Ezekieli 9 Swahili & English
Listen/Download AudioEzekieli 9 (Swahili) | Ezekiel 9 (English) |
---|---|
Kisha akalia kwa sauti kuu masikioni mwangu, akisema, Waamuru wale wanaousimamia mji wakaribie, kila mmoja na awe na kitu chake cha kuangamiza mkononi mwake. Ezekieli 9:1 |
Then he cried in my ears with a loud voice, saying, Cause you them that have charge over the city to draw near, every man with his destroying weapon in his hand. |
Na tazama, watu sita wakaja, wakitokea kwa njia ya lango la juu, lielekealo upande wa kaskazini, kila mmoja ana kitu chake cha kufisha mkononi mwake; na mtu mmoja kati yao amevaa bafta, naye ana kidau cha wino cha mwandishi kiunoni. Wakaingia, wakasimama karibu na madhabahu ya shaba. Ezekieli 9:2 |
Behold, six men came from the way of the upper gate, which lies toward the north, every man with his slaughter weapon in his hand; and one man in the midst of them clothed in linen, with a writer's inkhorn by his side. They went in, and stood beside the brazen altar. |
Na huo utukufu wa Bwana wa Israeli ulikuwa umepanda juu kutoka kwa kerubi, ambaye ulikuwa juu yake, mpaka kizingiti cha nyumba; akamwita mtu yule aliyekuwa amevaa bafta, mwenye kidau cha wino cha mwandishi kiunoni. Ezekieli 9:3 |
The glory of the God of Israel was gone up from the cherub, whereupon it was, to the threshold of the house: and he called to the man clothed in linen, who had the writer's inkhorn by his side. |
Bwana akamwambia, Pita kati ya mji, kati ya Yerusalemu, ukatie alama katika vipaji vya nyuso vya watu wanaougua na kulia kwa sababu ya machukizo yote yanayofanyika kati yake. Ezekieli 9:4 |
Yahweh said to him, Go through the midst of the city, through the midst of Jerusalem, and set a mark on the foreheads of the men that sigh and that cry over all the abominations that are done in the midst of it. |
Na hao wengine aliwaambia, nami nalisikia, Piteni kati ya mji nyuma yake, mkapige; jicho lenu lisiachilie, wala msione huruma; Ezekieli 9:5 |
To the others he said in my hearing, Go you through the city after him, and strike: don't let your eye spare, neither have you pity; |
Waueni kabisa, mzee, na kijana, na msichana, na watoto wachanga, na wanawake; lakini msimkaribie mtu ye yote mwenye hiyo alama; tena anzeni katika patakatifu pangu. Basi, wakaanza kwa wazee waliokuwa mbele ya nyumba. Ezekieli 9:6 |
kill utterly the old man, the young man and the virgin, and little children and women; but don't come near any man on whom is the mark: and begin at my sanctuary. Then they began at the old men that were before the house. |
Akawaambia, itieni nyumba unajisi, mkazijaze nyua mizoga ya hao waliouawa; haya, enendeni. Wakaenenda, wakapiga-piga katika mji. Ezekieli 9:7 |
He said to them, Defile the house, and fill the courts with the slain: go you forth. They went forth, and struck in the city. |
Tena ikawa, walipokuwa wakipiga, nami nikiachwa, nalianguka kifudifudi, nikalia, nikasema, Ee Bwana MUNGU! Utaangamiza mabaki yote ya Israeli, wakati wa kumwaga ghadhabu yako juu ya Yerusalemu? Ezekieli 9:8 |
It happened, while they were smiting, and I was left, that I fell on my face, and cried, and said, Ah Lord Yahweh! will you destroy all the residue of Israel in your pouring out of your wrath on Jerusalem? |
Ndipo akaniambia, Uovu wa nyumba ya Israeli na Yuda ni mwingi sana, nayo nchi imejaa damu, nao mji umejaa kupotosha hukumu; maana husema, Bwana ameiacha nchi hii, naye Bwana haoni. Ezekieli 9:9 |
Then said he to me, The iniquity of the house of Israel and Judah is exceeding great, and the land is full of blood, and the city full of wrestling [of judgment]: for they say, Yahweh has forsaken the land, and Yahweh doesn't see. |
Nami, jicho langu halitaachilia, wala sitaona huruma; lakini nitaleta njia yao juu ya vichwa vyao. Ezekieli 9:10 |
As for me also, my eye shall not spare, neither will I have pity, but I will bring their way on their head. |
Na tazama, mtu yule aliyevaa bafta, mwenye kidau cha wino kiunoni, akaleta habari, akisema, Nimefanya kama ulivyoniamuru. Ezekieli 9:11 |
Behold, the man clothed in linen, who had the inkhorn by his side, reported the matter, saying, I have done as you have commanded me. |