama makaa ya moto yawakayo, kama kuonekana kwa vinga vya moto; moto ule ulikuwa ukienda juu na kushuka chini, katikati ya vile viumbe hai; na ule moto ulikuwa na mwangaza mwingi, na katika ule moto ulitoka umeme. Ezekieli 1:13

As for the likeness of the living creatures, their appearance was like burning coals of fire, like the appearance of torches: [the fire] went up and down among the living creatures; and the fire was bright, and out of the fire went forth lightning.

Na vile viumbe hai walipiga mbio, kwenda na kurudi, kama kuonekana kwa kumulika kwa umeme. Ezekieli 1:14

The living creatures ran and returned as the appearance of a flash of lightning.

Basi, nilipokuwa nikivitazama vile viumbe hai, tazama, gurudumu moja juu ya nchi, karibu na kila kimoja cha vile viumbe hai, pande zake zote nne. Ezekieli 1:15

Now as I saw the living creatures, behold, one wheel on the earth beside the living creatures, for each of the four faces of it.

Kuonekana kwake magurudumu hayo na kazi yake kulikuwa kama rangi ya zabarajadi; nayo yote manne yalikuwa na mfano mmoja; na kuonekana kwake na kazi yake kulikuwa kana kwamba ni gurudumu ndani ya gurudumu lingine. Ezekieli 1:16

The appearance of the wheels and their work was like a beryl: and they four had one likeness; and their appearance and their work was as it were a wheel within a wheel.

Yalipokwenda yalikwenda pande zote nne; hayakugeuka yalipokwenda. Ezekieli 1:17

When they went, they went in their four directions: they didn't turn when they went.

Katika habari za vivimbe vyake; vilikuwa virefu, vya kutisha; nayo yote manne, vivimbe vyake vimejaa macho pande zote. Ezekieli 1:18

As for their rims, they were high and dreadful; and they four had their rims full of eyes round about.

Na viumbe hao walipokwenda, magurudumu yalikwenda kandokando yao, na viumbe hao walipoinuliwa, magurudumu nayo yaliinuliwa. Ezekieli 1:19

When the living creatures went, the wheels went beside them; and when the living creatures were lifted up from the earth, the wheels were lifted up.

Kila mahali ambako roho hiyo ilitaka kwenda, walikwenda; walikuwa na roho ya kwenda huko; nayo magurudumu yaliinuliwa karibu nao; kwa maana roho ya viumbe hai ilikuwa ndani ya magurudumu. Ezekieli 1:20

Wherever the spirit was to go, they went; there was the spirit to go: and the wheels were lifted up beside them; for the spirit of the living creature was in the wheels.

Walipokwenda hao, yalikwenda hayo nayo; na waliposimama hao, yalisimama hayo nayo; na walipoinuliwa hao juu ya nchi, magurudumu yaliinuliwa karibu nao; maana roho ya viumbe hai ilikuwa ndani ya magurudumu. Ezekieli 1:21

When those went, these went; and when those stood, these stood; and when those were lifted up from the earth, the wheels were lifted up beside them: for the spirit of the living creature was in the wheels.

Tena juu ya vichwa vya viumbe hai palikuwa na kitu mfano wa anga, kama rangi ya bilauri, lenye kutisha, limetandwa juu ya vichwa vyao. Ezekieli 1:22

Over the head of the living creature there was the likeness of an expanse, like the awesome crystal to look on, stretched forth over their heads above.

Na chini ya anga mabawa yao yamenyoshwa, moja kulielekea la pili; kila mmoja alikuwa na mawili yaliyowafunika miili yao upande mmoja, na kila mmoja alikuwa na mawili yaliyowafunika miili yao upande wa pili. Ezekieli 1:23

Under the expanse were their wings straight, the one toward the other: everyone had two which covered on this side, and every one had two which covered on that side, their bodies.

Nao walipokwenda nalisikia mshindo wa mabawa yao, kama mshindo wa maji makuu, kama sauti yake Mwenyezi, mshindo wa mvumo, kama mshindo wa jeshi; hapo waliposimama walishusha mabawa yao. Ezekieli 1:24

When they went, I heard the noise of their wings like the noise of great waters, like the voice of the Almighty, a noise of tumult like the noise of a host: when they stood, they let down their wings.

Tena palikuwa na sauti juu ya anga lile, lililokuwa juu ya vichwa vyao; hapo waliposimama walishusha mabawa yao. Ezekieli 1:25

There was a voice above the expanse that was over their heads: when they stood, they let down their wings.

Na juu ya anga, lililokuwa juu ya vichwa vyao, palikuwa na mfano wa kiti cha enzi, kuonekana kwake kama yakuti samawi; na juu ya mfano huo wa kiti cha enzi, ulikuwako mfano kama kuonekana kwa mfano wa mwanadamu juu yake. Ezekieli 1:26

Above the expanse that was over their heads was the likeness of a throne, as the appearance of a sapphire{or, lapis lazuli} stone; and on the likeness of the throne was a likeness as the appearance of a man on it above.

Nikaona kana kwamba ni rangi ya kaharabu, kama kuonekana kwa moto ndani yake pande zote, tangu kuonekana kwa viuno vyake na juu; na tangu kuonekana kwa viuno vyake na chini, naliona kana kwamba ni kuonekana kwa moto; tena palikuwa na mwangaza pande zake zote. Ezekieli 1:27

I saw as it were glowing metal, as the appearance of fire within it round about, from the appearance of his loins and upward; and from the appearance of his loins and downward I saw as it were the appearance of fire, and there was brightness round about him.

Kama kuonekana kwa upinde wa mvua, ulio katika mawingu siku ya mvua, ndivyo kulivyokuwa kuonekana kwa mwangaza ule pande zote. Ndivyo kulivyokuwa kuonekana kwake mfano huo wa utukufu wa Bwana. Nami nilipoona nalianguka kifudifudi, nikasikia sauti ya mmoja anenaye. Ezekieli 1:28

As the appearance of the bow that is in the cloud in the day of rain, so was the appearance of the brightness round about. This was the appearance of the likeness of the glory of Yahweh. When I saw it, I fell on my face, and I heard a voice of one that spoke.