Ezekieli 19 Swahili & English

Listen/Download Audio
Ezekieli 19 (Swahili) Ezekiel 19 (English)

Tena uwaombolezee wakuu wa Israeli, Ezekieli 19:1

Moreover, take up a lamentation for the princes of Israel,

useme, Mama yako alikuwa nini? Simba mke; alijilaza kati ya simba, kati ya wana-simba aliwalisha watoto wake. Ezekieli 19:2

and say, What was your mother? A lioness: she couched among lions, in the midst of the young lions she nourished her cubs.

Akamlea mtoto mmoja katika watoto wake, akawa mwana-simba, akajifunza kuwinda mawindo, akala watu. Ezekieli 19:3

She brought up one of her cubs: he became a young lion, and he learned to catch the prey; he devoured men.

Mataifa nao wakapata habari zake, akanaswa katika rima lao, wakamchukua kwa kulabu mpaka nchi ya Misri. Ezekieli 19:4

The nations also heard of him; he was taken in their pit; and they brought him with hooks to the land of Egypt.

Basi mamaye alipoona kwamba amemngoja, na tumaini lake limepotea, akatwaa mtoto mwingine katika watoto wake, akamfanya mwana-simba. Ezekieli 19:5

Now when she saw that she had waited, and her hope was lost, then she took another of her cubs, and made him a young lion.

Naye akaenda huko na huko kati ya simba, akawa mwana-simba, akajifunza kuwinda mawindo, akala watu. Ezekieli 19:6

He went up and down among the lions; he became a young lion, and he learned to catch the prey; he devoured men.

Akayajua majumba yao, akaiharibu miji yao; nchi ikawa ukiwa, navyo vitu vilivyoijaza, kwa sababu ya mshindo wa kunguruma kwake. Ezekieli 19:7

He knew their palaces, and laid waste their cities; and the land was desolate, and the fullness of it, because of the noise of his roaring.

Ndipo mataifa wakajipanga juu yake pande zote toka nchi zote; wakaunda wavu wao juu yake; akanaswa katika rima lao. Ezekieli 19:8

Then the nations set against him on every side from the provinces; and they spread their net over him; he was taken in their pit.

Wakamtia katika tundu kwa kulabu, wakamleta kwa mfalme wa Babeli wakamtia ndani ya ngome, sauti yake isisikiwe tena juu ya milima ya Israeli. Ezekieli 19:9

They put him in a cage with hooks, and brought him to the king of Babylon; they brought him into strongholds, that his voice should no more be heard on the mountains of Israel.

Mama yako alikuwa kama mzabibu, katika damu yako, uliopandwa karibu na maji; akazaa sana na kujaa matawi, kwa sababu ya maji mengi. Ezekieli 19:10

Your mother was like a vine, in your blood, planted by the waters: it was fruitful and full of branches by reason of many waters.

Naye alikuwa na vijiti vya nguvu, kwa fimbo za enzi zao watawalao, na kimo chao kiliinuka kati ya matawi manene, wakaonekana kwa urefu wao, pamoja na wingi wa matawi yao. Ezekieli 19:11

It had strong rods for the scepters of those who bore rule, and their stature was exalted among the thick boughs, and they were seen in their height with the multitude of their branches.

Lakini aling'olewa kwa ghadhabu, akaangushwa chini, upepo wa mashariki ukakausha matunda yake; vijiti vyake vya nguvu vikavunjika, vikakauka; moto ulivila. Ezekieli 19:12

But it was plucked up in fury, it was cast down to the ground, and the east wind dried up its fruit: its strong rods were broken off and withered; the fire consumed them.

Na sasa umepandwa jangwani, katika nchi kavu, ya ukame. Ezekieli 19:13

Now it is planted in the wilderness, in a dry and thirsty land.

Na moto umetoka katika vijiti vya matawi yake, umekula matunda yake, hata hana tena kijiti cha nguvu kifaacho kwa fimbo ya enzi ya kutawala. Na hayo ni maombolezo, nayo yatakuwa maombolezo. Ezekieli 19:14

Fire is gone out of the rods of its branches, it has devoured its fruit, so that there is in it no strong rod to be a scepter to rule. This is a lamentation, and shall be for a lamentation.