Ezekieli 8 Swahili & English

Listen/Download Audio
Ezekieli 8 (Swahili) Ezekiel 8 (English)

Ikawa katika mwaka wa sita, mwezi wa sita, siku ya tano ya mwezi, nilipokuwa nikikaa nyumbani mwangu, wazee wa Yuda nao wali wamekaa mbele yangu, mkono wa Bwana MUNGU ukaniangukia huko. Ezekieli 8:1

It happened in the sixth year, in the sixth [month], in the fifth [day] of the month, as I sat in my house, and the elders of Judah sat before me, that the hand of the Lord Yahweh fell there on me.

Ndipo nikaangalia, na tazama, kana kwamba ni mfano wa moto; tangu mfano wa viuno vyake na chini, moto; na tangu mfano wa viuno vyake na juu, kana kwamba ni mfano wa mwangaza, kama rangi ya kaharabu. Ezekieli 8:2

Then I saw, and, behold, a likeness as the appearance of fire; from the appearance of his loins and downward, fire; and from his loins and upward, as the appearance of brightness, as it were glowing metal.

Naye akanyosha mfano wa mkono, akanishika kwa kishungi kimoja cha nywele za kichwa changu; nayo roho ikaniinua kati ya dunia na mbingu, ikanileta katika maono ya Mungu mpaka Yerusalemu, mpaka mlango wa kuingilia ua wa ndani uelekeao upande wa kaskazini; mahali palipokuwa pamewekwa sanamu ya wivu, itiayo wivu. Ezekieli 8:3

He put forth the form of a hand, and took me by a lock of my head; and the Spirit lifted me up between earth and the sky, and brought me in the visions of God to Jerusalem, to the door of the gate of the inner [court] that looks toward the north; where was the seat of the image of jealousy, which provokes to jealousy.

Na tazama, huo utukufu wa Mungu wa Israeli ulikuwapo hapo, sawasawa na maono yale niliyoyaona katika uwanda. Ezekieli 8:4

Behold, the glory of the God of Israel was there, according to the appearance that I saw in the plain.

Ndipo akaniambia, Mwanadamu, inua macho yako sasa, uangalie upande wa kaskazini. Basi nikainua macho yangu, nikaangalia upande wa kaskazini, na tazama, upande wa kaskazini wa mlango, ilikuwako sanamu ile ya wivu, mahali pale pa kuingilia. Ezekieli 8:5

Then said he to me, Son of man, lift up your eyes now the way toward the north. So I lifted up my eyes the way toward the north, and see, northward of the gate of the altar this image of jealousy in the entry.

Akaniambia, Mwanadamu, je! Unayaona wanayoyafanya, yaani, haya machukizo makubwa wanayoyafanya nyumba ya Israeli hapa, hata niende zangu mbali na patakatifu pangu? Lakini utaona tena machukizo makubwa mengine. Ezekieli 8:6

He said to me, Son of man, see you what they do? even the great abominations that the house of Israel do commit here, that I should go far off from my sanctuary? but you shall again see yet other great abominations.

Akanileta hata mlango wa ua; nami nilipoangalia, tazama, pana tundu katika ukuta. Ezekieli 8:7

He brought me to the door of the court; and when I looked, behold, a hole in the wall.

Ndipo akaniambia, Mwanadamu, toboa sasa katika ukuta huu; nami nilipotoboa, tazama, pana mlango. Ezekieli 8:8

Then said he to me, Son of man, dig now in the wall: and when I had dug in the wall, behold, a door.

Akaniambia, Ingia uyaone machukizo mabaya wanayoyafanya hapa. Ezekieli 8:9

He said to me, Go in, and see the wicked abominations that they do here.

Basi, nikaingia, nikaona; na tazama, kila namna ya wadudu, na wanyama wachukizao, na taswira za vinyago vyote vya nyumba ya Israeli, zimepigwa ukutani pande zote. Ezekieli 8:10

So I went in and saw; and see, every form of creeping things, and abominable animals, and all the idols of the house of Israel, portrayed on the wall round about.

Na watu sabini wa wazee wa Israeli walikuwa wamesimama na kuzielekea, na katikati yao alisimama Yaazania, mwana wa Shafani; kila mmoja ana chetezo mkononi mwake, na harufu ya moshi wa uvumba ilipaa juu. Ezekieli 8:11

There stood before them seventy men of the elders of the house of Israel; and in the midst of them stood Jaazaniah the son of Shaphan, every man with his censer in his hand; and the odor of the cloud of incense went up.

Kisha akaniambia, Mwanadamu, umeyaona wanayotenda wazee wa nyumba ya Israeli gizani, kila mtu ndani ya vyumba vyake vya sanamu? Maana husema, Bwana hatuoni; Bwana ameiacha nchi hii. Ezekieli 8:12

Then said he to me, Son of man, have you seen what the elders of the house of Israel do in the dark, every man in his chambers of imagery? for they say, Yahweh doesn't see us; Yahweh has forsaken the land.

Akaniambia tena, Utaona tena machukizo makubwa mengine wanayoyatenda. Ezekieli 8:13

He said also to me, You shall again see yet other great abominations which they do.

Ndipo akanileta mpaka mlango wa kuingilia katika nyumba ya Bwana, ulioelekea upande wa kaskazini, na tazama, wanawake wameketi wakimlilia Tamuzi. Ezekieli 8:14

Then he brought me to the door of the gate of Yahweh's house which was toward the north; and see, there sat the women weeping for Tammuz.

Akaniambia, Mwanadamu umeyaona haya? Utaona tena machukizo makubwa kuliko hayo. Ezekieli 8:15

Then said he to me, Have you seen [this], son of man? you shall again see yet greater abominations than these.

Akanileta mpaka ua wa ndani wa nyumba ya Bwana, na tazama, mlangoni pa hekalu la Bwana, kati ya ukumbi na madhabahu, walikuwako watu kama ishirini na watano, wamelipa kisogo hekalu la Bwana, na nyuso zao zimeelekea upande wa mashariki, nao wanaliabudu jua, kwa kuuelekea upande wa mashariki. Ezekieli 8:16

He brought me into the inner court of Yahweh's house; and see, at the door of the temple of Yahweh, between the porch and the altar, were about twenty-five men, with their backs toward the temple of Yahweh, and their faces toward the east; and they were worshipping the sun toward the east.

Basi, akaniambia, Umeyaona haya, Ee mwanadamu? Je! Ni jambo dogo sana kwa nyumba ya Yuda, wayafanye machukizo wanayoyafanya hapa? Kwa maana wameijaza nchi hii udhalimu, tena wamerejea nyuma ili kunikasirisha; na, tazama, wanaliweka tawi puani. Ezekieli 8:17

Then he said to me, Have you seen [this], son of man? Is it a light thing to the house of Judah that they commit the abominations which they commit here? for they have filled the land with violence, and have turned again to provoke me to anger: and, behold, they put the branch to their nose.

Kwa sababu hiyo mimi nami nitatenda kwa ghadhabu; jicho langu halitaachilia, wala sitaona huruma, na wajapolia masikioni mwangu kwa sauti kuu, sitawasikiliza. Ezekieli 8:18

Therefore will I also deal in wrath; my eye shall not spare, neither will I have pity; and though they cry in my ears with a loud voice, yet will I not hear them.