1 Samweli 14 Swahili & English

Listen/Download Audio
1 Samweli 14 (Swahili) 1st Samuel 14 (English)

Basi ikatukia siku moja, ya kwamba Yonathani, mwana wa Sauli, akamwambia yule kijana aliyemchukulia silaha zake, Haya! Na tuwavukie Wafilisti ngomeni, pale ng'ambo ya pili. Walakini hakumwarifu babaye. 1 Samweli 14:1

Now it fell on a day, that Jonathan the son of Saul said to the young man who bore his armor, Come, and let us go over to the Philistines' garrison, that is on yonder side. But he didn't tell his father.

Naye Sauli alikuwa akikaa katika upande wa mwisho wa Giba, chini ya mkomamanga ulioko kwenye uga; na hao watu waliokuwa pamoja naye walipata watu mia sita; 1 Samweli 14:2

Saul abode in the uttermost part of Gibeah under the pomegranate tree which is in Migron: and the people who were with him were about six hundred men;

na Ahiya, mwana wa Ahitubu nduguye Ikabodi, mwana wa Finehasi, mwana wa Eli, kuhani wa Bwana huko Shilo, mwenye kuvaa naivera. Tena hao watu hawakujua ya kwamba Yonathani ameondoka. 1 Samweli 14:3

and Ahijah, the son of Ahitub, Ichabod's brother, the son of Phinehas, the son of Eli, the priest of Yahweh in Shiloh, wearing an ephod. The people didn't know that Jonathan was gone.

Na katikati ya mianya, ambayo Yonathani alitaka kuipitia ili kuifikilia hiyo ngome ya Wafilisti, palikuwa na genge la jabali upande huu, na genge la jabali upande huu; jina la moja liliitwa Bosesi, na jina la pili Sene. 1 Samweli 14:4

Between the passes, by which Jonathan sought to go over to the Philistines' garrison, there was a rocky crag on the one side, and a rocky crag on the other side: and the name of the one was Bozez, and the name of the other Seneh.

Hilo genge moja limesimama upande wa kaskazini, mbele ya Mikmashi, na hilo la pili upande wa kusini, mbele ya Geba. 1 Samweli 14:5

The one crag rose up on the north in front of Michmash, and the other on the south in front of Geba.

Basi, Yonathani akamwambia yule kijana aliyemchukulia silaha zake, Haya! Na twende tukawavukie ngomeni hao wasiotahiriwa; yamkini Bwana atatutendea kazi; kwa maana hakuna la kumzuia Bwana asiokoe, kwamba ni kwa wengi au kwamba ni kwa wachache. 1 Samweli 14:6

Jonathan said to the young man who bore his armor, Come, and let us go over to the garrison of these uncircumcised: it may be that Yahweh will work for us; for there is no restraint to Yahweh to save by many or by few.

Naye huyo mchukua silaha akamjibu, Fanya yote yaliyomo moyoni mwako; angalia, mimi hapa ni pamoja nawe, moyo wangu ni kama moyo wako. 1 Samweli 14:7

His armor bearer said to him, Do all that is in your heart: turn you, behold, I am with you according to your heart.

Ndipo Yonathani akasema, Tazama, sisi tutawavukia watu hawa, na kujidhihirisha kwao. 1 Samweli 14:8

Then said Jonathan, Behold, we will pass over to the men, and we will disclose ourselves to them.

Nao wakituambia hivi, Ngojeni, hata sisi tuwafikilie; ndipo tusimame pale pale mahali petu, tusiwapandie. 1 Samweli 14:9

If they say thus to us, Wait until we come to you; then we will stand still in our place, and will not go up to them.

Lakini wakisema hivi, Haya! Ninyi, tupandieni sisi; hapo ndipo tutakapopanda; kwa maana Bwana amewatia mikononi mwetu; na hii itakuwa ndiyo ishara kwetu. 1 Samweli 14:10

But if they say thus, Come up to us; then we will go up; for Yahweh has delivered them into our hand: and this shall be the sign to us.

Basi, hao wote wawili wakajidhihirisha mbele ya ngome ya Wafilisti, na wale Wafilisti wakasema, Kumbe! Wale Waebrania watoka katika mashimo walimojificha! 1 Samweli 14:11

Both of them disclosed themselves to the garrison of the Philistines: and the Philistines said, Behold, the Hebrews come forth out of the holes where they had hid themselves.

Nao watu wa ngomeni wakamjibu Yonathani na mchukua silaha zake, wakasema, Haya! Ninyi, pandeni juu hapa tulipo, na sisi tutawaonyesha jambo. Yonathani akamwambia yule aliyezichukua silaha, Haya! Panda nyuma yangu; kwa kuwa Bwana amewatia mikononi mwa Israeli. 1 Samweli 14:12

The men of the garrison answered Jonathan and his armor bearer, and said, Come up to us, and we will show you a thing. Jonathan said to his armor bearer, Come up after me; for Yahweh has delivered them into the hand of Israel.

Basi Yonathani akapanda kwa mikono na miguu yake, na mchukua silaha nyuma yake; na hao watu wakaanguka mbele ya Yonathani; na huyo mchukua silaha zake akawaua nyuma yake. 1 Samweli 14:13

Jonathan climbed up on his hands and on his feet, and his armor bearer after him: and they fell before Jonathan; and his armor bearer killed them after him.

Na uuaji huo wa kwanza walioufanya Yonathani na mchukua silaha zake, ulipata kama watu ishirini, katika nafasi kama nusu ya kiwanja kiwezacho kulimwa katika siku nzima. 1 Samweli 14:14

That first slaughter, which Jonathan and his armor bearer made, was about twenty men, within as it were half a furrow's length in an acre of land.

Kukawa na tetemeko katika marago, na katika mashamba, na katikati ya watu wote; watu wa ngomeni, na watekaji wa nyara, wakatetemeka nao; hata na nchi ikatetemeka pia; basi kulikuwa na tetemeko kubwa mno. 1 Samweli 14:15

There was a trembling in the camp, in the field, and among all the people; the garrison, and the spoilers, they also trembled; and the earth quaked: so there was an exceeding great trembling.

Nao wale walinzi wa Sauli huko Gibea ya Benyamini wakaangalia, na tazama, mkutano ule ulikuwa ukitoweka, na watu walikuwa wakienda huko na huko. 1 Samweli 14:16

The watchmen of Saul in Gibeah of Benjamin looked; and, behold, the multitude melted away, and they went [here] and there.

Ndipo Sauli akawaambia watu waliokuwa pamoja naye, Haya! Hesabuni sasa, mkaone ni nani aliyeondoka kwetu. Nao walipokwisha hesabu, tazama Yonathani na yeye aliyechukua silaha zake hawapo. 1 Samweli 14:17

Then said Saul to the people who were with him, Number now, and see who is gone from us. When they had numbered, behold, Jonathan and his armor bearer were not there.

Basi Sauli akamwambia Ahiya, Lilete hapa sanduku la Mungu. Kwa kuwa hilo sanduku la Mungu wakati huo lilikuwapo pamoja na wana wa Israeli 1 Samweli 14:18

Saul said to Ahijah, Bring here the ark of God. For the ark of God was [there] at that time with the children of Israel.

Ikawa Sauli alipokuwa katika kusema na kuhani, hayo makelele katika marago ya Wafilisti yakaendelea na kuzidi; basi Sauli akamwambia kuhani, Rudisha mkono wako. 1 Samweli 14:19

It happened, while Saul talked to the priest, that the tumult that was in the camp of the Philistines went on and increased: and Saul said to the priest, Withdraw your hand.

Naye Sauli na watu wote waliokuwapo pamoja naye wakakusanyika, wakaenda vitani; na tazama, huko upanga wa kila mtu ulikuwa juu ya mwenziwe, kukawa fujo tele kabisa. 1 Samweli 14:20

Saul and all the people who were with him were gathered together, and came to the battle: and, behold, every man's sword was against his fellow, [and there was] a very great confusion.

Basi na wale Waebrania waliokuwa pamoja na Wafilisti tangu zamani, wale waliopanda pamoja nao mpaka maragoni toka nchi iliyozunguka; watu hao nao wakageuka kuwa upande wa Waisraeli waliokuwa pamoja na Sauli na Yonathani. 1 Samweli 14:21

Now the Hebrews who were with the Philistines as before, and who went up with them into the camp, [from the country] round about, even they also [turned] to be with the Israelites who were with Saul and Jonathan.

Na vile vile watu wote wa Israeli waliokuwa wamejificha katika nchi ya milima milima ya Efraimu, waliposikia ya kwamba Wafilisti wamekimbia, hata hao nao wakawafuatia mbio vitani. 1 Samweli 14:22

Likewise all the men of Israel who had hid themselves in the hill-country of Ephraim, when they heard that the Philistines fled, even they also followed hard after them in the battle.

Hivyo Bwana akawaokoa Israeli siku ile; na vita vikapita mbele karibu na Beth-aveni. Wakati huo mbele ya wana wa Israeli. 1 Samweli 14:23

So Yahweh saved Israel that day: and the battle passed over by Beth Aven.

Nao watu wa Israeli walisumbuka sana siku ile; lakini Sauli alikuwa amewaapisha watu, akisema, Na alaaniwe mtu awaye yote alaye chakula cho chote hata jioni, nipate kujilipiza kisasi juu ya adui zangu. Basi hakuna mtu miongoni mwa watu aliyeonja chakula. 1 Samweli 14:24

The men of Israel were distressed that day; for Saul had adjured the people, saying, Cursed be the man who eats any food until it be evening, and I be avenged on my enemies. So none of the people tasted food.

Nao watu wote wakaingia mwituni; na humo mlikuwa na asali juu ya nchi. 1 Samweli 14:25

All the people came into the forest; and there was honey on the ground.

Na hapo watu walipokwisha kuingia mwituni, tazama, hiyo asali ilikuwa ikidondoka; walakini hakuna mtu hata mmoja aliyetia mkono wake kinywani; kwa sababu hao watu walikuwa wakikiogopa kile kiapo. 1 Samweli 14:26

When the people were come to the forest, behold, the honey dropped: but no man put his hand to his mouth; for the people feared the oath.

Ila Yonathani hakusikia, hapo babaye alipowaagiza watu kwa kiapo; basi yeye akainyosha ncha ya fimbo iliyokuwa mkononi mwake, na kuichovya katika sega la asali, kisha akatia mkono wake kinywani; na macho yake yakatiwa nuru. 1 Samweli 14:27

But Jonathan didn't hear when his father charged the people with the oath: therefore he put forth the end of the rod who was in his hand, and dipped it in the honeycomb, and put his hand to his mouth; and his eyes were enlightened.

Ndipo mmojawapo wa watu akamjibu, akasema, Baba yako aliwaagiza watu sana kwa kiapo, akisema, Na alaaniwe mtu alaye chakula leo. Na hao watu walikuwa wamepungukiwa na nguvu. 1 Samweli 14:28

Then answered one of the people, and said, Your father directly charged the people with an oath, saying, Cursed be the man who eats food this day. The people were faint.

Ndipo Yonathani akasema, Babangu ameifadhaisha nchi; tafadhali, angalia jinsi macho yangu yalivyotiwa nuru, kwa sababu nalionja asali hii kidogo. 1 Samweli 14:29

Then said Jonathan, My father has troubled the land. Please look how my eyes have been enlightened, because I tasted a little of this honey.

Je! Si zaidi sana, kama watu wangalikula na kushiba leo katika nyara hizi za adui zao walizoziteka? Kwa maana haukuwa uuaji mkuu sasa katikati ya Wafilisti. 1 Samweli 14:30

How much more, if haply the people had eaten freely today of the spoil of their enemies which they found? for now has there been no great slaughter among the Philistines.

Nao wakawapiga watu miongoni mwa Wafilisti siku ile kutoka Mikmashi mpaka Ayaloni; na hao watu walikuwa wamepungukiwa sana na nguvu. 1 Samweli 14:31

They struck of the Philistines that day from Michmash to Aijalon. The people were very faint;

Basi watu wakazirukia zile nyara, wakatwaa kondoo, na ng'ombe, na ndama, na kuwachinja papo hapo juu ya nchi, nao wale watu walikuwa wakiwala pamoja na damu. 1 Samweli 14:32

and the people flew on the spoil, and took sheep, and oxen, and calves, and killed them on the ground; and the people ate them with the blood.

Ndipo wakamwambia Sauli, wakisema, Angalia, watu hao wanakosa juu ya Bwana, kwa jinsi wanavyokula pamoja na damu. Naye akasema, Ninyi mmefanya kwa hiana; vingirisheni kwangu leo jiwe kubwa. 1 Samweli 14:33

Then they told Saul, saying, Behold, the people sin against Yahweh, in that they eat with the blood. He said, you have dealt treacherously: roll a great stone to me this day.

Kisha Sauli akasema, Haya! Tawanyikeni katikati ya watu mkawaambie, Nileteeni hapa kila mtu ng'ombe wake, na kila mtu kondoo wake, mkawachinje hapa na kula; wala msikose juu ya Bwana, kwa kula pamoja na damu. Nao watu wote wakaleta kila mtu ng'ombe wake pamoja naye usiku ule, nao wakawachinja hapo. 1 Samweli 14:34

Saul said, Disperse yourselves among the people, and tell them, Bring me here every man his ox, and every man his sheep, and kill them here, and eat; and don't sin against Yahweh in eating with the blood. All the people brought every man his ox with him that night, and killed them there.

Naye Sauli akamjengea Bwana madhabahu; hiyo ndiyo madhabahu ya kwanza aliyomjengea Bwana. 1 Samweli 14:35

Saul built an altar to Yahweh: the same was the first altar that he built to Yahweh.

Kisha Sauli akasema, Haya! Na tushuke kuwafuata Wafilisti wakati wa usiku, na kuwateka nyara hata mapambazuko, wala tusiwaache hata mmoja wao. Nao wakamjibu, Fanya yo yote uyaonayo kuwa ni mema. Ndipo yule kuhani akasema, Na tumkaribie Mungu hapa. 1 Samweli 14:36

Saul said, Let us go down after the Philistines by night, and take spoil among them until the morning light, and let us not leave a man of them. They said, Do whatever seems good to you. Then said the priest, Let us draw near here to God.

Basi Sauli akataka shauri kwa Mungu, Je! Nishuke ili kuwafuatia Wafilisti? Je! Utawatia mikononi mwa Israeli? Lakini hakumjibu neno lo lote siku ile. 1 Samweli 14:37

Saul asked counsel of God, Shall I go down after the Philistines? will you deliver them into the hand of Israel? But he didn't answer him that day.

Ndipo Sauli akasema, Karibieni hapa, enyi wakuu wote wa watu; mjue na kuona dhambi hii ya leo imekuwa katika kosa gani. 1 Samweli 14:38

Saul said, Draw near here, all you chiefs of the people; and know and see in which this sin has been this day.

Kwa maana, aishivyo Bwana, awaokoaye Israeli, ijapokuwa i katika Yonathani, mwanangu, kufa atakufa. Lakini miongoni mwa watu wote hakuna mtu ye yote aliyemjibu. 1 Samweli 14:39

For, as Yahweh lives, who saves Israel, though it be in Jonathan my son, he shall surely die. But there was not a man among all the people who answered him.

Ndipo akawaambia Israeli wote, Ninyi mtakuwa upande mmoja, na mimi na mwanangu Yonathani tutakuwa upande wa pili. Basi wakamwambia Sauli, Fanya uonayo kuwa ni mema. 1 Samweli 14:40

Then said he to all Israel, Be you on one side, and I and Jonathan my son will be on the other side. The people said to Saul, Do what seems good to you.

Kwa hiyo Sauli akamwambia Bwana, Mungu wa Israeli, [Kwani usimjibu mtumishi wako leo? Ikiwa dhambi i ndani yangu, au ndani yake Yonathani mwanangu, Ee Bwana, Mungu wa Israeli, utoe Urimu; bali ukisema hivi, Dhambi i katika watu wako Israeli,] utoe Thumimu ,Basi Yonathani na Sauli wakatwaliwa,lakini watu wakapona. 1 Samweli 14:41

Therefore Saul said to Yahweh, the God of Israel, Show the right. Jonathan and Saul were taken [by lot]; but the people escaped.

Basi Sauli akasema, Sasa piga kati ya mimi na mwanangu Yonathani, [naye awaye yote ambaye Bwana atamtwaa, atakufa. Nao watu wakamwambia Sauli, La! Sivyo hivyo; lakini Sauli akawaweza watu. Nao wakapiga kati ya yeye na mwanawe Yonathani,] 1 Samweli 14:42

Saul said, Cast [lots] between me and Jonathan my son. Jonathan was taken.

Ndipo Sauli akamwambia Yonathani, Niambie ulilolifanya. Basi Yonathani akamwambia, akasema, Ni kweli, mimi nalionja asali kidogo kwa ncha ya fimbo ile iliyokuwa mkononi mwangu; na tazama, imenipasa kufa. 1 Samweli 14:43

Then Saul said to Jonathan, Tell me what you have done. Jonathan told him, and said, I did certainly taste a little honey with the end of the rod that was in my hand; and, behold, I must die.

Naye Sauli akasema, Mungu anifanyie hivi, na kuzidi; kwa kuwa hakika utakufa, Yonathani. 1 Samweli 14:44

Saul said, God do so and more also; for you shall surely die, Jonathan.

Walakini watu wakamwambia Sauli, Je! Atakufa Yonathani, ambaye ndiye aliyeufanya huo wokovu mkuu katika Israeli? Hasha! Aishivyo Bwana, hautaanguka chini hata unywele mmoja wa kichwa chake; kwa maana ametenda kazi pamoja na Mungu leo. Hivyo hao watu wakamponya Yonathani, asife. 1 Samweli 14:45

The people said to Saul, Shall Jonathan die, who has worked this great salvation in Israel? Far from it: as Yahweh lives, there shall not one hair of his head fall to the ground; for he has worked with God this day. So the people rescued Jonathan, that he didn't die.

Ndipo Sauli akakwea kuacha kuwafuata Wafilisti; nao Wafilisti wakaenda zao kwao. 1 Samweli 14:46

Then Saul went up from following the Philistines; and the Philistines went to their own place.

Basi Sauli alipokwisha kuutwaa ufalme juu ya Israeli, alipigana na adui zake zote pande zote, juu ya Moabu, na juu ya wana wa Amoni, na juu ya Edomu, na juu ya wafalme wa Soba, na juu ya Wafilisti; na po pote alipogeukia, akawashinda. 1 Samweli 14:47

Now when Saul had taken the kingdom over Israel, he fought against all his enemies on every side, against Moab, and against the children of Ammon, and against Edom, and against the kings of Zobah, and against the Philistines: and wherever he turned himself, he put [them] to the worse.

Naye akatenda kwa ushujaa, akawapiga Waamaleki, na kuwaokoa Waisraeli katika mikono yao waliowateka nyara. 1 Samweli 14:48

He did valiantly, and struck the Amalekites, and delivered Israel out of the hands of those who despoiled them.

Basi, wana wa Sauli walikuwa ni hawa, Yonathani, na Ishvi, na Malkishua; na majina ya binti zake wawili yalikuwa haya; jina lake wa kwanza aliitwa Merabu, na jina lake mdogo aliitwa Mikali; 1 Samweli 14:49

Now the sons of Saul were Jonathan, and Ishvi, and Malchishua; and the names of his two daughters were these: the name of the firstborn Merab, and the name of the younger Michal:

na jina lake mkewe Sauli aliitwa Ahinoamu, binti Ahimaasi. Tena, jina la jemadari wa jeshi lake aliitwa Abneri, mwana wa Neri, aliyekuwa baba mdogo wa Sauli. 1 Samweli 14:50

and the name of Saul's wife was Ahinoam the daughter of Ahimaaz. The name of the captain of his host was Abner the son of Ner, Saul's uncle.

Na Kishi, babaye Sauli, na Neri, babaye Abneri, walikuwa wana wa Abieli. 1 Samweli 14:51

Kish was the father of Saul; and Ner the father of Abner was the son of Abiel.

Tena, kulikuwa na vita vikali sana juu ya Wafilisti siku zote za Sauli, naye Sauli alipomwona mtu ye yote aliyekuwa hodari, au mtu ye yote aliyekuwa shujaa, humtwaa ili awe pamoja naye. 1 Samweli 14:52

There was sore war against the Philistines all the days of Saul: and when Saul saw any mighty man, or any valiant man, he took him to him.