1 Samweli 22 Swahili & English

Listen/Download Audio
1 Samweli 22 (Swahili) 1st Samuel 22 (English)

Basi Daudi akaondoka huko, akakimbilia pango la Adulamu; na ndugu zake na watu wote wa mbari ya baba yake waliposikia habari hiyo, wakamwendea huko. 1 Samweli 22:1

David therefore departed there, and escaped to the cave of Adullam: and when his brothers and all his father's house heard it, they went down there to him.

Na kila mtu aliyekuwa katika hali ya dhiki, na kila mtu aliyekuwa na deni, na watu wote wenye uchungu mioyoni mwao, wakakusanyika kwake; naye akawa jemadari wao; nao waliokuwa pamoja naye walipata kama watu mia nne. 1 Samweli 22:2

Everyone who was in distress, and everyone who was in debt, and everyone who was discontented, gathered themselves to him; and he became captain over them: and there were with him about four hundred men.

Kutoka huko Daudi akaenda Mispa ya Moabu; akamwambia mfalme wa Moabu, Tafadhali ukubali baba yangu na mama yangu watoke huko waliko, wakakae kwenu, hata nitakapojua Mungu atakalotenda kwa ajili yangu. 1 Samweli 22:3

David went there to Mizpeh of Moab: and he said to the king of Moab, Please let my father and my mother come forth, [and be] with you, until I know what God will do for me.

Akawaleta mbele ya mfalme wa Moabu, nao wakakaa pamoja naye wakati wote Daudi alipokuwa ngomeni. 1 Samweli 22:4

He brought them before the king of Moab: and they lived with him all the while that David was in the stronghold.

Kisha nabii Gadi akamwambia Daudi, Usikae hapa ngomeni; ondoka, ukaende mpaka nchi ya Yuda. Ndipo Daudi akaondoka, akaenda zake, akakaa katika msitu wa Herethi. 1 Samweli 22:5

The prophet Gad said to David, Don't stay in the stronghold; depart, and get you into the land of Judah. Then David departed, and came into the forest of Hereth.

Kisha Sauli akasikia ya kwamba Daudi ameonekana, na wale watu waliokuwa pamoja naye. Basi Sauli alikuwa akikaa Gibea, chini ya mkwaju katika mahali palipoinuka, naye alikuwa na mkuki wake mkononi, na watumishi wake wote wakimzunguka. 1 Samweli 22:6

Saul heard that David was discovered, and the men who were with him: now Saul was sitting in Gibeah, under the tamarisk tree in Ramah, with his spear in his hand, and all his servants were standing about him.

Naye Sauli akawaambia watumishi wake waliomzunguka, Sikieni sasa, enyi Wabenyamini; je! Huyu mwana wa Yese atawapa ninyi kila mmoja mashamba, na mashamba ya mizabibu, atawafanya kuwa maakida wa watu elfu, na maakida wa watu mia; 1 Samweli 22:7

Saul said to his servants who stood about him, Hear now, you Benjamites; will the son of Jesse give everyone of you fields and vineyards, will he make you all captains of thousands and captains of hundreds,

hata ninyi nyote mkafanya fitina juu yangu, wala hapana mtu anifunuliaye habari hii mwanangu afanyapo agano na mwana wa Yese, wala hapana mmoja wenu anayenisikitikia, wala kunifunulia ya kuwa mwanangu amemwondokesha mtumishi wangu juu yangu, anivizie kama hivi leo? 1 Samweli 22:8

that all of you have conspired against me, and there is none who discloses to me when my son makes a league with the son of Jesse, and there is none of you who is sorry for me, or discloses to me that my son has stirred up my servant against me, to lie in wait, as at this day?

Ndipo akajibu Doegi, Mwedomi, aliyesimama karibu na watumishi wa Sauli, akasema, Mimi nalimwona mwana wa Yese akienda Nobu, kwa Ahimeleki, mwana wa Ahitubu. 1 Samweli 22:9

Then answered Doeg the Edomite, who stood by the servants of Saul, and said, I saw the son of Jesse coming to Nob, to Ahimelech the son of Ahitub.

Naye akamwuliza Bwana kwa ajili yake, akampa vyakula, akampa na ule upanga wa Goliathi, Mfilisti. 1 Samweli 22:10

He inquired of Yahweh for him, and gave him food, and gave him the sword of Goliath the Philistine.

Ndipo mfalme akatuma watu waende kumwita Ahimeleki, kuhani, mwana wa Ahitubu, na jamaa yote ya baba yake, hao makuhani, waliokuwako huko Nobu; nao wakaenda kwa mfalme wote pia. 1 Samweli 22:11

Then the king sent to call Ahimelech the priest, the son of Ahitub, and all his father's house, the priests who were in Nob: and they came all of them to the king.

Sauli akasema, Sikia sasa, Ewe mwana wa Ahitubu. Naye akaitika, Mimi hapa, bwana wangu. 1 Samweli 22:12

Saul said, Hear now, you son of Ahitub. He answered, Here I am, my lord.

Sauli akamwuliza, Mbona mmefanya fitina juu yangu, wewe na mwana wa Yese? Kwa maana umempa mikate, na upanga, nawe umemwuliza Mungu kwa ajili yake, ili aniondokee na kunivizia kama hivi leo? 1 Samweli 22:13

Saul said to him, Why have you conspired against me, you and the son of Jesse, in that you have given him bread, and a sword, and have inquired of God for him, that he should rise against me, to lie in wait, as at this day?

Basi Ahimeleki akamjibu mfalme, akasema, Katika watumishi wako wote ni nani aliye mwaminifu kama Daudi, aliye mkwewe mfalme, tena msiri wako, mwenye heshima nyumbani mwako? 1 Samweli 22:14

Then Ahimelech answered the king, and said, Who among all your servants is so faithful as David, who is the king's son-in-law, and is taken into your council, and is honorable in your house?

Je! Mimi nimeanza leo tu kumwuliza Mungu kwa ajili yake? Hasha! Mfalme asinidhanie mimi, mtumishi wake neno hili, Wala jamaa yote ya baba yangu, kwa maana mimi, mtumishi wako siyajui hayo yote, yaliyopungua au yaliyozidi. 1 Samweli 22:15

Have I today begun to inquire of God for him? be it far from me: don't let the king impute anything to his servant, nor to all the house of my father; for your servant knows nothing of all this, less or more.

Naye mfalme akasema, Kufa utakufa, Ahimeleki, wewe na jamaa yote ya baba yako. 1 Samweli 22:16

The king said, You shall surely die, Ahimelech, you, and all your father's house.

Kisha mfalme akawaambia askari walinzi waliosimama karibu naye Geukeni, mkawaue hao makuhani wa Bwana, kwa sababu mkono wao u pamoja na Daudi, na kwa sababu walijua ya kuwa amekimbia, wasiniarifu. Lakini watumishi wa mfalme walikataa kunyosha mkono na kuwaangukia makuhani wa Bwana. 1 Samweli 22:17

The king said to the guard who stood about him, Turn, and kill the priests of Yahweh; because their hand also is with David, and because they knew that he fled, and didn't disclose it to me. But the servants of the king wouldn't put forth their hand to fall on the priests of Yahweh.

Basi mfalme akamwambia Doegi, Geuka wewe, ukawaangukia hao makuhani. Basi Doegi, Mwedomi, akageuka, akawaangukia makuhani, akaua siku ile watu themanini na watano wenye kuvaa naivera ya kitani. 1 Samweli 22:18

The king said to Doeg, Turn you, and fall on the priests. Doeg the Edomite turned, and he fell on the priests, and he killed on that day eighty-five persons who wore a linen ephod.

Kisha akaupiga Nobu, mji wa makuhani, kwa makali ya upanga, wanaume na wanawake, watoto na wanyonyao, na ng'ombe, na punda, na kondoo. 1 Samweli 22:19

Nob, the city of the priests, struck he with the edge of the sword, both men and women, children and nursing babies, and oxen and donkeys and sheep, with the edge of the sword.

Na katika wana wa Ahimeleki, mwana wa Ahitubu, akaokoka mtu mmoja tu, aliyeitwa jina lake Abiathari, akamkimbilia Daudi. 1 Samweli 22:20

One of the sons of Ahimelech, the son of Ahitub, named Abiathar, escaped, and fled after David.

Naye Abiathari akamweleza Daudi ya kwamba Sauli amewaua makuhani wa Bwana. 1 Samweli 22:21

Abiathar told David that Saul had slain Yahweh's priests.

Daudi akamwambia Abiathari, Siku ile alipokuwako Doegi, Mwedomi, nalijua yakini ya kuwa atamwambia Sauli; mimi nimewapatia watu wote wa jamaa ya baba yako kifo. 1 Samweli 22:22

David said to Abiathar, I knew on that day, when Doeg the Edomite was there, that he would surely tell Saul: I have occasioned [the death] of all the persons of your father's house.

Kaa wewe pamoja nami, usiogope; kwa maana yeye atafutaye roho yangu, ndiye atafutaye na roho yako; nawe utakaa kwangu salama. 1 Samweli 22:23

Abide you with me, don't be afraid; for he who seeks my life seeks your life: for with me you shall be in safeguard.